THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.

  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com






Rais Kikwete afungua na kuongoza semina ya Wabunge wa CCM Dodoma leo

Mwenyekiti Wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua semina maalum ya wabunge wa CCM ilkiyofanyika katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo.Wengine katika picha kutoka kushoto ni Spika wa bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM Jenista Mhagama, Waziri mkuu Mizengo Pinda,Makamu wa CCM Bara Ndugu Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Baadhi ya wabunge wa CCM waliohudhuria semina maalum iliyofanyika katika ukumbi wa White House mjini Dodoma leo.(picha na Freddy Maro)


DIAMOND, NEY WA MITEGO WAFANYA KUFURU DAR LIVE

Diamond Platnumz akiwapa hi mashabiki.
Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.

DAR Live usiku wa kuamkia leo ilitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho la pamoja kati ya wanamuziki wawili nyota wa kizazi kipya, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Ney wa Mitego ambao walikuwa wakizindua video ya wimbo wao wa 'Muziki Gani'.

Wanamuziki hao kwa pamoja walitoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar.


BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI


MZEE ALLY KLEIST SYKES AFARIKI DUNIA LEO JIJINI NAIROBI


FAMILIA YA SYKES INASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA  MZEE WAO ALLY KLEIST SYKES  (PICHANI) KILICHOTOKEA LEO MEI 19, 2013  KATIKA HOSPITALI YA AGA KHAN JIJINI NAIROBI, KENYA,  ALIKOKUWA AMELAZWA.

MSIBA UKO NYUMBANI KWA MAREHEMU MBEZI BEACH JIJINI DAR ES SALAAM. 

MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA KESHO MEI 20, 2013 KATIKA MAKABURI YA KISUTU BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUSWALIWA KATIKA MSIKITI WA KIPATA WAKATI WA SWALAT ALAASIR.

HABARI ZIWAFIKIE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI POPOTE PALE WALIPO.

إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعونَ
Inna-na lillahi wa inna ilayhi raji'un.
Hakika sisi sote ni waja wa Mwenyezi Mungu, na kwake tutarejea.
Surely we belong to Allah, and to Him shall we return.




majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote yamalizika Visiwani Zanzibar

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (tnbc) Bw. Raymond Mbilinyi, akizungumza na washiriki mbalimbali mjini Unguja Visiwani Zanzibar wakati wa kuhitimisha majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote (smart partnership dialogue) katika ngazi ya kanda ikiwa ni hatua ya kuelekea katika ngazi ya kitaifa, (katikati) ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Dk. Idrisa Hija na mwisho (Kulia) nia Katibu Mtendaji wa Baraza la Biashara la Zanzibar Bw. Ali Vuai.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (tnbc) Bw. Raymond Mbilinyi, (kushoto) akifurahia jambo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Biashara la Zanzibar Bw. Ali Vuai, wakati wa kuhitimisha majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote (smart partnership dialogue) katika ngazi ya kanda ikiwa ni hatua ya kuelekea katika ngazi ya kitaifa. Majadiliano hayo yalifanyika huko Unguja Visiwani Zanzibar.


Miss Tabata kutembelea hifadhi ya wanyama ya Mikumi Mei 26, 2013

Washiriki wa Miss Tabata 2013  (pichani) watatembelea mbuga ya wanyama ya Mikumi wikiendi ijayo. Mratibu wa shindano hilo Godfrey Kalinga anasema lengo la ziara hiyo ni kukuza utalii wa ndani, na kwamba  warembo hao pia watapata fursa ya kujua vivutio vilivyomo kwenye mbuga hiyo iliyoko mkoani Morogoro.
 “Hii siyo mara yetu ya kwanza kuwapeleka warembo wetu mbugani. Tumekuwa tukifanya kila mwaka,” alisema Kalinga. Kapinga alisema kuwa ziara hiyo imedhaminiwa na CXC Africa. 
 Shindano la kumsaka Miss Tabata litafanyika Mei 31 katika ukumbi wa Da’ West Park, Tabata. Wadhamini wa shindano hilo ni Nipashe, Redds, Dodoma Wine, Nipashe, Vayle Springs, Multichoice, Fredito Entertainment, CXC Africa, Brake Point, Michuzi Blog  na Saluti5. 
Warembo watakaoshiriki kwenye shindano hilo  (pichani) linaloandaliwa na Bob Entertainment na Keen Arts ni Madgalena Bhoke (21), Kabula Juma Kibogoti (20), Upendo Dickson Lema (22), Hidaya David Mwenda (22), Aneth Ndumbalo (19), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Musa Kitereja (19), Rehema Kihinja (20), Pasilida Mandali (21), Brath Chambia (23), Joaniter Kabunga (21), Recho Mushi (20),Caroline Sadiki (20) na Suzan Daniel (18). 
 Warembo watano watachaguliwa kushiriki mashindano ya Miss Ilala na baadaye Miss Tanzania. Anayeshikilia taji la Miss Tabata kwa sasa ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.


Jaji Mkuu wa Tanzania ziarani mkoa wa katavi leo

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman, akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Katavi na baadhi ya Watumishi wa Mahakama ya Tanzania mkoani humo walikokuja kumpokea leo asubuhi Katika Ofisi ya Ikulu ndogo ya Mkoa wa Katavi kuanza ziara yake ya kikazi ya kutembelea Mahakama na kujionea hali ya utoaji haki mkoani humo. Picha na Mary Gwera wa Mahakama ya Tanzania


news alert: PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-


Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.

Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.

 Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania 
(TFF)


SUMAYE AENDESHA HARAMBEE CHUO CHA TUMAINI MJINI IRINGA ASUBUHI HII


 Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye akizungumza na  wasomi  wa chuo  cha Tumaini hivi  sasa 
 
 Na Francis Godwin
Waziri Mkuu mstaafu, Mhe Frederick Sumaye amewafunda  wasomi  wa  chuo  kikuu Iringa  zamani Tumaini  kuwa  watumie  kanisa  hilo litakalojengwa kwa ajili ya kueneza amani  zaidi  huku  akiwataka kuachana na malalamiko  yasiyokwisha yanayotokana na  baadhi yao  kutojituma katika  kazi. 
Mhe Sumaye  ametoa kauli  hiyo  leo katika  hotuba  yake kwa wasomi  wa chuo   kikuu cha Iringa cha Tumaini kabla ya kuanza kuendesha harambee kwa ajili ya ujenzi  wa kanisa  la  chuo hicho. 
Amesema  kuwa katika  Bibilia  rushwa na ufisadi ni  dhambi kubwa katika Taifa na  kuwa  vitu  hivyo  tunavilea wenyewe japo kuna tatizo  kubwa  na kuwa kaburi  pekee la mambo machafu ni  ujenzi  wa kanisa  hilo na matumizi yake  kutumika kwa malengo ya  kuhubiri amani na kukemea ufisadi. 
" Mfano  ni nani kati yenu amepata  kutozwa  rushwa na mkulima ila rushwa  inatozwa na  wenye nafasi na hivyo lazima  vijana  wasomi  mkumaliza hapa lazima  kwenda  kubadilisha Taifa....ndio maana  nilipoitwa na baba  askofu kwa ajili ya changizo la kanisa nikasema nitafika kwani ni jambo jema" Mhe. 
Sumaye  alisema na kuongezea  kuwa kumshangilia  mtu anayeendesha gari la kifahari alilolipata  kwa njia ya wizi ni hatari na kuendelea kuliangamiza Kanisa.
 Alisema  kuwa  hivi  leo  watu  wanajenga  chuki kati ya  wanyonge na matajiri na  kuwa   limezuka jambo baya  zaidi kwa  watu kuchukiana kwa misingi ya  dini  zao na kuwa  nchi  yeyote  itakayoingia katika machafuko ya imani ni hatari  zaidi.
 Mhe Sumaye  alisema  kuwa vita  ya kiimani ni mbaya  zaidi na siku  zote  vita  hiyo huwa haina mshindi  hivyo ni vema kila dini kuanza utaratibu  wa kuwafundisha  vijana  wake  ili  kuwa na uzalendo katika Taifa   hili.  
Aidha  alisema  kuwa  malumbano ya  kidini yanayoendelea  mbali ya kutokuwa na mshindi ila  bado  vita  hiyo haitakuwa na mshindi na  hivyo ni  vyema  kila mmoja kuachwa akiendelea  kuamini kile ambacho ana amini  hata kama ni chini ya mti  asisumbuliwe. 
Alisema  vita  ya  udini inayoendelea kwa   sasa  ni mbaya  zaidi  na  kuwa  watanzania  tusiruhusu vita   hiyo kupandikizwa .



 Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akiwa katika harambee ya ujenzi  wa kanisa chuo  cha Tumaini ambako mgeni rasimi  ni waziri mkuu mstaafu  Mhe Frederick Sumaye 


Mbunge Msigwa akisalimia katika  harambee  hiyo

Askofu wa KKKT Dayosisi ya  Iringa Dkt Mdegella ,waziri mkuu mstaafu Mhe  Frederick Sumaye na mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dkt Ishengoma  wakiwa katika harambee  hiyo. Picha na Francis Godwin. 


MTWARA WAPOKEA TUZO ZA SAFARI LAGER


 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Mhe Ponsiano Nyami (wa pili kushoto) akipokea moja ya tuzo za Bia Bora Afrika ilizoshinda bia ya Safari Lager kutoka kwa Mwakilishi wa TBL mikoa ya Lindi na Mtwara, Bariki Massawe(kushoto)  Makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa ziara maalum ya Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kuonesha Tuzo ilizoshinda Bia yake ya Safari Lager ambapo jana walikuwa Mkoani Mtwara. Kulia ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Mhe Ponsiano Nyami (kushoto), Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo (wapili kushoto),Meya wa Maspaa ya Mtwara Mikindani, Shilingi Mtalika (wapili kulia) na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Smythes Pangisa wakiwa wameshikilia tuzo za Ubingwa wa Bia Bora Afrika ambayo ilitwaliwa na Bia ya Safari Lager inayozaliwa na Kampuni ya Bia Tanzania mara baada ya Tuzo hizo kupokelewa na Viongozi hao Mkoani Mtwara jana.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba, Mhe Ponsiano Nyami akionge BD Y kupokea moja ya tuzo za Bia Bora Afrika ilizoshinda bia ya Safari Lager katika shindano la Bia Bora Afrika lililofanyioka nchini Ghana.


KILELE CHA WIKI WA HIFADHI YA JAMII MJINI DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dkt Jakaya Mrsisho Kikwete akifurahia zawadi aliyopewa na makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi SSRA Bi, Jayne Nyimbo  akimtambia “ kuwa ni championi wa Hifadhi ya Jamii’wakati wa kilele cha wiki ya hifadhi ya Jamii hivi karibuni wakitizama ni waziri wa kazi na ajira Mh. Gaudencia Kabaka na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi.

 Mh Waziri wa  Kazi na  Ajira  Mhe. Gaudencia Kabaka akifurahia zawadi aliyopewa na makamu mwenyekiti wa bodi ya SSRA  Bi. Jayne Nyimbo akimtambua jitihada zake katika kuendeleza sekta  ya hifadhi ya Jamii nchini

 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa SSRA waliosimama kuanzia  safu ya nyuma kuanzia kushoto Bw. Mchafu Chakoma na Bw. Jonathan Peles. Mstari wa pili ni  wakuu wa mifuko ya hifadhi ya Jamii Tanzania Bara  wakiwa tuzo  kutoka  SSRA. Walioketi kuanzia kulia ni Mkurugenzi mkuu wa SSRA  BI. Irene Isaka , Makamu mwenyekiti wa Bodi Bi, Jayne Nyimbo, Raisi   wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt Jakaya Kikwete, waziri wa kazi na ajira mh. Gaudencia Kabaka na mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi  
 Picha ya Pamoja ya kamati ya maandalizi na Wanamaonesho wa wiki ya hifadhi ya Jamii chini ya uenyekiti  wa Bi, Sarah Kibonde Msika – Mkuu wa   Mahusiano na Uhamasishaji SSRA
Picha ya  Mgeni rasmi  akiwa pamoja na baadhi ya wajumbe wa  menejimenti ya SSRA  wakati wa kilele cha maonesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii mjini Dodoma.


mama tunu pinda amjulia hali majeruhi wa bodaboda arusha

Mama Tunu Pinda akimpa pole Mzee Athumani Abdala (76) ambaye amevunjika miguu yake miwili kutokana na kugongwa na pikiki Mzee huyo amelazwa katika Hospitali ya Mkoa  Arusha Maunt Meru Mama pnda alifika hospitalini hapo kuwajulia hali wahanga wa Bomu Picha na Chris Mfinanga


mambo ya gado


Good luck to President Jonathan - Against Boco Haram!


sensei Rumadha Fundi ala nondozzz marekani

Mtanzania mtaalamu wa Karate na Yoga Sensei Rumadha Fundi (3rd Dan,Black Belt ) mwenye maskani yake kule marekani juzi Mei 17, 2013 Sensei Rumadha Fundi amekula nondozzz ya "Associate in Applied Science Cardiopulmonary Respiratory Care" katika chuo cha "Collin College, McKinney, Texas, USA. 
Sensei Rumadha sasa amekuwa mtaalam wa hewa na gesi ya kupumua (wa Respiratory Therapist) anayetibu mapafu na moyo chini ya maelekezo ya mganga wa mapafu"pulmonalogist. 
Respiratory therapist ana majukumu mengi kama kuwatibu wagonjwa wa pumu,COPD,Ephysema,Asthma,TB na majonjwa yote yanayohusu mapafu na moyo. Pia ana uwezo wa kutafsiri damu baada ya kupima hali ya mgonjwa kama ana oxygen ya gesi ya kutosha na kama inahitaji tiba yeyote. 
Kwa mengi zaidi kuhusiana na utaalam wa Respiratory Therapist nenda"Who is a Respiratory Therapist? http://en.wikipedia.org/wiki/Respiratory_therapy
 Sensei Rumadha Fundi akielekea kuchukua Nondozzzz zake
 Sensei Rumadha na mkewe Anita pamoja na mdogo wake Rumadha,Kibwana Fundi katika shangwe
 Sensei Rumadha Fundi (mstari wa nyuma) akiwa na wataalamu wenzie wa mapafu
Sensei Rumadha akiwa na ndugu na marafiki.
Sensei Rumadha akiwa na binamu yake Dotto Haruna


ngoma azipendazo ankal

Miriam Makeba aliirusha bendera ya Tanzaniajuu duniani kwa wimbo huu wa 'Malaika'


Michuzi Blog Exclusive!



YANGA WAKIKABIDHIWA KOMBE LA UBINGWA WA SOKA 2013/14



NA MPIRAAAAA UMEKWIIISHAAAAAAAA YANGA WANAONDOKA NA USHINDI WA BAO 2-0 DHIDI YA SIMBA

MABINGWA WAPYA WA KANDANDA NCHINI YANGA WAMEMALIZA LIGI KUU YA VODACOM KWA KUWAPA RAHA MASHABIKI WAKE KWA KUICHAPA SIMBA BAO 2-0 KATIKA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR E SALAAM LEO NA MPIRA NDIO UMEMALIZIKA DAKIKA HII.

PAMOJA NA KUMCHINJA MYAMA KATIKA MECHI HIYO YA KUTIMIZA WAJIBU (YANGA WALISHATANGAZWA MABINGWA SIKU KADHAA ZILIZOPITA), YANGA PIA IMEKABIDHIWA KOMBE LAKE LA UBINGWA MBELE YA UMATI WA WATAZAMAJI 60,000 WALIOFURIKA UWANJANI HAPO. 
HII NI MARA YA 24 KWA YANGA KUIFUNGA SIMBA WAKATI SIMBA IMEWAFUNGA YANG MARA 19. ILA HADI SASA SIMBA INAONGOZA KWA KUIFUNGA YANGA KWA MABAO MENGI, IKIWA NI PAMOJA NA 6-0 NA MABAO 5-0 AMBAYO BADO YANGA HAWAJAJIBU MAPIGO.



SIMBA YAPIGWA BAO LA PILI DAKIKA YA 63

Mshambuliaji Hamis Kiiza anaipatia Yanga bao la 2 dakika ya 63 baada ya piga nikupige katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam 


MKUTANO WA WASTAAFU ZANZIBAR WAFANYIKA LEO

MWENYEKITI wa Jumuia ya Wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaoishi Zanzibar, Mohammed Ali Maalim akimkaribisha mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa jumuia hiyo uliofanyika katika ukumbi wa Eacrotanal mjini Zanzibar.
Kwa habari na picha zaidi BOFYA HAPA


Mwili wa marehemu Dkt Masau kuagwa kesho, kusafirishwa Jumatatu kwa mazishi Ukerewe

Baadhi ya waombolezaji waliokutwa na mtandao huu nyumbani kwa marehemu Dk. Masau, Mbweni Kwa Jumbe, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.  
Imeelezwa kuwa Dk. Ferdinand Masau, aliyefariki jana katika hospitali ya Aga Khan jijini Dar es salaam alikokuwa amelazwa, anatarajiwa kuugwa kesho hapo hapo katika Hospitali ya Aghakan saa 5:00 asubuhi. 

Baada ya hapo mwili utarudishwa nyumbani kwake kabla ya kusafirishwa keshokutwa kwenda kwa maziko kijijini kwao Murutunguru, Wilaya ya Ukerewe. Picha na GPL


NI MAPUMZIKO NA YANGA WANAONGOZA 1-0 DHIDI YA SIMBA

Mpira ni mpumziko katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam huku Yanga wakiendelea kuongoza kwa bao 1-0 lililofungwa dakika ya sita kipindi cha kwanza na mshmbuliaji Didier Kavumbagu. Simba ilipata penati dakika ya 28 na mpigaji Mussa Mudde akakosa kwa kupiga kizemba.

 Mchezo kipindi cha kwanza ulikuwa ni wa vuta nikuvute, lakini Yanga walitawala hasa sehemu ya kiungo.


Maadhimisho ya Miaka 4 ya Ibada ya Kiswahili Columbus - Ohio



SIMBA WAPATA PENATI DAKIKA YA 26, mpigaji afanya uzembe wanakosa bao...

Mrisho Ngassa  wa Simba anafanyiwa faulo na  beki Nadir Haroub Cannavaro  wa Yanga dakika ya 26 na mpigaji wa penati waliyopata Mussa Mure anampasia kipa Ali Mustafa Barthez ambaye anaudaka kiulainiiii...
hivyo bao bado ni Yanga 1 na Simba 0....


Rasimu ya Sera ya Gesi Asilia aionavyo Mhe Zitto Kabwe katika maoni yake ya awali


Mhe Zitto Kabwe anasema amepata muda kidogo wa kuipitia hii rasimu ya 3 nikiwa ya Gesi Asilia akiwa safarini kwenda Tabora kwa shughuli za chama chake cha CHADEMA  na ana maoni yake ya  awali kama ifuatavyo: 


NGOMA YA WATADI WA JADI IMESHAANZA YANGA INAONGOZA BAO 1-0

Mchezo wa watani wa jadi Yanga na Simba umeanza uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dakika nane zilizopita na tayari vijana hao wa Jangwani wameshampiga Simba SC bao 1-0 mapemaaaaa kwa bao la Didier Kavumbagu dakika ya nne kipindi cha kwanza. 
Updates zitaendelea baada ya muda...

Listi ni kama ifuatavyo:
Simba SC : Juma Kaseja, Nassor Masoud 'Chollo', Haruna Shamte, Shomari Kapombe, Mussa Mudde, William Lucian, Mwinyi Kazimoto, Abdallah Seseme, Mrisho Ngassa, Amri Kiemba na Haruna Chanongo. Sub: Abel Dhaira, Miraji Adam, Ramadhan Singano 'Messi', Felix Sunzu, Christopher Edward, Jonas Mkude na Hassan Mkude

Yanga FC : Ally Mustapha 'Barthez', Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub 'Cannavaro', Kelvin Yondan, Athuman Idd 'Chuji', Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na Haruna Niyonzima. Sub: Said Mohamed, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nurdin Bakar, Nizar Khalfan, Said Bahanuz na Jerry Tegete


Rais Kikwete katika Sherehe za Kuapishwa Askofu Mkuu wa Anglikana Tanzania, akutana na Skofu wa Cantebury

 Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini aliyemaliza muda wake Dr.Valentino Mokiwa akimtawaza aksofu Mpya wa Kanisa hilo Askofu Dkt. Jacob Erasto Chimeledya wakati wa ibada iliyofanyika katika kanisa Kuu la Roho Mtakatifu mjini Dodoma leo.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Askofu Mkuu Mpya wa Kanisa la Anglikana nchini Askofu Dkt.Jacob Erasto Chimeledya wakati wa ibada ya kumtawaza kuwa askofu Mkuu iliyofanyika katika kanisa Kuu la roho Mtakatifu,mjijni Dodoma Leo
Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania aliyemaliza muda wake Dkt.Valentino Mokiwa(katikati) akimtambulisha kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete  Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Portal Welby muda mfupi kabla ya kuanza kwa ibada ya kumtawaza askofu Mkuu Mpya wa Kanisa hilo hapa nchini Askofu Jacob Erasto Chimeledya iliyofanyika katika Kanisa kuu la Roho Mtakatifu Dodoma. Picha na Freddy Maro

Kupata hotuba ya Rais Kikwete aliyoitoa


Mfuko wa Pensheni wa PSPF watoa elimu kwa wanafunzi wa chuo kikuu Dodoma

Mmoja wa wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma akichangia mada wakati wa uwasilishwaji wa mada ya manufaa ya mfuko wa Pensheni wa PSPF
 Afisa Mfawidhi wa PSPF akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada katika Semina hiyo kwa wanafunzi wa UDOM
 Afisa wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF mkoa wa Dodoma Rahim Hashim akitoa elimu kwa wanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo kikuu cha Dodoma kuhusu Mfuko na fursa zinazopatikana ukijiunga na Mfuko wa PSPF.
Sehemu ya washiriki wa semina kuhusu Mfuko wa PSPF iliyofanyika katika chuo kiuu cha Dodoma.


ZIFF yatangaza Filamu zilizochaguliwa

 The 16th ZIFF official selection has just been announced. A total of 80 films are featured in 4 categories:   ZIFF Competition, Sembene Prize, Bongo Movies, Out of Competition. (Click on link or image). The festival kicks off on 29th June until 7th July. Here's the complete selection of ZIFF 2013 films including the country and the director for easy reference.

ZAIDI BOFYA HAPA.


UZINDUZI WA TAWI LA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE ZANZIBAR

Na Maelezo Zanzibar-18/05/2013 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ameitaka Bodi na Menejiment ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kuendelea na jitihada za kukiimarisha Chuo hicho ili kutoa Elimu bora yenye viwango vya kitaifa na kimataifa. 
 Rais Shein ameyasema hayo katika hotuba yake ya uzinduzi wa Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalim Nyerere lililipo Bububu nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Amesema njia nzuri ya kupelekea kiwango cha ubora wa elimu chuoni hapo ni kuhakikisha Wanafunzi wanaojiunga wanakuwa na sifa zinazotakiwa pamoja na kupata Walimu wenye ujuzi. 
 Ameongeza kuwa ubora wa Elimu unaotolewa Chuoni hapo utawafanya Wahitimu kukabiliana na ushindani wa Soko la Ajira jambo ambalo litaweka heshima ya Chuo hicho. Aidha Dkt. Shein ameitaka Bodi ya Chuo kuandaa mikakati ya kuliwezesha Tawi la Chuo hicho kuwa Chuo kamili kinachojitegemea badala ya kubakia kuwa Tawi. 
 Amesema Utaratibu wa aina hiyo ndio unaofuatwa Duniani kote ambapo Matawi ya Vyuo vya Elimu ya Juu huwa yanaendelezwa na kuwa Vyuo kamili vinavyojitegemea. Dkt. Shein amewataka Wanafunzi wa Chuo hicho kuitumia fursa waliyoipata ya kuwepo Chuoni hapo kwa kujikita zaidi katika masomo bila ya kujiingiza katika mambo yanayowapelekea katika malumbano. 
 Amewasihi Wanafunzi wa Chuo hicho kuendeleza maadili mema sambamba na kufuata Mila na silka zinazoendana na utamaduni wa kitanzania. 
 Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere Dkt. John Magotti alielezea mafanikio ya Chuo hicho kuwa ni pamoja na kukamilika kwa Jengo hilo ambalo lina uwezo wa kuwahudumuia wanafunzi katika ngazi za Cheti, Stashahada na Shahada. Aidha alielezea changamoto zinazokikabili Chuo hicho kuwa ni pamoja na upungufu wa Mabweni ya kulalia Wanafunzi na Idadi ndogo ya Wanafunzi wanaojiunga na Chuo hicho. 
 Amewataka Wanafunzi wenye sifa kujiunga na Chuo hicho na kuwataka Wazanzibari wenye ujunzi kuomba nafasi za ajira ikiwemo ufundishaji ili kukifanya Chuo hicho kuwa na sura ya kitaifa. 
 Awali akimkaribisha Dkt. Shein Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Dkt. Salim Ahmed Salim amewataka Vijana kuithamini Elimu wanayoipata Chuoni hapo ili iweze kuwa Mkombozi wa maisha yao.
 Jengo la Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere lililopo Bububu limegharimu Jumla ya Shilingi Bilioni 3.6 ambazo zimegharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo kwa sasa Tawi hilo ni kwa ajili ya Wanafunzi wa ngazi ya Cheti.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya uzinduzi wa Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo. Kushoto ni  Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Dk.Salim Ahmed Salim
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Chuo Dk. John Magoti, baada ya kuzindua rasmi  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Mshauri wa Kitaalamu wa Chuo cha Ardhi serikali ya Muungano Dk.Staulans Ntiyakunze,(wa tatu kulia) baada ya kuzindua rasmi  Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo. Kushoto ni  Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Dk.Salim Ahmed Salim
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiangalia meza na vikalio vyake wakati alipotembelea moja ya madarasa katika  Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,huko Bububu Zanzibar leo, baada ya kuzindua Chuo hicho,(kushoto) Mkuu wa Chuo Dk. John Magoti, na pili kulia makamo wa kwanza wa Rauis wa Maalim Seif Sharif,akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi
ya Chuo Dk.Salim Ahmed Salim.[
Mwalimu wa Darasa la Kompyuta Julius Maungo,akitoa maelezo kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipotembelea katika darasa la kompyuta chuoni hapo
 Baadhi ya wanafunzi wa Chu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Tawi la Zanzibar wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa chuo hicho leo 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akipokea zawadi kutooka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Mwalimu Nyerere  Dk.Salim Ahmed Salim,wakati wa uzinduzi wa Tawi la Chuo hicho uliofanyika leo huko Bububu Nje ya Mji wa Zanzibar. Picha zote na Ramadhan Othman,Ikulu