KUFUATIA mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Msimu wa Pili wa Coke Studio Africa, Kampuni ya Coca-Cola kwa kushirikiana na Shirika la Ndege la Kenya, inayo furaha kutangaza kuanza tena msimu wa tatu wa burudani ya muziki maarufu kwa jila la Coke Studio Africa. msimu huu utajumuisha wanamuziki wakali 26 barani Afrika huku nyimbo mpya 52 kutumbuizwa ikiambatana na maonyesho 9 ya wanamuziki wanaotamba hapa duniani. 

Maonyesho hayo ya muziki ya Coke Studio Africa ni tofauti na mengine ya aina hiyo yanayolenga zaidi kupatikana mshindi. Badala yake, maonyesho haya yanalenga kujumuisha pamoja vipaji tofauti vya wanamuziki mbalimbali kutoka barani Afrika. Aidha, yanatoa fursa kwa wasanii wanaochipukia kufanya pamoja kazi zao na wanamuziki nguli wa ndani na wale wa ngazi za kimataifa.
Alikiba
Msimu huu unaozinduliwa utawakutanisha wanamuziki kutoka katika nchi za Tanzania, Msumbiji, Kenya, Uganda na Nigeria, na kwa mara ya kwanza wasanii hawa wataweza kukonga nyoyo za wapenzi wa muziki kwa kushirikiana katika staili ya kipekee ijulikanayo kama mash-ups – ambayo inatawala kwa sasa katika tasnia ya muziki duniani. “Kufurahia muziki wa Kiafrika” ikiwa ndiyo kiini kikuu cha burudani hiyo, msimu huu mpya wa Coke Studio Africa utawakutanisha wasanii maarufu ambao wameonyesha mafanikio makubwa katika kazi zao, na pia maonyesho hayo yatawaleta pamoja wasanii nyota wanaochipukia katika ulimwengu wa muziki.

Chini ya ushirikiano huo mpya na Kampuni ya Coca-Cola, Shirika la Ndege la Kenya kwa upande wake litawasafirisha wasanii wote na waandaaji wa muziki wanaoshiriki katika Msimu wa Tatu wa Coke Studio Africa. Mpango huo wa ushirikiano wa makampuni haya makubwa unatokana na imani ya kwamba hatua hiyo itajenga msingi wa ubia muhimu wa kufanya kazi kwa pamoja.
Vanessa Mdee

Akizungumzia juu ya Coke Studio Africa Msimu wa Tatu, Meneja Bidhaa wa Coca-Cola Tanzania, Maurice Njowoka alisema: “Lengo letu ni kuufanya na kuwezesha namna ambayo muziki unavyoweza kuchukua nafasi katika kukonga nyoyo za watu katika Bara letu. Coke Studio Msimu wa Tatu si kwa ajili ya kuwakutanisha tu wanamuziki wa Afrika, bali pia maonyesho haya yanatoa fursa ya pekee ya ushirikiano ambao ni imani yetu kuwa wateja wetu pamoja na umma kwa ujumla wangependa kuusikia.”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...