Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu (kulia) akimsikiliza kwa makini mshindi wa milioni 100/-kupitia promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na kampuni hiyo Bi.Uwezo Magedenge (22) akimfafanulia jambo kuhusiana na ushindi wake,wakati alipomtembelea kijijini kwao Pamilini Kilolo mkoa wa Iringa kwa ajili ya kumchukua na kumpeleka jijini Dar es Salaam, kwa makabidhiano rasmi ya kitita chake hivi karibuni.Wengine katika picha kushoto ni Mama yake mzazi Delfine Kisoma(64) na Baba yake Alatanga Magendenge (70).
Baba mzazi wa mshindi wa kwanza wa milioni 100 kupitia promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania, Alatanga Magendenge akimfafanulia jambo Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo Matina Nkurlu(kulia) kuhusiana na ushindi wa mwanae Uwezo Magendenge(watatu toka kushoto)wakati alipomtembelea mshindi huyo nyumbani kwao kijiji cha Pamilini Kilolo Iringa kwa ajili ya kumchukua na kumpeleka Dar es Salaam kwa ajili ya kumkabidhi rasmi ya kitita chake hivi karibuni,kushoto ni mama mzazi wa mshindi Delfine Kisoma.
Mshindi wa Milioni 100/- kupitia promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania,Bi. Uwezo Magedenga (kushoto) akifurahia jambo na Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kulia)wakati alipofika kijijini kwao Pamilini Kilolo Iringa ili kujua mazingiara yake na kumpeleka jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kwa ajili ya kumkabidhi rasmi ya kitita chake hivi karibuni. Katikati ni Mkuu wa kampuni hiyo Kanda ya Kusini magharibi Amos Vuhahula.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Msichana huyu apatiwe ushauri jinsi ya kutumia pesa, la sivyo hatajua jinsi ya kuzitumia, kuboresha maisha ya jamii yake na kuwekeza ili ziendelee kumsaidia yeye na jamii yake.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...