Marafiki mbalimbali wa Programu ya Wafanye Watabasamu, hivi karibuni wamejitwalia zawadi za michoro ya ukutani iliyochorwa na Mchora vibonzo maarufu ambaye pia ni Mratibu wa programu hiyo, Nathan Mpangala aka Kijasti, baada ya kuposti mara nyingi kwenye mitandao ya kijamii bango lililokuwa likihamasisha watu kujitokeza kwa wingi kwenye onesho la michoro lililoandaliwa na Nafasi Art Space ya jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita. Pichani Mpangala aliyevaa suruali ya rangi ya Wekundu wa Msimbazi, akimkabidhi zawadi Mjasiriamali, Bi. Joyce Athanas huku wakishuhudiwa na marafiki mbalimbali hivi karibuni. Wengine Waliojitwalia zawadi hizo (hawapo pichani) ni Jesca Haule, Kanuni Midundo, Linah Mrimia, Orest Kawau wa Magic Fm na Othman Michuzi wa Michuzi Blog.
Mchoraji nguli nchini, Komredi Lute Mwakisopile (mwenye kifriji), akidakishwa zawadi yake toka kwa Mratibu wa Wafanye Watabasamu, Nathan Mpangala.
Mratibu wa Wafanye Watabasamu, Nathan Mpangala (anayekaribia paa), akimzawadia mchoro wa kupamba ukutani Meneja mafunzo, motisha na mawasiliano wa Vodacom, Bi. Belinda Wera.
Mjasiriamali Bi. Nana Mzobora wa Dar es Salaam akijitwalia yake.
Meneja masoko wa Nafasi Art Space, Kelvin Kyando akidaka ya kwake. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...