Na  Bashir  Yakub. 

Nilipoandika  kuhusu  namna  ya  kuunda kampuni  kwa  mujibu  wa  Sheria ya  Makampuni  sura ya 212 nilieleza  pia   kuwa   unapokuwa  umekamilisha  usajili  wa  kampuni     na  umepata  cheti  cha  usajili   yapo  mambo  mengine  ya  kufanya  kabla  ya  kuanza  rasmi  biashara. 

Moja  ya  mambo  hayo  nilisema   ukishapata  cheti unatakiwa  uende  manispaa  husika  ukapate  leseni  ya  biashara. Manispaa husika  ni  manispaa  ambako  ofisi  ya  kampuni  yako  itakuwa.  Kitu  kingine  baada ya  kupata  cheti  cha usajili  ni  kupata  namba  ya  mlipa  kodi (TIN). Ili  kampuni  ifanye  biashara  kisheria  inatakiwa  kuwa imepata  namba  hii.  

Yawezekana  wanahisa  kila  mmoja  anayo  namba  yake ya  mlipa  kodi   lakini  namba  hizo  haziwezi kutumika  kwakuwa  ni  za  watu  binafsi  na  si  za  kampuni.  Kampuni  inatakiwa  ipate namba  yake  inayojitegemea.  Halikadhalika  kwa  wanaoanzisha  vikundi kwa  mfano  saccos, na asasi  za  kiraia( NGOs) nao wanatakiwa  kuwa  na  namba  ya  mlipa kodi  ya  vikundi  hivyo. 

1.TIN  NAMBA  HUPATIKANA  WAPI.

Mamlaka  ya  mapato  Tanzania ( TRA) ndiyo  mamlaka  inayoshughulika  na  utoaji  wa  namba  za  mlipa  kodi. Awali  namba  hizi  zilikuwa  zikitolewa  makao  makuu  ya  mamlaka  ya  mapato ambapo  kwasasa  katika  kuboresha  huduma    wameweka  ofisi  za  kikanda  sehemu  mbalimbali  ambazo  huhudumia   wahitaji  wa  kanda  husika  kwa  mfano  kwa  Dar  es  salaam  eneo  la  ilala , buguruni, tabata, kariakoo  ofisi  zipo  makutano  ya  Shaurimoyo badala  ya  mnazi  mmoja  au  samora . Hata  hivyo   yapo  maeneo  mengine  ambayo  ofisi  za  kanda  hazijawekwa  kwa  mfano  mikoani  ambapo  wahitaji  hulazimika  kufuata  huduma  hii  makao  makuu  ya  mamlaka  ya  mapato.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...