

inafurahisha kuona siku hizi vijana wajasiriamali wamechangamka kiasi cha kupeleka bidhaa zao kwenye maonesho ya sabasaba katika kujitangaza. hawa ni wadau wa Bongo Street Wear ambao lebo yao inashika chati kwa chati kutokana na vionjo wanavyoandika juu ya flanazzz
twanga pepeta wakishiriki mashindano ya bendi za muziki wa dansi mwaka 2001 katika ukumbi wa vijana social hall dar. toka wakati huo hakijasikika kitu hadi hii leo na bingwa bado ni walewale sikinde ngoma ya ukae. iko haja ya kufufua mashindano hayo ambayo yalikuwa na changamoto kubwa kwa bendi kujiweka fiti katika kila idarakatika muendelezo wa kuonesha vipaji bwelele bongo, leo tunaye msanii hodari k-sher ambaye ni mmoja wa walio juu katika safu ya wasanii wa kike nchini
zoezi la kusajili namba za simu za mkononi kwa kila aliyonayo limeanza rasmi julai 1, 2009 na mchakato unaendelea vizuri kwani wenye simu wengi wanajitokeza kufanya hivyo ili kuwahi mstari-mfu wa miezi 6 uliowekwa. pamoja na mambo mengine ikiwa ni pamoja na kuonesha huduma wazitoazo kwenye banda lake katika maonesho ya sabasaba, vodacom imeweka makarani wanaoendesha shughuli hizo kama inavyoonekana pichani.
profesa alec chemponda na mai waifu wake wakiwa katika shopping kwenye maonesho ya sabasaba. natumai da'chemi atafurahi kuona taswira hii ambayo inaambatana na salamu za sabasaba toka kwa wazazi wake hawamsanii anayetamba kwa sana hapa bongo kwa sasa, marlaw, anatupeleka kwa 'rita' katika kuthibitisha kwamba yeye ni moto wa kuotea mbali katika bongo fleva. hii ni kabla ya blockbuster yake ya 'pii pii' ambayo leo hii imekuwa kama wimbo wa taifa
kamanda muhidin maalim gurumo akiongoza msondo ngoma band ambayo kwa sasa inatamba na vyombo vipya na vya kisasa ambavyo walaji wa safari lager wamechangia upatikanaji wake. hapa ni katika banda la kizota bar ndani ya viwanja vya mwalimu nyerere barabara ya kilwa rodi ambapo hutumbuiza kila jioni wakati wa maonwsho ya sabasaba 2009
papaa saidi mabera kajificha kwa nyuma wakati romanus mng'ande romario na mwenzie wakipuliza midomo ya bata
MDAU ANAYEKWENDA KWA JINA LA BUNURI SHEFA, AMA FATUMA KAMA ALIVYOELEZA KWENYE INGIZO LAKE, NDIYE MDAU WETU WA MILIONI 6 NA MSHINDI WA KITITA CHA DOLA 1000.

THURSDAY, mchambuzi wa mambo Dr. Licky Abdallah leo amajiunga rasmi na globu ya jamii kama mchangiaji maalumu kwa kuongelea mdau anayeitwa 'anonymous' pamoja na teknolojia mpya ya kibongo ya kupiga mswaki kichwani. mada zote ni mijadala na unakaribishwa kuchangia.
mkurugenzi wa benchmark productions madame rita paulsen aongea na globu ya jamii juu ya bongo star search (BSS)