Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon, akiwa na Mabalozi Macharia Kamau wa Kenya na David Donoghue wa Ireland wakati walipozungumza na waandishi wa habari kuelezea namna mchakato wa majadiliano yaliyokamilisha na hatimaye kupitishwa nan chi wanachama Tamko kuhusu Ajenda za Maendeleo Endelevu baada ya 2015. Tamko hilo lilipitishwa jumapili usiku. Mabalozi wao ndio waliosimamia mchakato mzima wa majadiliano hayo.
Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi, muda mfupi baada ya kuahirishwa mkutano kwa mapunziko mafupi hapo siku ya ijumaa usiku na kisha mkutano kuendelea tena hadi alfajiri ya Jumamosi, wakarejea tena mchana na kuendelea tena hadi usiku wa kuamkia jumapili na kuendelea jumpily mchana hadi usiku walilopitisha tamko hilo. Pamoja na naye Mkurungenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestin Mushy.
Afisa Mkuu Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Bw.Songelael Shilla ambaye amekuwa akisimamia mchakato wa majadiliano yaliyopelekea kupatika kwa ajenda mpya za maendeleo endelevu baada ya 2015, aliyeketi nyuma ni Dk. Lorah Madete kutoka Tume ya Mipango hii ilikuwa ni Ijumaa usiku.

Baaada ya  majadiliano  makali yaliyodumu kwa wiki mbili  na wakati mwingine wajumbe  kulazimika kukesha hadi asubuhi. Hatimaye nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa,     Jumapili   usiku (Agosti mbili), wamepitisha kwa kauli moja,  rasimu ya  tamko kuhusu  Agenda ya  Malengo ya Maendeleo  Endelevu  2015.

 Katika kuhakikisha kwamba  ilikuwa ni lazima  tamko hilo likamilike na kupitishwa,  wajumbe walilazimika kukesha ndani ya  ukumbi wa mkutano  kulikokuwa kukifanyika  mkutano huo,  wakipimzika  kwa saa chache na kurejea tena na hatimaye kufanikisha kukamilishwa kwa raslimu hiyo siku ya jumapili majira ya usiku.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiongozwa na  Mwakilishi wa Kudumu Balozi Tuvako  Manongi na Afisa Mkuu  Bw. Shilla,  kwa kushirikiana  na    wataalamu  kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,   wakiongozwa na Mkurugenzi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi Celestin Mushy,  Wataalamu kutoka  Tume ya  Rais Mipango,  Tanzania   Bara na Visiwani,   Wizara ya Fedha na  Asasi zisizo za Kiserikali,  imeshiriki kikamilifu katika  kipindi chote  miaka miwili  tangu kuanza kwa  mchakato wa majadiliano  hayo.

Tamko lilolopitishwa  i   Jumapili,   itawasilishwa mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa katika  tarehe  itakayopangwa   kupitishwa   rasmi.

Viongozi Wakuu wa Nchi na  Serikali watapokea na  kupitisha tamko hilo katika mkutano wao   wa Kihistoria utakaofanyika mwezi  ujao (  25-27Septemba) hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.

Akionyesha kufurahishwa na kuridhika kwake baada ya  wajumbe  kupitisha tamko hilo  , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, licha ya kuwapongeza wajumbe kwa kazi kubwa , kujituma kwao na zaidi kupitisha  rasimu hiyo kwa kauli moja,  amesema  anasubiri kwa hamu kuungana na Viongozi  Wakuu wa  Nchi na Serikali  zaidi ya 150 na  wawakilishi wengine katika mkutano  wa kilele utakaopitisha  za ajenda hizo za maendeleo endelevu kwa miaka 15 ijayo.

Akasema   mchakato mzima wa majadiliano ya maandalizi ya  tamko hilo ambao umedumu  kwa miaka miwili   umefanyika kwa   mshikamano,  weledi na ulikuwa shirikishi , ambapo hata makundi mbalimbali ya kijamii,  yalishiriki kwa ukamilifu.

Ban Ki  Moon, amesema,  ajenda mpya za maendeleo endelevu ambazo zinachukua nafasi ya  Malengo ya  Maendeleo ya Millenia  yanayofikia ukingoni mwaka huu, zinalenga katika kuwaondoa watu kutoka  katika  lindi la umaskini  pasipo kumwacha  yeyote.

“Napenda kuwapongeza nchi wanachama kwa uongozi wenu na kujituma kwenu, nawashukuru pia Mabalozi   Macharia Kamau  wa Kenya na   David Donoghue wa Ireland  kwa namna   walivyoendesha na kuusimamia mchakato huo bila  kuchoka na kwa kuonyesha  ufundi mkubwa  wa  kidiplomasia ” amesema Ban  Ki Moon.

 Na kuongeza kwamba Ajenda hiyo iitwayo: "kubadili dunia yetu: ajenda ya mwaka 2030 kwa maendeleo endelevu" inajumuisha masuala yanayowahusu wote ikilenga pia kuhakikisha Amani, ufanisi na kubuni ubia unaojali watu na sayari duni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Juhudi kubwa lakini utekelezaji vipi? Malengo ya milenia wametuuza. Ukweli maendeleo ni watu wenyewe tusitegemee misaaada!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...