Kijana aliyetambulika kwa jina la Musa Mbeko(24) anayedaiwa kuwa ni mwandishi wa habari mkoani Tabora akiwa mikononi mwa Jeshi la Polisi mkoani humo baada ya kujifanya kuwa ni afisa kutoka idara ya usalama wa taifa (TISS). Kijana huyo inadaiwa aliwahi kufanya kazi kituo cha radio cha Voice of Tabora (VOT) kinachomilikiwa na mbunge wa Jimbo la Tabora mjini, Mhe. Ismail Aden Rage. Hata hivyo Uongozi wa VOT umekana kijana huyo kuwa ni mwandishi wao na kwamba ulikwisha mfukuza kazi kutokana na makosa mbalimbali yakiwemo ya tuhuma za utapeli
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda akiwaonesha waandishi wa habari kitambulisho kilichokuwa kikitumiwa na Mussa Mbeko akijifanya ni Afisa Usalama wa Taifa.
 . 
Kitambulisho alichokuwa akitumia kijana Musa Mbeko.
Kijana Musa Mbeko akiwa mbele ya kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzana Kaganda.

Kijana Musa Mbeko akiwa chini ya Ulinzi 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 23, 2014

    So Sad. Si wamsaidie tu ajiunge na idara kama yeye ndo anaifia hiyo kazi!!! Maana nadhani ataifanya kwa umahiri sana kwani ndo ndoto yake pengine. Pole kijana usiwe unadanganya. Kote duniani ukiwa mwongo utajikuta katika hali mbaya. Jifunze kutoka kosa hili.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 24, 2014

    Vijana siku hizi ndo imekuwa deal, mnatusumbua sana huko kwenye mabaa kidogo tu unanijua mimi nitakupoteza ooh, huyu sasa naye ameshindwa hata kujitambua mana hicho kitambulisho kimechanganywa lugha si mchezo, hapo kwen=li ni Tabora mwanawane mh

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...