Mwenyekiti wa Bodi ya AICC na Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya wiki ya Ukombozi wa Bara la Afrika, Balozi Christopher Liundi akikata utepe katika maadhimisho hayo ikiwa leo ni siku ya Kuona Mchango wa Wanawake katika Ukombozi wa Bara la Afrika, maadhimisho hayo yamefanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Profesa Ruth Meene akizungumza na baadhi ya wanafunzi na watu wengine waliohudhuria (hawapo pichani) ili kujua mchango wa wanawake katika ukombozi wa Bara la Afrika, wanawake hao ambao wamesaidia zaidi ni Mke wa Rais wa Mozambiq,Jocina Machel,Bi Ndaitwa wa Namibia,Winnie Mandela wa Afrika Kusini,Albetina Kisulu,Elizabeth Sebeko,Mariam Makeba wote wa Afrika kusini  na hapa nchini ni Bibi Titi Mohamed,Lucy Maulid na Sophia Kawawa ambao walikuwa wakihamasisha wananchi Kisiasa katika kulikomboa Bara la Afrika.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Victoria waliohudhuria katika Mkutano wa kujua jinsi wanawake walivyoshiriki katika kulikomboa Bara la Afrika, katika Mkutano uliofanyika Makumbusho ya Taifa jijiji Dar es Salaam leo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya AICC na Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya wiki ya Ukombozi wa Bara la Afrika, Balozi Christopher Liundi akizungumza leo na waandishi wa habari mara baada ya kutoka katika kumbi zenye  picha na vitu mbalimbali ndani ya jengo la Makumbusho ya Taifa vinavyoonyesha kumbukumbu ya matukio mbalimbali yalivyowahi kutokea hapa nchini.Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...