Mheshimiwa Uhuru Kenyatta Rais wa Jamuhuri ya Kenya akimpongeza na kumkaribisha rasmi Mheshimiwa Balozi John Michael Haule mara baada ya kupokea Hati zake rasmi za utambulisho.
Mheshimiwa John Michael Haule, Balozi wa Tanzania nchini Kenya akiteta jambo na Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta wa Jamuhuri ya Kenya mara baada ya kuwasilisha Hati za utambulisho.
Mheshimiwa Balozi John Michael Haule akiwa kwenye picha ya pamoja na Mabalozi wengine waliowasilisha Hati zao za utambulisho kwa Mheshimiwa Uhuru Kenyatta, Rais wa Jamhuri ya Kenya.
Mheshimiwa Balozi John Michael Haule akipokea shada la maua kutoka kwa Mke wake, Bibi Mary John Haule mara baada ya kuwasili kwenye makazi yake, Muthaiga 81 akitokea Ikulu ya Nairobi baada ya kuwasilisha Hati zake za utambulisho kwa Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta.
Whenever i see a picture of honorable Haule is like i see diluted version of comrade Mugabe........look like brothers.
ReplyDelete