Hellow Mr. Michuzi,
nadhani u mzima. Ingawa siyo mdau wa Blog yako ila ni mfuatiliaji , msomaji na mpenzi mzuri sana wa blog hii. Sielewi sifa za kuwa mdau lakini tuyaache hayo ila nakutumia picha alipozikwa Rais wa Malawi Kamuzu Banda. Sijui ni kiasi gani cha fedha kilitumika kujenga kaburi hilo ila kweli wamalawi wameamua kumuenzi kiongozi wao huyo. Pamoja na yote sehemu hiyo ya kaburi imekuwa ni kivutio kikubwa kwa watalii wengi wafikapo huko malawi. Nami nilibahatika kufika huko kama mtalii wa kibongo. Sijui Baba yetu wa taifa alizikwa vipi ila naomba kama itawezekana tuwekee picha ya sehemu alipozikwa na kama ilishawahi kuwekwa tafadhali nijuze ni tarehe gani uliweka. Maana wengine hatujawahi fika butihama.
Kazi njema.
Kazi njema.

















