Na Rose Masaka MAELEZO-Dar es Salaam

TAASISI ya  Hawzat Imam Swadiq wameandaa maandamano ya kulaani mashambulizi yanayofanywa na Vikosi vya Israel dhidi ya wananchi wa Palestina wasio na hatia.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Taasisi hiyo Profesa Abdul Shariff, maandamano hayo yanalenga kuueleza ulimwengu kuwa wananchi wa Tanzania wanalaani mauaji yanayoendelea huko Gaza Palestina.

Amesema kuwa maandamano hayo  ambayo yatafanyika siku ya Ijumaa  Julai 25 mwaka huu yanatarajia kuanzia Kituo cha Daladala cha Boma na kuishia Kigogo uwanja wa Bibo.

Profesa Shariff ameongeza kuwa wameamua kupaza sauti zao kulaani baada ya kuona Jumuiya mbalimbali za Kimataifa ikiwa imenyamaza huku mamia ya watu wakizi kupoteza maisha yao.

Amesema kuwa inasikitisha kuona hata vyombo vya habari hasa vya Magharibi havitoi nafasi kubwa kwa mauaji hayo ukilinganisha na mauaji yaliyotokea kwa kulipuliwa kwa ndege Malyasia.

Naye Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Sheikh Hamed Jalala amesema kuwa wamealika viongozi na Mabalozi wa Nchi mbalimbali ili nao waweze kushiriki katika  kupaza sauti zao pamoja na watanzania kulaani vitendo vinavyofanywa na Israel vya kuua watu wasio na hatia.

Sheikh Jalala amesema kuwa kunyamazia tatizo hilo ni kufanya kosa kwani hakuna hata dini moja inaruhusu mauaji ya binadamu mwingine.

Amesema kuwa maandamano  hayo yatahusisha watu wa dini zote na yamepata Kibali cha Mamlaka husika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 23, 2014

    Michuzi usibanie hii.
    Cha kushangaza hao wapalestina kwa siku wanafyatua makombora zaidi ya 1000 Israel. Licha ya kuwa Israel ina technologia ya kuyazuia lakini Wapalestina wakipewa mkongoto wanatafuta huruma ya dunia. Israel inawatafuta Hamas ambao wanajificha uraiani na wanatumia raia wa kawaida kama kinga. Vilevile wanavyowafyatulia Waislaeli makombora siyo yadondokee kwenye makambi ya jeshi bali uraiani yakauwe raia wa Isarael wasio na hatia. Unazi huu wa kushabikia ujinga hautupeleki popote. Mbona Wapalestina wa Ramallah wanakula kuku kwani toka enzi za Arafat walikubalian na Waislaeli. Bwana Profesa profesi amani kuliko kushabikia.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 24, 2014

    Shut up wee anonymous wa hapo juu. Mambo ya ngoswe muachie mwenyewe

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 24, 2014

    shutup na wewe anonymous, kama ya Ngoswe wamuachie Ngoswe, hata hawa wanaoandamana wangekaa ndani !

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...