Mdau mkuu wa Libeneke na nanihii
THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT "THE SMART CHOICE" Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Ila nawaomba tuweze kujieshimu kila mmoja wetu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya globu ya jamii, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoeleza vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.



 

Sunday, July 5, 2009
libeneke la mdau sabato e. tarimo

Baadhi ya watu watakuwa wamemsoma Mhandisi na Mwelimishaji ndugu Sabato E. Tarimo katika gazeti la MsemaKweli kwenye makala zake mbalimbali.


Sasa amejikita katika ulimwengu wa
blogu ili kuwafikia wengi zaidi hasa wale wanaoishi nje ya Tanzania.


Makala alizoandika hadi sasa na zinazotia changamoto ni zile zinazohusu
URITHI na MAVAZI ni kama vile:
URITHI: Mahakama ya kufungulia mirathi
URITHI: Urithi kwa watu wasio na undugu na marehemu...
URITHI: Kumnyima mtu haki ya urithiURITHI: Umuhimu wa wosia
URITHI: Je, urithi ni haki au ni fadhila?
URITHI: Biblia inasema nini kuhusu watoto wa kambo...
URITHI: Sheria za mirathi
URITHI: Kwanini mzaliwa wa kwanza alipendelewa?
URITHI: Ni wakati gani wa kurithisha au kurithi?
URITHI: Nani anastahili kurithi?
URITHI: Kiini cha makalaNi vitu gani sisi wanadamu tunavyoweza kurithishana...
URITHI: HAKI NA WAJIBU WAKO


Jina la Blogu ni:
tanzaniachristianheritage.blogspot.com
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
mandhari ya bandari nyakati za jioni
ufukwe na bandari ya dar vinavyoonekana majira ya jioni.
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
swali la kizushi
Mkuu wa Nanihii na Wadau,
Mie nna kero kubwa dhidi ya hawa ma-DJ wanaotumbuiza kwenye minuso hasa ya harusi. Ukiacha kudai pesa kibao kwa kazi yao hiyo, huwa wanakera sana pale wanaposhobokea kupiga manyimbo yale yale utayosikia kwenye karibu kila harusi, yaani utadhani wameambiana.
Nyimbo nzuri, hasa za nyumbani ambazo zimejaa kibao kutokana na jitihada za vijana wetu wa bongo fleva na hata muziki wa dansa, huwa hawazigusi kabisa utadhani wamegombana nazo. Ukimwamba anakuja juu kama moto wa kifuu, huku akifakamia bia zetu za bure....
Utakuta DJ kakomalia kuwapigia mandombolo ya solo ama manyimbo zilipendwa ya sauzi, na wakati wa kula wanakupigia manyimbo ya ughaibuni ya kina miles david na kenny roggers. hivi kweli bongo tuna ukame kiasi hicho wa nyimbo za nyumbani hadi wakomalie manyimbo wanayopenda kusikia wao na sio waliowalipa kuwaburudisha?
Swali langu la kizushi kwa wadau ni je kifanyike nini ili kubadili fikra za maudhi za ma-DJ wetu wa bongo kwenye minuso???
YAANI MA-DJ WA BONGO MNABOA MPAKA BASI!!
Mdau Festo
Mlimani jirani na UDSM
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 7
JK aenda zambia leo
JK akizungumza na Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere kabla ya kuondoka kwenda Lusaka Zambia kwa ziara siku tatu ya kiserikali asubuhi hii, ambapo leo anatarajiwa kufunguwa maonesho ya kimataifa ya Biashara katika mji wa Ndola Lusaka.
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 8
shein atembelea mabanda ya maonesho ya biashara sabasaba
makamu wa rais akitembelea banda la maonesho la kundi la albino baada ya kufungua rasmi maonesho ya sabasaba mwaka huu. kulia kwake ni waziri wa viwanda na biashara dk. mary nagu
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
vodacom foundation yamwaga madawati 400 kwa shule za msingi dar
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Ukombozi Baraka James(kushoto)akisalimiana na Vodacom Miss Tanzania Nasreem Karim wakati wa makabidhiano ya madawati 55 yaliyotolewa msaada na Vodacom Foundation leo. Kati ni Mkuu wa Vodacom Foundation Mwamvita Makamba, Shule ya Uwanja wa ndege ilifaidika kwa msaada huo pia na kupata madawati 55.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi ya uwanja wa ndege wakiwa wamekalia moja ya madawati 55 na kuonyesha alama ya dole kuashiria kufurahia kwao kwa msaada wa madawati waliyopata leo. shule ya msingi Ukombozi alifaidika kwa msaada wa madawati 55 kutoka Vodacom Foundation ambapo imeanzisha kampeni yake ya kugawa madawati 400 katika shule za msingi za Mkoa wa Dar
Mwalimu wa shule ya Msingi ya Uwanja wa ndege Benard Shao(kushoto)akimuonyesha mazingira Mkuu wa Vodacom Foundation alipofika shuleni hapo kutoa msaada wa madawati 55, ambapo Vodacom imeanzisha kampeni yake ya kugawa madawati 400 katika shule za msingi za Mkoa wa Dares Salaam,(katikati)Vodacom Miss Tanzania Nasreem Karim.
Mkuu wa Mfuko wa kutoa misaada wa Vodacom(Vodacom Foundation)Mwamvita Makamba(katikati) akiongea jambo wakati alipokuwa anatembelea moja ya madarasa ambayo hayana madawati katika shule ya msingi ya uwanja wa ndege leo na kutoa msaada wa madawati 55. Mwenye blauzi ya buluu Mwalimu mkuu wa shule hiyo Edita Semkali.




 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
libeneke la bongo street wear
inafurahisha kuona siku hizi vijana wajasiriamali wamechangamka kiasi cha kupeleka bidhaa zao kwenye maonesho ya sabasaba katika kujitangaza. hawa ni wadau wa Bongo Street Wear ambao lebo yao inashika chati kwa chati kutokana na vionjo wanavyoandika juu ya flanazzz
baadhi ya vionjo katika flanazzz za Bongo Street Wear
baadhi ya wadau wanaotumia bidhaa za Bongo Street Wear
lebo yao
contact zao





 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
nondozzz
Ni katika chuo kikuu cha Voronezh State University huko Urusi ambapo wadau M.Mwinyi (shoto) na ni M.Mohammed (pili kulia) na wenzao wa nchi zingine wakijidai baada ya kuvuta ndondozzz za International law na Political science wikiendi hii.

 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
mashibbota kulikoni?
twanga pepeta wakishiriki mashindano ya bendi za muziki wa dansi mwaka 2001 katika ukumbi wa vijana social hall dar. toka wakati huo hakijasikika kitu hadi hii leo na bingwa bado ni walewale sikinde ngoma ya ukae. iko haja ya kufufua mashindano hayo ambayo yalikuwa na changamoto kubwa kwa bendi kujiweka fiti katika kila idara
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
Diversity Visa Lottery 2009 (DV-2009) Results
Ndugu michuzi,
naomba tu uwajulishe ndugu zangu watanzania kwamba kuni hii DV Lottery unapocheza na kushinda waweza kuja kuishi na kufanya kazi Marekani.
Watanzania wengi tuwe tunaijaribu maana kwa sasa tunapigwa bao kwa sana na watani wa jadi. kucheza kwake ni free na link ni hii hapa http://travel.state.gov/visa/immigrants/types/types_1318.html
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
kutana na k-sher

video

katika muendelezo wa kuonesha vipaji bwelele bongo, leo tunaye msanii hodari k-sher ambaye ni mmoja wa walio juu katika safu ya wasanii wa kike nchini

 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
umeshasajili namba ya simu yako ya mkononi?
zoezi la kusajili namba za simu za mkononi kwa kila aliyonayo limeanza rasmi julai 1, 2009 na mchakato unaendelea vizuri kwani wenye simu wengi wanajitokeza kufanya hivyo ili kuwahi mstari-mfu wa miezi 6 uliowekwa. pamoja na mambo mengine ikiwa ni pamoja na kuonesha huduma wazitoazo kwenye banda lake katika maonesho ya sabasaba, vodacom imeweka makarani wanaoendesha shughuli hizo kama inavyoonekana pichani.

 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 5
maonesho ya sabasaba 2009 yazidi kunoga
profesa alec chemponda na mai waifu wake wakiwa katika shopping kwenye maonesho ya sabasaba. natumai da'chemi atafurahi kuona taswira hii ambayo inaambatana na salamu za sabasaba toka kwa wazazi wake hawa
msanii wabogojo akionesha vitu vyake ikiwa ni mojawapo ya vivutio katika banda la zain kwenye maonesho ya sabasaba barabara ya kilwa rodi dar
wadau kibao wanatembelea maonesho hayo

pamoja na kuangalia bidhaa pia kunakuwaga na shopping la nguvu

wadau wakijipatia bidhaa za dezo kwenye moja ya mabanda

kwa mwaka huu banda la home shopping centre limeleta taswira mpya ya maonesho






 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
mishikaki orijino
nasikia bongo wanatamba sana kwa 'mishikaki' (staili ya upakiaji wa abiria wengi kwenye pikipiki) na kusahau kuwa kuna mishikaki iliyotukuka afrika magharibi
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 12
ZIFF 2009 AWARD WINNERS
12TH ZANZIBAR INTERNATIONAL FILM FESTIVAL

VERONA Award – Seasons of A Life (Malawi)
SIGNIS Jury Award - Commendation
(1)Mah Saah Sah (Cameroon) Dir: Daniel Kamwa
(2)Go With Peace Jamil (Denmark/Afghanistan) Dir:Omar Sharwagi
- East Africa Region Talent – Suwi (Zambia)-Dir: Cathrine Kaseketi Musola
-Signis Award – Izulu Lami (South Africa) – Dir: Madoda Ncayiyana
SEMBENE OUSMANE Award–Keiskamma-A Story of love (South Africa)
Dir:Miki Redelinghuys
ZIFF Chairman Award – Seasons of a Life (Malawi) – Dir: Dir:Charles Shemu Joyah
ZIFF Life Time Achievement Award – Hamid Vuai
UNICEF Award – Mother Unknown (Sudan) –Dir: Taghreed Alsanhouri
ZIFF Jury Award - Special Juror’s choice – African Tales (Tanzania) Producer:Imruh Bakari
- East African Talent – From a Whisper (Kenya) – Dir: Wanui
- Short/Animation – Warahutseho (Cameroon) Dir: Auguste Bernad Koueho
- Documentary - Bilal (India) – Dir: Sourav Sarangi
- Silver Dhow Award – Mon Histoire…Papy (DRC) Dir: Tunda Wa Munga
- Golden Dhow Award – Jerusalema (South Africa) Dir: Ralph Ziman
 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
holiday inn yaibuka upya dar
hoteli ya holiday inn ilipokuwa mawenzi ya zamani barabara ya samora avenue imeshafunguliwa na tayari kwa libeneke la makulaji na malazi.

 
© Michuzi | Sunday, July 05, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
Saturday, July 4, 2009
FC Bongo yaibenjua TAS ya Tampere
Timu ya FC BONGO ya helsinki leo imefuta majonzi ya kufungwa na kilimanjaro ya stockholm baada ya kuibamiza timu ya ndugu zao wa finland TAS ya mji wa tampere kwa goli 3-2.FC BONGO iliweza kuumudu mchezo kwa dakika zote tisini na kabla ya mapumziko walikua wakiongoza kwa magoli 2-0.

TAS ya Tampere iliweza kubebwa na refa ambaye ni shemeji ya mmoja wa wachezaji wao kwa kupewa penati tatu, penati mbili wakapata magoli na penati moja iliokolewa na kipa wa FC BONGO Steve Mashallah ambaye alikuwa ni nyota wa mchezo huo uliochezwa katika kiwanja cha mazoezi cha FC Bongo kijulikanacho kama (Vumbi Stadium).

Pichani Kipa wa Fc Bongo Steve Mashallah mwenye jezi ya orange akiokoa kona. Picha zaidi tunamuomba Edo Ndaki wa Tampere atushushie kwa michuzi.

Habari na Michuzi correspondant
Helsinki.
 
© Michuzi | Saturday, July 04, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 8
msaada tutani
Michuzi na wadau
Naomba msaada wenu. Si unaujua ule wimbo wa
"Michael Jackson njoo...sitaki....kama hutaki nenda...''
naomba kama mnajua nani aliimba na jina la wimbo.
naomba sana msaada wenu mnisaidie hapa tutani.
Natanguliza shukurani mbele
Mdau
 
© Michuzi | Saturday, July 04, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 9
henry na angela wameremeta leo
mdau henry kalunga na mai waifu wake angela hayuma baada ya kumeremeta leo asubuhi katika kanisa la mtakatifu petro jijini dar. wote ni wakazi wa melbourne, australia, na wapo bongo kwa vekesheni ya mai wedingi yao pamoja na fungate.
maharusi na wapambe wao - lusako na sarah
maharusi na wazazi wao
maharusi na wapambe wao wakielekea kwenye mnuso ubungo plaza




 
© Michuzi | Saturday, July 04, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 11
mdau na danny glover zenji
Salaam toka ZIFF. Tunaendelea vizuri na kila siku tuonaonesha documentary za Dakika 7 za Matukio yote ya ZIFF. Na nimepata bahati ya kupiga picha na ZIFF special guest Bwana Danny Glover. Kwa wale ambao ungependa waone daily documentaries waende kwenye link hii http://www.zgfilms.com/events.html
Ahsante!
Ibrahim Matukuta
 
© Michuzi | Saturday, July 04, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
wabongo minnesota wawafunga wakwe 2-1
kikosi cha Uganda(kina shemeji) Minnesota
kikosi cha timu ya Tanzania Minnesota

timu ya tanzania ikipata mawaidha wakati wa mapunziko chini ya kocha wao Peter

Na Mwandishi wako glob ya jamii Minnesota
Ile timu kabambe inayoundwa na vijana watanzania waishio Minnesota, jana ijumaa katika kusherehekea saba saba 2009 inayo sherehekewa kila mwaka 4th of july,ikicheza kwa ustadi na huku ikitandaza kabumbu la kisasa, iliweza kuibanjua timu ngumu ya kutoka Uganda inayoundwa na Waganda wanaoishio Minnesota.
mechi ilikua kali huku Tanzania ikiishambulia uganda takribani muda wote kipindi cha kwanza cha mchezo,na kama si jitihada za golikipa wa Uganda,Vijana hao Watanzania wangekua na karamu kubwa ya mabao.
ilikua kwenye dakika ya 25 ya kipindi cha kwanza Frank Lahinana(Ndombolo) aliipatia Tanzania bao la kuongoza baada ya gonga za hapa na pale na hatimae mpira kumfikia mfungaji aliepiga shuti kali la nyavu ndogo huku akimuacha golikipa wa uganda,Robert akigalagala chini asijue la kufanya na huku beki ya Uganda ikibaki ikilaumiana.
mpaka mapumziko vijana Watanzania walikua mbele kwa bao 1-0 dhidi ya Uganda,refa kutoka Cameroun aliimudu mechi ya jana vyilivyo,kunako dakika ya 37 ya kipindi cha kwanza alimtoa Renes mchezaji kutoka Uganda kwa kadi nyekundu baada ya kupiga ngumi mchezaji David Kinyaiya wa Tanzania beki wa kushoto ambaye alikua anakaba mpaka anawatia fowadi hasira.
kipindi cha pili kilianza taratibu huku Tanzani ikiendelea kutawala mchezo lakini umaliziaji ulikua butu,Kocha Peter wa Tanzania aliifanyia mabadiliko safu ya ushambuliaji ndipo alimtoa Ebra,Kevo na Frank na nafasi zao kuchukuliwa na Robert, Tom na Jerry Katope.
mabadiliko hayo yalionekana kuongeza nguvu na kasi ya ushambuliaji huku mshambuliaji Tuma akiinyanyasa ngome ya Uganda kama anavyotaka,na kunako dakika ya 74 ya mchezo supa sab Robert aliipatia Tanzania bao la 2 kwa kuunganisha krosi ya Tuma kutoka wingi ya kulia,mpira ambao ulianzia kwa beki ya kulia God aliyepanda na mpira na kumtanguliazia tuma aliyekimbia na mpira wingi ya kulia na kufuatwa na mabeki wa Uganda huku wakimsahau mfungaji akiwa peke yake na golikipa wa Uganda.
Tuma aliinua macho na kumwangalia mfungaji na kupiga krosi iliunganishwa na Rob kwa guu lake la kulia na kumuacha kipa akipishana nao.
baada ya bao hilo Kocha wa Uganda Noah alifanya mabadiliko ya kumtoa lyod na kumwingiza Henry mabadiliko hayo yaliongeza ya nguvu kwenye safu ya uganda na ndipo katika dakika ya 97 Kiojozi aliweza kuipatia Uganda bao la kufutia machozi,kwa pasi kutoka kwa Henry.
mpaka dakika 90 Tanzania 2-Uganda 1

 
© Michuzi | Saturday, July 04, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
marlaw akikupa 'rita'

video

msanii anayetamba kwa sana hapa bongo kwa sasa, marlaw, anatupeleka kwa 'rita' katika kuthibitisha kwamba yeye ni moto wa kuotea mbali katika bongo fleva. hii ni kabla ya blockbuster yake ya 'pii pii' ambayo leo hii imekuwa kama wimbo wa taifa

 
© Michuzi | Saturday, July 04, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 8
msondo ngoma band yapeta na vyombo vipya
kamanda muhidin maalim gurumo akiongoza msondo ngoma band ambayo kwa sasa inatamba na vyombo vipya na vya kisasa ambavyo walaji wa safari lager wamechangia upatikanaji wake. hapa ni katika banda la kizota bar ndani ya viwanja vya mwalimu nyerere barabara ya kilwa rodi ambapo hutumbuiza kila jioni wakati wa maonwsho ya sabasaba 2009
papaa saidi mabera kajificha kwa nyuma wakati romanus mng'ande romario na mwenzie wakipuliza midomo ya bata
vyombo vipya na ari mpya ndani ya msondo ngoma band
mkongwe shaaban lendi akiendeleza libeneke la msondo ngoma



vyombo vipya haviongopagi



fundi mitambo wa msondo ngoma kama analia vile kwa jinsi vyombo vipya vinavyomrahihishia kazi



vyombo kama vya michael jackson enzi za uhai wake


sauti ya msondo ngoma sasa inatisha kwa vyombo vipya








 
© Michuzi | Saturday, July 04, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
Friday, July 3, 2009
wadau wa TBL wakivinjari viwanja vya sabasaba
wadau wa kampuni ya bia (TBL) wakivinjari viwanja vya sabasaba leo
wadau wa TBl wakiwa katika banda la Tanzania Distilleries Limited ambalo pia liko chini ya TBL ambapo linazalisha vilaji kadhaa ikiwa ni pamoja na Konyagi, Savannah, Valeur na vilaji vingine kibao


 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
mnuso wa nguvu milton keynes julai 11, 2009

 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
mkutano wa AU wafikia kilele sirte
JK akiwa na Rais wa Zimbabwe Mh. Robert Mugabe pamoja na mwenyeji wao ambaye ni mwenyekiti wa Umoja wa Afrika na Kiongozi wa Libya Kanali Muamar Ghadaffi mjini Sirte wakati wa hafla ya chakula cha usiku kwa viongozi waliohudhuria mkutano wa AU huko Libya usiku wa kuamkia leo ambapo mkutano huo wa siku tatu umefikia kilele

 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 14
msaada tutani
NAOMBA MSAADA WA WADAU KUHUSU RIWAYA YANGU YA KISWAHILI:
"ZIMWI LIKUJUALO"
na
Swallehe Msuya
Pan African Publishing Company
P.O. Box 4212,
Dar es Salaam.
Mnamo mwaka 1986 nilitoa riwaya yangu ya kwanza kwa lugha ya Kiswahili iliyojulikana kama "Zimwi Likujualo..." kupitia Kampuni ya Uchapishaji ya Pan African Publishing iliyomilikiwa na hayati Kanyama Chiume (ex-Malawi).
Baada ya kifo cha Mh. Chiume, sina hakika kampuni hiyo sasa inaendeshwa na nani. Nimekutana na watu toka Kenya wanaonithibitishia kuwa kitabu changu walikisoma katika shule za sekondari huko kwao, na pia kuna jamaa mmoja wa Kijerumani aliniambia kuwa kitabu hicho kimetafsiriwa kwa lugha ya Kijerumani.
Naomba msaada toka kwa yeyote mwenye taarifa juu ya wapi kinapatikana au kinauzwa kitabu hiki anijulishe ili niweze kufuatilia kwani wapo watu wengi wanakihitaji ili nitoe toleo jipya.
Natanguliza shukrani zangu kwani kidole kimoja hakivunji chawa na masuala haya ya "Intellectual Property theft" yameibuka kwa wimbi kubwa siku hizi!
Nawasilisha.
Ndugu yenu
Swallehe Msuya
e-mail address: ssmsuya@yahoo.com
 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 10
mama kikwete mkutanoni sirte leo
Mama Salma Kikwete akiingia katika ukumbi wa mikutano wa Sirte tayari kuhudhuria kikao maalumu cha kamati ya Umoja wa Wake wa Marais wa Afrika dhidi ya Ukimwi OAFLA, mjini Sirte Libya
Mama Salma Kikwete akisalimiana na mke wa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mama
Azeb Mesfin kabla ya kuingia katika ukumbi wa mikutano wa Sirte tayari kuhudhuria kikao maalumu cha kamati ya Umoja wa Wake wa Marais wa Afrika dhidi ya Ukimwi OAFLA, mjini Sirte Libya
Mama Salma Kikwete na Mama Azeb Mesfin katika mkutano huo


 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 5
MABADILIKO YA TAREHE YA MISA YA KUMSALIA MAMA YETU MPENZI MAREHEMU MWALIMU MARGARET KUMBUKA LONDON UNITED KINGDOM
MAREHEMU MWALIMU MARGARET KUMBUKA

KUTOKANA NA SABABU ZISIZOWEZA KUZUILIKA TUNAPENDA KUTANGAZA TAREHE MPYA AMBAYO PADRI AMETUPANGIA KWA AJILI YA MISA YA KISWAHILI YA KUMSALIMIA MAMA MAREHEMU MWALIMU MARGARET KUMBUKA, BADALA YA MISA KUFANYIKA TAREHE 5TH JUMAPILI KAMA ILIVYOTANGAZWA KABLA.

SASA HIVI MISA ITAFANYIKA TAREHE 19TH JULY 2009 JUMAPILI SAA NANE MCHANA (2.00 pm) HADI SAA KUMI JIONI (4.00 pm) KATIKA KANISA LA

ST ANNE'S & ST AGNES CHURCH,

OPPOSITE # 2 GRESHAM ST,

EC2V 7BX

KWA WANAOTUMIA TRAIN ZA UNDERGROUND KITUO CHA KARIBU NI ST PAUL'S (CENTRAL LINE) ,
FOR INFO CONTACT
KHALID 07886897813,
ARAFA 07951503042,
RHODA 07852289892
AND
ACHU 07884420118

KWA NIABA YA KHALID, ARAFA NA MAHADIA KUMBUKA, TUNAPENDA KUTANGULIZA SHUKURANI ZA DHATI KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI WOTE AMBAO TULIOSHIRIKIANA NAO TOKA MWANZO HADI MWISHO WA MSIBA WA MAREHEMU MAMA.

PIA TUNAWATAARIFU KUWA KUTAKUWA NA MISA MAALUM YA KISWAHILI YA KUMUOMBEA MAREHEMU MAMA MARGARET KUMBUKA SIKU YA JUMAPILI TAREHE 5TH JULY 2009 LONDON UNITED KINGDOM KUANZIA SAA NANE MCHANA (2.00 PM) HADI SAA KUMI JIONI (4.00 PM) KATIKA KANISA LA

ST. AGNES/MARGARET CHURCH,
OPPOSITE #2 GRESHAM ST,
EC2V 7QP,LONDON
FOR MORE INFO
CONTACT
07886897813,
07951503042
0R
07852289892
 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
mbilia bel kutumbuiza na king kikii leo police officers mess
mwimbaji wa kutoka congo kinshasa mbilia bel akiwa katika moja ya shoo zake. leo atakuwa police officers mess oysterbay jijini dar akishirikiana na king kikii na kundi lake la wazee sugu. dau mlangoni ni 10,000/- kwa kichwa.

 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 5
Mbilia Bel na King kikii Leo usiku police mess!

Mwanamuziki mkongwe wa rhumba kutoka Kongo,Mbilia Bel leo kwa kushirikiana na mwanamuziki King Kikii usiku wa leo usiku watafanya onesho la pamoja ndani ya ukumbi wa Police Mess,Oysterbay jijini dar,ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni 10,000.kwa kila mtu.

Karibuni wote.
 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
MDAU BUNURI SHEFA NDIYE MSHINDI
MDAU ANAYEKWENDA KWA JINA LA BUNURI SHEFA, AMA FATUMA KAMA ALIVYOELEZA KWENYE INGIZO LAKE, NDIYE MDAU WETU WA MILIONI 6 NA MSHINDI WA KITITA CHA DOLA 1000.
HONGERA SANA MDAU BUNURI SHERFA AMA FATUMA KWA USHINDI HUO. GLOBU YA JAMII INAKUOMBA UWASILIANE NAYO KWA KUPITIA ANUANI ILE ILE YA EMAIL ULIYOTUMIA UKURASA WA GLOBU YA JAMII YENYE TARAKIMU ZA 6,000,000 ILI MIPANGO YA KUKUPATIA CHAKO IKAMILISHWE.
HAPA CHINI NI UKURASA WA EMAIL YA issamichuzi@gmail.com IKIWEKA BAYANA INGIZO LA MSHINDI NA BILA SHAKA NA MAINGIZO MENGINE KAMA INAVYOONEKANA KATIKA UKURASA HUU CHINI AMBAPO INGIZO LA MSHINDI LIMEWEKEWA MRABA WA RANGI YA CHUNGWA.



 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 34
MDAU WA MILIONI 6 APATIKANA
HATIMAYE MDAU WA MILIONI 6 AMEPATIKANA NA HIVI SASA JOPO LA WATAALAMU LINAHAKIKI INGIZO LA MDAU HUYO LILILOTINGA MARA TU BAADA YA HESABU KUTIMIA, NA ATATANGAZWA RASMI SAA SITA KAMILI SAA ZA BONGO LEO.

GLOBU YA JAMII INAPENDA KUTOA SHUKRANI KWA WOTE WALIOJARIBU BAHATI ZAO, NA WENGINE HATA KUTUMA UKURASA UKIWA UNAONESHA KUPITA 6,000,000 NA KUAHIDI KUJARIBU TENA PANAPO MAJAALIWA WAKATI WA KUMSAKA MDAU WA MILIONI 7 ISNHAALLAH KABLA MWAKA HAUJAISHA.


MDAU WA MILIONI 6 AMEPATIKANA SAA 4:42 (10:42am) KWA SAA ZA BONGO. MDAU HUYU AMESHAJULIKANA NA GLOBU YA JAMII INAWASILIANA NAYE KABLA YA KUMTANGAZA KWANI IKIWEZEKANA TUTAHITAJI PICHA YAKE PIA.
 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 7
wadau wa kipindi cha leo tena cha clouds 88.4fm
Dina Marios
Gea Habibu 'VIP'
Zamaradi Mketema
Wakiwa wanafanya vyema katika kipindi cha 'Leo Tena' kinachorushwa na Clouds kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa saba mchana, wadau hawa hakika wako juu na wameshaweza kulazimisha watani wa jadi waige mapigo yao ili kujihakikishia usikilizaji wa kutosha. Habari zao kamili zinapatikana kwenye toleo jipya la jarida la KITANGOMA ambalo lipo mitaani sasa.



 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 14
NANI KUWA MDAU WA MILIONI 6 NA KULAMBA DOLA 1000????

MDAU WA MILIONI SITA ATAPATIKANA WAKATI WOWOTE KUANZIA SASA NA WADAU KAENI MKAO WA KULA MAANA SPIDI YA HESABU ZA WADAU SI YA KAWAIDA KWA MUJIBU WA TARAKIMU ZINAVYOONESHA HAPO CHINI KULIA KUELEKEA KWENYE MILIONI SITA, NA HAMNA KWIKWI WALA NINI....

NAMNA YA KUJISHINDIA DOLA 1,000 ZITAZOTOLEWA NA VODACOM TANZANIA KUPITIA HUDUMA YAKE BOMBA YA 'THE GRID' NI RAHISI SANA.

UNACHOTAKIWA KUFANYA NI KWAMBA ENDAPO UTAFUNGUA GLOBU YA JAMII NA KUKUTA TARAKIMU PALE CHINI ZIKIONESHA 6,000,000 BASI UJUE UMEULA.

UNACHOTAKIWA KUFANYA NI KUKOPI UKURASA HUO WENYE TARAKIMU HIZO ZA 6,000,000 NA KUUTUMA KWA EMAIL KWENDA:



NA MUDA SI MREFU UTATANGAZWA MSHINDI NA UTAAMBIWA UTAPATAJE MKWANJA WAKO.


NAMNA YA KUKOPI UKURASA HUO NI AIDHA PIGA PICHA SEHEMU HUSIKA NA KUITUMA AMA BOFYA KIDUDE CHA 'Prt SC Sys Rq' AMA CHA AINA HIYO KINACHOKUWEZESHA KUKOPI UKURASA (KWA WATUNMIAJI WA MAC) , KISHA NENDA KWENYE 'START' AMBAPO UKISHABOFYA TAFUTA 'PAINT' KUPITIA 'ACCESSORIES' NA UKISHABOFYA NENDA KWENYE 'EDIT' AMBAPO UTABOFYA 'PASTE' NA KUKUTA UKURASA ULIOKOPI UNAJAA HAPO. 'SAVE' NA KISHA TUMA KAMA ATTACHEMENT KWENDA EMAIL HIYO.

MASHARTI NI YALE YALE
1. MSHINDI NI MMOJA TU NA MDAU YEYOTE POPOTE ALIPO GLOBU YA JAMII INAPOPATIKANA RUKSA KUSHIRIKI.
2. UJANJA UNJANJA HAURUHUSIWI NA WALA USIJISUMBUE KWANI JOPO LA WATALAMU LIKO MACHO KUNG'AMUA HILO
3. UAMUZI WA JOPO LA MAJAJI NI WA MWISHO, HAKUNA KUTAKA RUFAA
4. MSHINDI ATAPATIWA MKWANJA WAKE CHAP CHAP NA MARA TU BAADA YA KUTHIBITISHWA KUWA INGIZO LAKE NI LA HALALI.
5. ENDAPO KAMA MSHINDI YUPO DAR ATAELEKEZWA WAPI AJE KUCHUKUA MZIGO WAKE, KAMA YUKO NJE YA DAR ANARUHUSIWA KUTUMA WAKALA KUMCHUKULIA, AMA ATASEMA ATUMIWE VIPI MKWANJA WAKE POPOTE.
-MICHUZI
 
© Michuzi | Friday, July 03, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 15
Thursday, July 2, 2009
Dr. shayo on economic downturn vs public service
Debate on economic Downturn versus public service delivering in a volatile market
The brutal force of the credit crunch and the global economic slowdown, on public, private and companies, government agencies and individuals does not seem to relent.
The intensity or the impact of the downturn has just started to emerge on some economies that seed to be immune when the whole fiasco started. Our monetary experts, economist and even law makers who normally jumps the ship of helping the poor seems clue less and mute on what to do, yet architecting their return following the 2010 elections are at the door.

The Tanzania economy now appears to have accepted that we are not an “island” and downturn will definitely hit our economy more than we are informed. Various sectors of our economy have started to feel the pinch and the ultimate sufferer is not the rich, but the ordinary tax payer.
Soon or later, we are going to witness falling output across most major sectors of the economy and no doubt rising unemployment.
The budget deficit will rise in the first half of 2010/11 and this will have huge impact on inflation, interest rates etc. With the current interest rates at unprecedented levels, one can only wonder what our bankers are thinking; when every nation around the globe is trying to reduce the rates, poor borrowers in Tanzania still, are forced to cough exuberant high rates. And sooner than later, due to the strain, many banks will be forced slash their Interest rates in order stimulate borrowing from the public

A key issue arising for both central and local governmental organisations that I would like readers of Jamii blog to debate and try to suggest solutions to is: what impact the downturn will have on the public sector and the delivery of public services to the poor Tanzanians? Will or should it sweep some of these dozer’s under the bridge?

To make this debate fruitful, contributors will need to scrutinize the critical challenges that will face local governmental organisations in delivering its services: Or explores how lessons from the private sector might be used to deliver change in the public sector.

While the heat of 2010 general elections starts to scorch from a distant, the same old stories of our public leaders elected to find solutions to some of our social problems, so will be the rhetoric from the same people who are contributing nothing to the current crisis, as most of them gear for another round of lucrative and comfy permanent dosing seats in Dodoma.
While we focus on how to incline the economic meltdown consequences, we are also requesting our readers to be realistic and suggest how to deal with these MP’s, who have nothing new to the people, yet planning to blackmail us in 2010 elections.

God Bless Tanzania

Hildebrand shayo
shayohill@yahoo.co.uk
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 22
Sweet Easy this July
Saturday Night Live presents

THT Band feat. Marlaw, Mwaciti & Maunda Zoro
This Saturday, 4 July, from 9pm.
Reservations: 0755 75 40 74.
Sweet Eazy Oysterbay
for the Best Live Music
Every Thursday & Saturday.
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
dili kwa kinadada la chapchap
Mzee wa nanihii habari ya wewe.
Tafadhali naomba nirushie tangazo langu kwa wadau.

Tunahitaji secretary ambaye ana experience isiyopungua miaka miwili na (asiwe maimuna) mwenye kujua kuzungumza na kuongea kingereza kizuri. Umri wowote lakini usizidi miaka 30.
Yeyote mwenye sifa zilizotajwa hapo juu tafadhali atume CV yake kwenye email: tneema58@gmail.com.
CV zote zitajibiwa ikiwa ni pamoja na kupewa taarifa zaidi na maelekezo zaidi.
Mwisho wa kutuma maombi ni Jumatano tarehe 8 / 7/ 2009.
Wenu Mdau.
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 26
CHEKA UNENEPEANE
MY DEAR BOTTLE
A guy, sitting outside his home about to be
evicted from his house, was Contemplating
how the future would be after he had divorced
his wife, abandoned by his Children and lost his job.

He notices a crate of beer bottles and walks up to it. He
takes out an Empty bottle, smashing it into the concrete wall swearing,
"You are the reason I don' t have a wife",
second bottle, "You are the reason I don't have my Children"
third bottle "You are the reason I lost my job".

He notices the fourth bottle is sealed and still full of beer.
He takes the Bottle, puts it aside and says
"Stand aside my dear friend, I know you were Not involved....'
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
jarida la voda world lazinduliwa dar
Mkurugenzi wa teknolojia ya Mawasiliano Tanzania (ICTS) Dr Zaipuna Yonah(kushoto)na Mkuu wa Mahusiano wa Kampuni ya simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania wakionyesha Jarida la Vodaworld mara baada ya kuzinduliwa rasmi usiku wa kuamkia leo
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Dietlof Mare (kushoto)Mkurugenzi Mtendaji wa TCRA Prof John Nkoma(katikati)Mbunge wa Igunga Rostam Azizi wakibadilishana mawazo wakati wa uzinduzi wa Jarida la Vodaworld,Linalomilikiwa na Vodacom Tanzania, Sea Cliff Hotel usiku wa kuamkia leo.

Mkuu wa Mkoa wa Dares Salaam William Lukuvi(kulia) akibadilishana mawazo na Mbunge wa Igunga Rostam Azizi (kushoto)katika hafla ya uzinduzi wa Jarida la Vodaworld (katikati)Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Dietlof Mare.
'TEKNOHAMA KICHOCHEO CHA MAENDELEO NCHINI'

SERIKALI kupitia Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia imesema ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Teknohama) nchini umechochea ukuaji wa kimaendeleo kwa taifa na jamii kwa ujumla ambapo pia umesaidia kukuza uchumi wa nchi.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Teknolojia, Habari na Mawasiliano wa Wizara hiyo, Mhandisi, Dk.Zaipuna Yonah kwenye hafla ya uzinduzi wa jarida la VodaWorld litakalokuwa pia likitangaza historia ya mikoa mbalimbali ya Tanzania.

Akifafanua zaidi Dk. Zaipuna alisema kuwa kwa licha ya Teknohama kuwaunganisha wananchi wa eneo moja na jingine pia imeibadilisha nchi kimaendeleo baada ya baadhi ya kampuni mbalimbali zilizowekeza katika sekta hiyo kujitokeza kuisaidia jamii ya Watanzania katika masuala mbalimbali.

“Kwa sasa Tanzania imebadilika kupitia teknolojia hiyo na kwamba haihitaji kurudi nyuma, kilichobaki ni kwa wadau katika sekta hiyo kuufahamisha umma juu ya maendeleo yaliyopatikana kupitia huduma za Teknohama,” alisema mhandisi huyo.

Akizungumzia jarida hilo la VodaWorld litakalokuwa likichapishwa na kampuni ya simu ya Vodacom Tanzania kupitia kitengo cha 'Vodacom Foundation' kila baada ya miezi mitatu na kutolewa bure alisema likitumiwa vizuri litasaidia kutangaza vivutio vya kitalii, fursa za uwekezaji zilizopo Tanzania nje ya nchi.

“Kwa kuwa jarida hili liko kimataifa na limedhamiria kutoa historia, mila na desturi ya kila mkoa na kwamba kama halitatumika kiubaguzi litaelimisha Watanzania kuhusiana na maendeleo yaliyopatikana kutokana na kuingia kwa teknolojia hiyo nchini,” alisema Dk. Zaipuna.

Awali Mkuu wa kitengo cha mahusiano na Vodacom Foundation Mwamvita Makamba alisema kuwa jarida hilo limeanzishwa ili kueleza mambo mbalimbali yanayofanywa na kampuni hiyo yenye wafanyakazi takribani 700.
Vilevile alieleza kwamba nakala 30,000 zitakazokuwa zikitolewa kila baada ya miezi mitatu kwa asilimia 30 litatoa nafasi kwa wananchi kufahamu kazi mbalimbali wazifanyazo wafanyakazi wa kampuni hiyo, asilimia nyingine zilizobaki zitatumika na kampuni na taasisi zingine za umma kueleza huduma zao ikijumuisha historia ya mkoa mmoja wapo wa Tanzania.

“Soko la Teknohama linabadilika kila siku, wananchi wengi hawafahamu kuhusiana na suala hili, hivyo jarida letu mbali ya kuzungumzia mambo tunayoyatekeleza kila siku pia litaelimisha kuhusiana na historia, siasa, mila na desturi za kila mkoa mmoja kila litakapotoka,” alisema Mwamvita.

 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 10
DOCTORAL AND POST DOCTORAL RESEARCH OPPORTUNITIES AT IHI
Ifakara Health Institute (IHI) is a non-for profit research and training institute whose mission is to develop and sustain a district-based health research and resource centre capable of generating new knowledge and relevant information for public health policy and actions. IHI is among the leading health research institutes in Africa and was awarded the prestigious 2008 Prince of Asturias Award.

Due to expansion in its operations, IHI invites talented young Tanzanians currently in Tanzania or abroad, who intend to pursue a career in health research to join the institute. Candidates will be hired to work within existing IHI research programmes or establish their own Doctoral (PhD) or Post-Doctoral research within the institute. The institute shall facilitate acquisition of funding for Doctoral and Post-doctoral research studies in the following areas:-

Clinical studies
Epidemiology & Public health
Medical statistics
Health System ( including Economics & Informatics)
Immunology
Molecular biology
Nutrition and Non-communicable diseases

A public presentation on IHI’s existing opportunities will be held at IHI Dar-es-salaam Office, Mikocheni, conference room on 21/08/2009 at 2.00 pm. Candidates are invited to attend to obtain more information and discuss their future career plans.
For further information contact Mr Kabegi:

Interested candidates are invited to send their expression of interest, attaching curriculum vitae (CVs) and photocopies of academic and professional certificates to:

The Director
Ifakara Research Institute
Kiko Avenue, Mikocheni
P.O.Box 78373
Dar es Salaam
Fax No. 022 2771714
or send your application through email:

The deadline for receiving expression of interests is 7th August 2009. Only potential and qualified candidates shall be notified and invited for interview during the week of 17th August 2009.

IHI is an equal opportunities employer, women are highly encouraged to apply.
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
zabibu freshi toka idodomya
ushindwe wewe tu. dar kuna zabibu freshi toka makao makuu

 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 11
maonesho ya sabasaba 2009 yameiva
lango kuu la kuingilia kwenye maonesho ya sabasaba
milango ya wadau imebadilika sasa
vifaa vya kisasa katika maonesho
vodacom tanzania wamejipanga kisawasawa mwaka huu
wadau wa lebo ya 'WakaWaka' wapo pia
kama kawaida yao NSSF wapo gado
sura mpya za aina ya mabanda zinaonekana safari hii
kama kawa banda la wizara ya utalii na maliasili wana kila kitu
wachina wamechukua mtaa mzima maoneshoni
watani wa jadi wako kamili kabisa
wachapaji hawa hawako nyuma
wadau kibao wanatiririka sabasaba
manukato toka mashariki ya kati yapo maoneshoni pia













 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 7
Celebrate 'no more limbo' CD by Dennis Massawe

A musical labor of love and faith that’s been a long time coming is completed and you’re invited to the celebration.

A California based artist and Minister, Dennis Massawe, who is a native of Tanzania, has put his inspirational message of faith into songs and you’re invited to celebrate the release of his CD 'No More Limbo'.

His message transcends all faiths and his uplifting rhythms that combine gospel, reggae and soul will move you to get into the spirit of love. His journey has not been easy but he believes all things are possible when you follow the path you were called to walk on.

From childhood to teenage, Dennis grew up in the slums of Nairobi Kenya. He later moved to his native country Tanzania with his father where he started his family at the age of twenty five.

Massawe and his family were lead from Dar-es-salaam Tanzania to Southern California and when you hear his music you too will be inspired, motivated and encouraged to go from your journey of challenges and desperation to one filled with hope and purpose.

For more information go to:
http://www.reverbnation.com/dennismassawe
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
sabasaba 2009 spesho ughaibuni


THURSDAY,
JULY 2ND 20098:00pm - 2:00am
KARIBU Enjoy downtown Minneapolis at the city’s trendiest Rooftop Lounge, where glamour and hospitality abound. Come for dinner, stay for drinks, reconnect with old pals, & make new friends.
Seven,
7th & Hennepin,
Downtown Minneapolis
FREE ADMISSION
-------------------------------------------------------------------------------------------------FRIDAY,
JULY 3RD 20093:30pm - 6:30pm
Umoja Society’s Saba Saba Cup SoccerTanzania vs. Uganda
FREE ADMISSION 8:30pm - 2:00am
Extra Vaa-Khanga FunkHouse Entertainment & MN Fashion Week present a ground breaking Runway show featuring local and international designers, Best Dressed Khanga Competition (must be in by 9:30 pm to qualify to win) and a party hosted by FunkHouse DJ CrewNew Venue for ExtraVaaKhanga
Graves 601 Hotel601 1st Ave N,
Minneapolis
$15.00 for general admission
$25.00 for VIP by the Runway
-------------------------------------------------------------------------------------------------
SATURDAY,
JULY 4TH 2009
MorningShop @ Mall of AmericaTour Nicollet MallCatch Up with friends7:00pm - 1:00am Red Carpet AffairWalk the Red Carpet like the RockStar you are. Dinner served at this luxurious 3 level boat including an open deck. Watch the fireworks from the River in Wisconsin. Enjoy breath-taking views of the St. Croix as we travel from MN into Wisconsin.
St. Croix Boat Co.,
525 South Main Street,
Stillwater MN 55082
Featuring oldskool mix master DJ Luke (DC) & DJ Dennis (MN)
For admission costs and discount packages visit
-------------------------------------------------------------------------------------------------SUNDAY, JULY 5TH 2009
3:00pm - 9:00pm
Umoja Society KWAHERI BBQ Catered BBQ
DJ Dennis will provide the music entertainment
ADMISSION Free with boat ticket
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
freddy macha kuja tena septemba kuendesha semina endelevu
Freddy Macha akijinoma juisi ya dafu alipokuwa hoteli ya mnarani wakati wa vekesheni yake Zenji.

Na Mwandishi Maalum
Mwezi Mei mwaka huu mwandishi na mwanamuziki, Freddy Macha aliendesha warsha mbalimbali zilizochangamkiwa na wakazi mjini Dar es Salaam. Warsha zilifanywa ukumbi wa British Council, Soma Cafe (Mikocheni), Shule ya Sekondari Mwandege na Nyumba ya Sanaa na kugawanywa katika mada kuu nne:
1-Uandishi na Fasihi
2- Muziki
3- Maisha Ughaibuni
4- Mazoezi, afya na chakula bora.

Watayarishaji wa shughuli hii ni gazeti jipya la Lucky-Ideas for Living (lililoanzishwa mwaka huu) ambalo linaipa elimu kipa umbele.

Akizindua warsha hizo zilizokuwa za bure kwa wananchi, Anna Rugaba, mhariri wa Lucky- alisema lengo kuu la semina ni kutoa fursa kwa baadhi ya watalaamu ndani na nje ya nchi kusaidia maendeleo ya kifikra na kimwili kwa Watanzania.

Kutokana na mvuto ulioonekana baada ya shughuli hiyo iliyochukua siku tano; Lucky imeamua kufanya semina mara kwa mara na wataalamu wenye ujuzi tofauti pale itakapowezekana kigharama.

Freddy Macha, anayeishi London na ambaye anajulikana zaidi kama mwanasafu wa magazeti ya Mwananchi, Citizen na Kwanza Jamii anatazamiwa kurudi tena kuendesha semina hizo Septemba mwaka huu.
Website :http://www.freddymacha.com
African TV London: http://www.ailtv.com
Mtembelee Freddy akiendesha semina endelevu Dar http://www.kitoto.wordpress.com
 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
dr. licky abdallah alonga juu ya ma-anonymous na miswaki

video

mchambuzi wa mambo Dr. Licky Abdallah leo amajiunga rasmi na globu ya jamii kama mchangiaji maalumu kwa kuongelea mdau anayeitwa 'anonymous' pamoja na teknolojia mpya ya kibongo ya kupiga mswaki kichwani. mada zote ni mijadala na unakaribishwa kuchangia.

 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 26
madame rita paulsen alonga

video

mkurugenzi wa benchmark productions madame rita paulsen aongea na globu ya jamii juu ya bongo star search (BSS)

 
© Michuzi | Thursday, July 02, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 25
Wednesday, July 1, 2009
JK na mama salma mkutanoni sirte
Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika na Kiongozi wa Libya Kanali Muammar Ghadaffi akiwakaribisha JK na Mama Salma Kikwete kwenye ukumbi wa Ouagadugou jijini Sirte kwenye mkutano wa siku tatu wa Umoja wa Afrika ulioanza leo.
Na Mwandishi Maalum, Sirte, Libya
MKUTANO wa 13 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) umeanza leo, Jumatano, Julai Mosi, 2009, kwenye Kituo cha Mikutano cha Ougadougou mjini Sirte, Libya.

Mkutano huo wa siku tatu unafanyika chini ya uenyekiti wa Kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddaffi, mwenyeji wa mkutano huo na Mwenyekiti wa AU kwa sasa, na mada yake kuu itakuwa ni Umuhimu wa Kuwekeza Katika Kilimo kwa Maendeleo ya Uchumi na Usalama wa Chakula.

Huo ni moja ya mikutano miwili ya wakuu hao wa AU ambayo hufanyika kila mwaka kikatiba, na miongoni mwa viongozi waliozungumza kwenye ufunguzi huo ni pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya AU, Balozi Jean Ping na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Dk. Asha Rose Migiro.

Wengine ni Rais Lula da Silva wa Brazil, Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi za Kiarabu (Arab League), Balozi Amr Moussa, kiongozi wa wafalme wa jadi katika Afrika, Profesa John Nyebela na Mtawala wa Qatar, The Emir of Qatar.

Miongoni mwa viongozi wanaohudhuria Mkutano huo ni Rais Jakaya Mrisho Kikwete, mwenyekiti aliyepita wa AU, ambaye na ujumbe wake aliwasili mjini Sirte usiku wa kuamkia jana, Jumanne, Juni 30, 2009, akitokea Dar Es Salaam.
Ujumbe wa Rais unamshirikisha Mama Salma Kikwete ambaye atahudhuria program maalum ya wake wa viongozi wanaohudhuria Mkutano huo.

Wengine katika ujumbe huo ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wassira.

Akizungumza kwenye sherehe ya ufunguzi wa Mkutano huo, Balozi Ping ametahadharisha juu ya hatari ya kurejea kwa mapinduzi ya kijeshi na mauaji ya viongozi wa nchi za Bara hili.

“Mauaji ya kisiasa na mapinduzi haramu ya viongozi katika Guinea Bissau, Mauritania na Madagascar yanathibitisha kuwa mchakato wa demokrasia ulioanza katika miaka ya 1990 bado haujapata nguvu za kutosha kuzuia mwenendo huo hasi. Jawabu ya hali hiyo ni kuimarisha utawala wa sheria na kuongeza kasi ya ujenzi wa demokrasia.”

Balozi Ping pia ameonya kuhusu athari zinazolikumba Bara la Afrika kutokana na mtikisiko mkubwa wa hali ya uchumi wa dunia na kusisitiza kuwa ulikuwa mtikisiko huo ulioishawishi AU kuchagua mada ya Mkutano huo.

“Tuko katika zahama ya kweli kweli. Afrika inakabiliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi, hali ambayo inaweka shinikizo kubwa katika bajeti za mataifa mbali mbali na kusababisha matatizo makubwa ya upungufu wa chakula,” amesema Ping na kuonya kuwa kama nchi za Afrika hazitakua hatua za haraka kujitosheleza kwa chakula, Afrika haiwezi kuwa na amani na utulivu.

“Chakuka ndilo mahitaji ya msingi kabisa na moyo wa maisha ya binadamu. Bila chakula, Bara letu haliwezi kuwa na amani na utulivu.”

Naye Dk. Migiro pia amezungumzia hali inayoanza kujitokeza tena ya mapinduzi ya kijeshi katika Afrika kwa sura nyingine na pia kutumia muda mwingi kuzungumzia umuhimu wa Afrika kujisheleza kwa chakula.
Rais Lula da Silva amesisitiza uhusiano wa karne nyingi kati ya Afrika na Brazil na jinsi utawala wake ulivyochukua hatua za dhahiri kuimarisha uhusiano huo.

“Kiasi cha wananchi wa Brazil milioni 76 wana asili yao katika Afrika ikiwa ni matokeo ya biashara haramu ya utumwa. Wengine milioni 10 wana asili ya Kiarabu. Binafsi nimetembelea Afrika mara 10 na kutua katika nchi 20,” amesema kiongozi huyo na kuongeza:
“Tunafanya juhudi kubwa kuimarisha uhusiano wetu na Afrika. Tumechangia kilimo cha Afrika kwa kuanzisha mashamba katika nchi nne za Afrika Magharibi zikiwamo Mali, Ghana na Benin…Tunaanzisha kiwanda cha dawa za kutuliza makali ya ukimwi katika Mozambique, na pia kuanzisha Chuo Kikuu chenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 5,000 katika nchi hiyo ya Mozambique. Kwetu sisi Afrika ni bara kaka”

Rais Lula pia amewaomba viongozi wa Afrika kukataa mapinduzi ya kijeshi yaliyotokea katika nchi ya Honduras, na pia amewaomba waunge mkono jitihada za mji wa Rio de Janeiro wa nchi hiyo kuteuliwa kuwa mwenyeji wa Michezo ya Olimpiki ya mwaka 2016.

Naye kiongozi wa wafalme wa jadi, Profesa Nyebela amesema kuwa yeye na ujumbe wake wamealikwa kuhudhuria mkutano huo na Rais Gaddaffi, baada ya viongozi hao kuwa wamemtawaza kiongozi huyo wa Libya kuwa Mfalme wa Wafalme wa Afrika.

“Tunawakilisha, katika mkutano huu, wafalme wote, masultan wote, watoto na koo za kifalme pamoja na machifu wote wa Afrika,” amesema profesa huyo kutoka Ghana katika hotuba iliyovutia zaidi vicheko na kejeli kutoka kwa baadhi ya waliohudhuria sherehe za ufunguzi wa Mkutano huo.
 
© Michuzi | Wednesday, July 01, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 13
TAARIFA YA UCHAGUZI MKUU TBF WATOLEWA
TAARIFA INATOLEWA KUWA MUDA WA KUKAA MADARAKANI UONGOZI WA TANZANIA BASKETBALL FEDERATION (TBF) UNAFIKA KIKOMO MWAKA HUU BAADA YA KUINGIA MADARAKANI SEPT 2005.
KWA MUJIBU WA KANUNI ZA BARAZA LA MICHEZO LA TAIFA (BMT), FEDERATION INATAKIWA KUTOA TANGAZO LA KUITISHWA UCHAGUZI MKUU MIEZI MITATU KABLA, NA TBF INATEGEMEA UCHAGUZI MKUU HUU UFANYIKE DSM OCTOBA 2009 KATIKA TAREHE ITAKAYOTANGAZWA BAADAE UKITANGULIWA NA MKUTANO MKUU WA MWAKA.
BAADHI YA TARATIBU ZA KUZINGATIWA ZA UCHAGUZI HUU NI KAMA IFUATAVYO
1. MIKOA YOTE AMBAYO VIONGOZI WAKE WAKO MADARAKANI KWA KUVUNJA KATIBA (HAWAJAFANYA UCHAGUZI, MAPINDUZI) HAWATARUHUSIWA KUSHIRIKI
2. MIKOA NA UONGOZI WA MKOA YOTE AMBAYO HAIJASAJILIWA KWA MSAJILI HAITARUHUSIWA KUSHIRIKI UCHAGUZI HUU
3. MIKOA YOTE AMBAYO HAIJALIPA ADA YA UANACHAMA TBF PIA HAITARUHUSIWA KUSHIRIKI UCHAGUZI HUO
4. WAJUMBE HALALI WA KUPIGA KURA NI MWENYEKITI, KATIBU NA MWAKILISHI WA WACHEZAJI WA KILA MKOA
5. NAFASI ZITAKAZOGOMBEWA NI RAISI, MAKAMU WA RAIS , KATIBU MKUU, KATIBU MKUU MSAIDIZI, MWEKA HAZINA, KAMISHNA WA WALEMAVU, WATOTO, WANAWAKE, TIBA, UFUNDI, WAAMUZI, MAKOCHA NA WA MAENDELEO
6. MIKOA/WAJUMBE WAJITAYARISHE KUKIDHI GHARAMA ZA KUSHIRIKI MIKUTANO YOTE YA KAWAIDA NA YA UCHAGUZI MIKOA YOTE INAOMBWA KUZINGATIA TANGAZO HILI NA KULIFANYIA KAZI.
LAWRENCE CHEYO
KATIBU MKUU
TBF
 
© Michuzi | Wednesday, July 01, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2


Idadi ya watu
eXTReMe Tracker