Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete akipokewa na Mama Zakhia Meghji, Makamu Mwenyekiti wa WAMA wakati alipowasili nyumbani kwa Marehemu Mama Hulda Kibacha, Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA aliyefariki dunia tarehe 28.8.2015.
 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akishiriki kwenye ibada ya kumwombea Marehemu Hulda Kibacha, Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA iliyofanyika nyumbani kwa marehemu eneo la Ada Estate tarehe 2.9.2015. Aliyekaa kushoto kwa Mama Salma ni Mheshimiwa Zakhia Meghji na kulia ni binti wa marehemu Nampombe Kibacha.
 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka udongo kaburini wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mdhamini wa Taasisi ya WAMA Mama Hulda Kibacha aliyefariki dunia tarehe 28.8.2015 hapa Dar Es Salaam. Marehemu Kibacha aliwahi kufanya kazi Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).  
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiweka udongo kaburini ulimolazwa mwili wa Mama Hulda Kibacha aliyekuwa Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA. Marehemu Hulda Kikbacha alizikwa kwenye makaburi ya Kinondoni tarehe 2.9.2015.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (katikati) kwa kushirikiana na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha Rose Migiro (kushoto) na Mama Zakhia Meghji (kulia) wakiweka shada la maua kwenye kaburi LA Marehemu Hulda Kibacha aliyezikwa katika makaburi ya Kinondoni tarehe 2.9.2015.
 Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka shada la maua kwenye kaburi la Marehemu Hulda Kibacha.
 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya WAMA, Ndugu Zakhia Meghji akitoa salamu maalum za Taasisi hiyo wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mdhamini na Mjumbe wa Bodi hiyo Marehemu Hulda Kibacha.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiaagana na Binti wa Marehemu Nampombe Kibacha mara baada ya Mazishi ya Mdhamini na Mjumbe wa Bodi ya WAMA, Mama Hulda Kibacha.
PICHA NA JOHN LUKUWI. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...