Mwili wa Marehemu Sydney Damson ambaye aliyekuwa Mhadhiri wa Chuo cha Uhasibu Dar es Salaam(sasa kikijulikana Taasisi ya Uhasibu Tanzania) ukiwasili nyumbani kwake Tandika Magorofani, Wilayani Temeke tayari kwa taratibu za kuaga kabla ya kwenda mazikoni.
Mchungaji wa Kanisa la Moravian, Mchungaji Mwakalinga(kushoto) akiendesha Ibada Maalum ya kumuombea Marehemu Sydney Damson kabla ya zoezi la kuuaga mwili wa Marehemu kuanza nyumbani kwake Tandika Magorofani leo Julai 27, 2014 Temeke Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kulia aliyeketi) ni Mtoto wa kwanza wa Marehemu ambaye ni Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Masokola Damson.
Baadhi ya Watu waliojitokeza kuuaga mwili wa aliyekuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Uhasibu Dar es Salaam(TIA) wakimsikiliza Mchungaji wakati wa Ibada Maalum ya kumuombea Marehemu iliyofanyika nyumbani kwake Tandika Magorofani, Temeke Jijini Dar es Salaam.
Mke wa Marehemu Sydney Damson akisindikizwa na ndugu na jamaa kuuaga mwili wa Marehemu.
Mtoto wa Marehemu, John Damson akiweka Shada la Maua katika kaburi Baba yake baada ya kukamilisha taratibu za mazishi katika Makaburi ya Wireless, Temeke Jijini Dar es Salaam.
Umati wa ndugu na jamaa waliojitokeza katika mazishi ya aliyekuwa Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Uhasibu Dar es Salaam(TIA) Marehemu Sydney Damson ambaye amezikwa leo Julai 27, 2014 katika Makaburi ya Wireless, Temeke Jijini Dar es Salaam(Picha na Lucas Mboje).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...