Mdau mkuu wa Libeneke na nanihii
THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT "THE SMART CHOICE" Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Ila nawaomba tuweze kujieshimu kila mmoja wetu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya globu ya jamii, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoeleza vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.





 

Saturday, November 21, 2009
JK mwenyekiti mpya EAC
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki aliyemaliza muda wake Rais Paul Kagame wa Rwanda akimkabidhi mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo Rais Jakaya Mrisho kikwete zana za kazi wakati wa mkutano wa wakuu wa jumuiya hiyo uliofanyika AICC mjini Arusha leo.
Mwenyekiti mpya wa jumuiya ya Afrika Mashariki Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi kombe la ushindi Kapteni wa timu ya Bunge la Tanzania Mh. Iddi Azan baada ya timu hiyo kuibika mshindi wa kwanza katika mashindano ya mpira wa miguu wa mabunge ya Afrika mashariki . Picha na mdau Freddy MARO wa Ikulu.


 
© Michuzi | Saturday, November 21, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
Friday, November 20, 2009
LIBENEKE LA SCHOLARSHIP FORUM
Anko akiwa na Makulilo Jr. alipokuja vekesheni bongo hivi karibuni. Mnyonge mnyongeni ila mdau anastahili sifa kwa kuwa si mchoyo wa kuanika hadharani dili kibao za nondozzzz.


Kaka Michuzi, Mh Balozi na Mdau wa Libeneke la Nanihii
Napenda kuwatangazia ndugu wadau wote kuhusu maboresho niliyoweka katika mtandao kuhusiana na mambo ya scholarships.
Nimeanzisha SCHOLARSHIP FORUM ambayo ni www.scholarshipnetwork.ning.com
Hii ukijiunga itakusaidia kupata updates za kila scholarship info ninayoiweka katika link hiyo. Kila tangazo la scholarship niki-post hapo utapata e-mail kukujulisha.

Pia libeneke la
nalo litaendelea kuwa hewani kama kawaida.
NOTE: Mh Balozi, natoa shukrani zangu kwako kwa wewe kuwa mmoja kati ya wadau ambao wameshajiunga katika Forum hii.

Mdau
MAKULILO, Jr.
San Diego, CA
 
© Michuzi | Friday, November 20, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 5
MISA YA KUMBUKUMBU YA KUMUOMBEA MAREHEMU JOHN KIYUNGU MAGENI JUMAMOSI TAREHE 21/11/2009 DAR ES SALAAM

Tarehe 21/11/2009 mpendwa wetu marehe John Kiyungu Mageni (pichani) atakuwa anatimiza mwaka mmoja (1) tokea afariki dunia.
Kutakuwa na Misa ya kumuombea marehemu John Kiyungu Mageni katika Kanisa Katoliki Chang'ombe Polisi saa 12 kamili asubuhi. Pia kutakuwa na Misa ya kumuombea marehemu nyumbani kwao Mwanza, Ngudu Kwimba.

Sisi tulikupenda lakini mwenyezi mungu amekupenda zaidi. Tunakuombea upate amani mpaka hapo mwenyezi mungu atakapotukutanisha nawe, Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amen.

Kwa maelezo zaidi.
Wasiliana na Joseph Mageni ( 0713-380-750)
 
© Michuzi | Friday, November 20, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 5
maporomoko ya marangu
mdau akiwa marangu falls huko moshi. pamoja nayo pana kahistoria kwa kuvutia sana ambapo binti alipojigundua ana mimba akataka kujirusha afe, lakini roho ilipokataa kufanya hivyo alipogeuka akakutana na chui. ikabidi ajirushe. sanamu za hadithi hiyo zipo juu kule

 
© Michuzi | Friday, November 20, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 8
mpoki apata ajali
Mpoki, mwigizaji maarufu wa kundi la Ze Original Komedy (kulia) amepata ajali ya gari usiku wa kuamkia jana, na inasemekana amevunjika mkono wake wa kushoto ambapo mfupa umeachia.
Habari kutoka ndani ya kundi hilo zinasema hali yake sio mbaya sana na jana aliruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospitali ya Kairuki iliyoko mikocheni jijini Dar, na ataendelea na matibabu akiwa nyumbani.
Ajali hiyo ilitokea mikocheni wakati gari alilokuwa anaendesha lilipogongana uso kwa uso na Rav4 iliyokuwa inaendeshwa na mwanamama ambaye naye kalazwa hospitali ya TMJ.
 
© Michuzi | Friday, November 20, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
dogo wa uswazi leo

----------------------------------------
LIBENEKE JIPYA LA KATUNI
Kaka Michuzi mi ni mdau sana wa libeneke nataka nishee na wadau web moja ya mkatunist ambaye amewaunganisha wenzao na kupost kazi zao; zipo kazi za kina Said Michael, Chris Katembo na Simon Regis, pamoja na Patrick Dumulinyi, web yenyewe inaitwa
http://www.galachakatuni.com/katuni/
 
© Michuzi | Friday, November 20, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
libeneke la dot TZ
Kumbuka , “Jina la kikoa cha .tz = .tz domain name” na domain ni kama vile “kalumekenge.co.tz” ama "libeneke.co.tz" na faida yake ni kwamba hii inatambulisha chap chap kwamba libeneke lipo bongo. maelezo mengine ni kama inavyoonekana kwenye bango



 
© Michuzi | Friday, November 20, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
Thursday, November 19, 2009
FIFA World Cup trophy jets into Tanzania
The First Family pose with the trophy
President Jakaya Kikwete holds the FIFA World Cup Trophy at the NAtional Stadium in Dar es salaam today. Right is FIFA representative Hadi Amal and left is Coca Cola Tanzania Marketing Manager Herrieth Mutayobwa. Hundreds of soccer fans turned up at the stadium to witness the coveted troph and some had the chance to have their photos taken while standing near it.

First Lady Salma Kikwete is happy to hold the trophy

Your Excellency... Sorry. Its you, only you, who is allowed to touch the trophy...

President Jakaya Kikwete holds aloft the trophy

dancers entertain

a police chopper was but one of the many security measures taken to guard the trophy

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE KWENYE UZINDUZI WA ZIARA YA KOMBE LA FIFA LA DUNIA UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM 19 NOVEMBA, 2009

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Joel Bendera (Mb;
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe. Chiku Garawa;
Waheshimiwa Wabunge;
Wawakilishi wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA;
Viongozi wa Kampuni ya Coca-Cola;
Viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF;
Wageni Waalikwa;Mabibi na Mabwana

Najisikia mwenye furaha kubwa kupata fursa hii ya kujumuika nanyi katika tukio hili la kihistoria kuhusu ziara ya Kombe la FIFA la Dunia hapa Tanzania.Nchi yetu imebahatika, kwa mara nyingine tena, kupata ugeni huu mkubwa wa Kombe la FIFA la Dunia ambayo ndiyo tuzo ya juu inayotolewa kwa nchi bora kuliko zote katika soka duniani. Hii ni mara ya pili sasa kwa FIFA kutupa heshima hii. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2006.

Napenda kuwashukuru FIFA na Coca- Cola kwa upendeleo huo kwa nchi yetu.Kabla ya FIFA na Coca-Cola kuanzisha ziara ya Kombe la FIFA la Dunia, wapenda soka wengi duniani walikuwa wanaliona kombe hili kupitia kwenye picha za magazeti na luninga.

Leo hii kupata bahati ya kuliona kombe lenyewe “live” ni jambo la kihistoria litakalodumu katika kumbukumbu yetu kwa miaka mingi. Naipongeza FIFA kwa kuanzisha utaratibu huu wa kuwezesha maelfu ya wapenda soka duniani kuliona kombe hilo kwa karibu na wengine hata kupata nafasi ya kulishika na kupiga nalo picha.

Hii ni fursa ya pekee na ya kujivunia. Kwa Watanzania wenzangu tuichukulie ziara ya Kombe la Dunia nchini mwetu kama ni changamoto kubwa kwetu inayotutaka tufanye vizuri zaidi katika soka ili tulingane nayo heshima hii tuliyopewa.

Hasa ni changamoto kwa viongozi wa soka wa ngazi zote pamoja na wachezaji na wapenzi wa mpira wa miguu nchini. Kuja kwa kombe hili ni deni kwetu na kulilipa kwetu sisi ni kuzinduka, tuendeleze kiwango chetu cha soka nchini ili na sie siku moja tushiriki fainali za kombe hili.

Hili ni jambo linalowezekana. Wapo wenzetu Afrika wameweza, kwa nini sisi tusiweze. Wao ni watu kama sisi, maadamu wameweza na sisi tutaweza. Lakini, ili tuweze hatuna budi kuiga mfano wao hususan waliyofanya na wanayoendelea kufanya kuendeleza mpira wa miguu. Twende tukajifunze kutoka kwao.

Lakini hata kabla ya kwenda huko, yapo mambo ambayo hatuna budi kuyafanya. Naomba nitaje baadhi yake:-

1. Tuimarishe uongozi, utendaji na uendeshaji wa vilabu vya mpira. Mchezaji hufundishwa kucheza mpira katika klabu yake. Hapo ndipo hufundishwa maarifa ya kucheza mpira na vipaji kuendelezwa. Hebu tujiulize hali ya vilabu vyetu vya soka nchini ikoje.

Je vinaongozwa vizuri? Vinaendeshwa vizuri? Jibu tunalijua sote kwamba ni hapana. Lazima suala hili tulitafakari kwa yakini na kulipatia jawabu. Tukishindwa kupata jawabu muafaka na mambo yakaachwa kuendelea yalivyo, mpaka mwisho wa dunia hatutakuwa tumesogea popote.

2. Tupate walimu wenye ujuzi na uzoefu kufundisha timu zetu. Hii ndiyo njia ya uhakika ya kukuza na kuendeleza vipaji na hivyo kupata wachezaji walio bora.

3. Tuwekeze katika kuibua na kuendeleza vipaji vya wachezaji toka umri mdogo. Vilabu viwe na timu za watoto na vijana. TFF isaidie kuanzishwa kwa shule za mchezo wa mpira wa miguu kwa watoto na vijana. Mashuleni wapatikane walimu wa michezo walio wazuri kufundisha.

4. TFF ionekane zaidi ya ilivyo sasa katika mipango ya kuendeleza soka mashuleni, vijijini, mitaani na hata vilabuni. TFF ikiwa na mipango na ikasimamia na kuwabana wadau kuitekeleza itasaidia. Vinginevyo TFF itabakia kusimama ligi kuu, kutoa adhabu kwa wachezaji, na timu ya taifa.

Hiyo haitoshi.Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi kwa kampuni ya Coca-Cola kwa mchango wake muhimu inaotoa kuendelea mchezo wa soka nchini na hasa soka la vijana. Mashindano ya Kombe la Copa Coca-Cola kwa vijana wa chini ya miaka 17 ni ushahidi tosha wa mchango huo adhimu.

Mashindano hayo yamegusa vijana wengi kote nchini. Naambiwa zaidi ya timu 1500 zilijitokeza kwa mwaka huu na maelfu ya vijana walijitokeza kuonyesha vipaji vyao. Naomba utaratibu huu uendelee kwani utakuwa na manufaa makubwa siku za usoni.

Maombi yangu kwa TFF ni kujipanga vizuri kutambua vijana wenye vipaji vizuri na kupanga mipango ya kuiendeleza.Ujio kwa Kombe la FIFA la Dunia hapa nchini mbali na kuhamasisha vijana wetu pia ni fursa nzuri ya kutangaza nchi yetu pamoja na fursa zake za utalii na uwekezaji.

Watu wengi zaidi wataifahamu nchi yetu vizuri zaidi kupitia ziara hii ya Kombe la Dunia. Hivi sasa tuna uwanja mpya wa kisasa ambao utaonekena vizuri wakati wa ziara hii na pengine kuvutia timu kubwa duniani kuja kufanya mazoezi hapa wakati wa fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Afrika Kusini 2010.

Changamkieni fursa hii kwa maslahi ya taifa letu ili tunufaike na sisi. Baada ya kusema maneno haya machache, sasa niko tayari kufanya kazi iliyotuleta hapa sote. Nawashukuruni kwa kunisikiliza.








 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 33
malkia mmoja, marais 11 wa marekani
Malkia Elizabeth II wa uingereza anashikilia rekodi ya kuwa mmoja wa viongozi aliyedumu madarakani kuliko yeyote duniani. Katika taswira hizi anaonekana akiwa na marais 11 wa marekani ambao wengi wamedumu madarakani kwa vipindi viwili vya kati ya miaka 5 hadi 7, ukiondoa Obama. Juu akiwa na Rais Richard Nixon (pili kulia). Kumbuka Marekani hadi sasa imetawaliwa na jumla ya marais 44. BOFYA HAPA
Malkia Elizabeth II akiwa na Rais Barak Obama wa Marekani
Malkia Elizabeth II akiwa na George Bush Jnr.
Malkia Elizabeth akiwa na Bill Clinton
Malkia Elizabeth II akiwa na George Bush Snr.
Malkia Elizabeth II akiwa na Ronald Reagan
Elizabeth II akiwa na Jimmy Carter
Malkia Elizabeth II akiwa na Gerald Ford
Malkia Elizabeth II na mumewe Prince Philip wakiwa
na John F. Kennedy na Jaquiline Onasis Kennedy
Malkia Elizabeth II akiwa na Dwight D. Eisenhower
Malkia Elizabeth II akiwa na Harry S. Truman











 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 22
january makamba alonga
SWALI: Wewe ni mtoto wa mwanasiasa marufu ambaye ni Katibu Mkuu wa Chama Tawala CCM, Mh. Yusuph Makamba, je unafikiria kuna mategemeo makubwa yanayokuja kama dhamana ukizaliwa kwenye familia maarufu ya kisiasa kama ya Makamba?

JIBU: Kwanza kuna heshima kubwa kutambua kwamba mzazi wako ameyatoa maisha yake kwa utumishi wa umma. Kuna sacrifices ambazo kama familia lazima mzikubali kutokana na shughuli za Mzee.

Pili, kuwa na jina la Makamba kuna uzuri na ubaya wake. Uzuri wake ni kwamba wapo watu wengi katika sehemu mbalimbali za nchi hii ambao wamefanya kazi na baba na wanamheshimu sana. Kwahiyo tayari unayo network kubwa ya extended family ambao wengi wanakujua tangu uko mdogo na wanafurahishwa na wanajiona ni sehemu ya mafanikio yako, na wako tayari kukusaidia kwa ushauri au mambo mengineyo wakati wowote.

Lakini pia wapo ambao wanaona Mzee Makamba ni mtu fulani hivi hafai au mtu wa hovyo au wana kutokuelewana naye kimitizamo au kisiasa. Mara nyingi, katika mazingira ya kwetu hapa, hawa watu hawawezi kutofautisha kati ya mawazo na misimamo ya baba na mtoto. Kwahiyo, unajikuta unarithi marafiki na maadui wa baba yako hata bila ya wewe mwenyewe kutaka.

Vilevile, ukiwa mtoto wa mwanasiasa mara nyingi kuna dhana katika jamii yetu kwamba umeishi a privileged life na kwamba umeharibika au umedekezwa na kwamba huwezi kujisimamia mwenyewe. Hii si kweli. Maisha yetu sisi miaka yote yamekuwa ya kawaida sana. Nakumbuka Mzee wangu kwa mara ya kwanza amemiliki nyumba yake si muda mrefu uliopita, na ilikuwa ni nyumba ya makuti pale kijijini Kiomoni, Tanga.
Wakati wa mvua, nyumba hii ilikuwa inavuja. Tunahamisha vitanda na furniture. Na wakati tunakaa Kiomoni tulikuwa tunasoma Masiwani, Tanga Mjini ambapo ni Kilomita 12, na tulikuwa tunaenda kwa mguu, ukibahatisha ni baiskeli, na lunch ilikuwa ni mihogo ya kuchoma na maji, mama alikuwa anatupa shilingi hamsini kila asubuhi. Lakini leo kila mtu anadhani maisha yako yote umekula mkate na siagi na umepelekwa shule kwa gari.

Hata hivyo, siamini kama kuishi maisha ya shida au ya starehe kunaweza kuwa kigezo cha wema au ubaya wa mtu na uwezo au udhaifu wa mtu.
Ukitaka haya na mengi
mengineyo kumhusu January:
 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 36
TUTUNZE MAZINGIRA SIYE TUISHIO PEMBEZONI MWA BAHARI
Kaka michuzi naomba unisaidie katika kuelimisha wananchi waishio pembezoni mwa bahari waelewe umuhimu wa kutumia vyoo. Watu wengi waishio pembezoni mwa bahari kuchimba vyoo inakuwaga ngumu sana wengi hatumia fukwe ili kukidhi haja zao kubwa na ndogo. Siyo Pembezoni mwa bahari tu hata wale waishio pembezoni mwa maziwa na mito.
Regards,
Mdau wa Mazingira
 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 19
vodacom tanzania yamwaga 25m/- zenji kwa mapinduzi cup
Mkurugenzi masoko wa Vodacom Tanzania, Ephraim Mafuru (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi ya sh.milioni 25 kwa naibu waziri kiongozi na waziri wa habari utamaduni na michezo wa Zanzibar Mh. Ali Juma Shamhuna kwa ajili ya udhamini wao wa kombe la Mapinduzi kwenye sherehe iliyofanyika kwenye hoteli ya zanzibar ocean view leo.

Naibu waziri kiongozi na waziri wa habari utamaduni na michezo zanzibar, Mh. Ali Juma Shamhuna akiongea kwenye hafla ya kupokea hundi ya sh.milioni 25 udhamini wa Vodacom Tanzania kwa kombe la mapinduzi 2010. hafla ilifanyika le kwenye hoteli ya zanzibar ocean view.


Mkurugenzi Masoko wa Vodacom Tanzania Ephraim Mafuru akiongea katika hafla hiyo ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni 25 kwa ajili ya kombe la Mapinduzi.

Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania leo imetangaza udhamini wake wa kombe la Mapinduzi 2010. Ambapo mashindano haya yataanza Mwezi mosi 6 .2010.Mashindano haya hufanyika kila mwaka kuazimisha siku ya mapinduzi Zanzibari ya 1964.

Akitangaza udhamini huo Mkurugenzi wa masoko wa Vodacom Tanzania Eprhaim Mafuru, alisema kampuni yake itatumia kiasi cha shilingi milioni 68/=katika kudhamini mashindano hayo ya kombe la Mapinduzi, “tumedhamini kombe la Mapinduzi mapema mwaka huu na mwakani tutakuwa wadhamini wakuu wa kombe la Muungano kwasababu Vodacom Tanzania imejidhatiti katika sekta ya kuendeleza michezo hapa nchini”alisema.
Vodacom Tanzania itaendelea kudhamini michezo mbalimbali hapa nchini na kutoa nafasi kwa vijana ili waweze kuendeleza vipaji vyao na kujijengea dhana ya kujiajiri wenywe na kuweza kuchezea timu za nje miaka ijayo.

Kombe la Mapinduzi litashirikisha timu nane za Tanzania bara na visiwani,kati ya timu ambazo zitashiriki katika kombe hilo ni Simba,Yanga na Mtibwa kutoka Tanzania bara na Tanzania visiwani ni Malindi, Miembeni, Mafunzo na Ocean View FC.

Mafuru alisema fainali za mashindano hayo yatafanyika katika kiwanja cha Gombani kilichopo Pemba ambapo itakuwa ni siku ya kuazimisha siku ya mapinduzi ya Zanzibar,alisema hayo wakati akikabidhi hundi ya shilingi Milioni 25 kwa Waziri wa habari utamaduni na michezo wa Zanzibar Mheshimiwa Juma Shamhuna.

Nae mgeni rasmi Waziri wa habari utamaduni na michezo aliipongeza Vodacom kwa kuendeleza utamaduni wake wa kudhamini michezo na kutaka wawe na moyo huohuo ili waweze kuinua vipaji mbalimbali vya vijana wa kitanzania waje kupeperusha bendera ya Taifa siku zijazo,pia alitoa wito kwa mashirika binafsi kuiga mfano wa Vodacom na kudhamini michezo mingine kwani siyo soka tu bali kuna michezo mingi hapa nchini ikiwepo michezo ya mikono ya wanawake(netball)






 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
Kiswahili Wikipedia Competition
What is the Kiswahili Wikipedia Challenge?

This is your opportunity to bring Africa's information online by creating Wikipedia articles in Kiswahili. You can participate by translating English Wikipedia articles into Kiswahili or by writing your own articles from scratch. You can choose your own topic to write about.

Are you a pursuing a degree in Physics?
Translate the entry for 'condensed matter' from English to Kiswahili.

Studying literature?
Write an entry on your favorite local author. Or translate an article about your favorite musician or sports team. Just think about what topics would be of interest to some of the 100 million Kiswahili speakers worldwide.

Read more about it at:
/kiswahili-wikipedia-competition.html

Subi: wavuti.com
 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
TANZANIA RED RIBBON CHILDREN'S DAY
MDAU UNAKARIBISHWA KWENYE HAFLA HII YA RED RIBBON JUMAPILI HII UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE HALL JIJINI DAR, AMBAPO MALI NA WASANII NYOTA KUTUMBUIZA, WABUNIFU WA MITINDO WOTE WATAPANDA JUKWAANI KUCHEZA MITINDO MBALIMBALI YA DANSI.

 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
hasheem thabeet yuko gado
hasheem thabeet ambaye juma moja lililopita aliripotiwa kuumia taya wakati wa gemu anasema kwamba yuko gado na anaendeleza libeneke kama kawa na memphis grizzlies. bongocerebrity wameongea naye na kwa kuona kaongea nini
 
© Michuzi | Thursday, November 19, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
Wednesday, November 18, 2009
MKUTANO WA KUMSHUKURU MUNGU NA KULIOMBEA TAIFA-TANZANIA
Rev: Mathayo J. Malekela anawatangazia Watanzania wote waishio Washington DC, Maryland na Viginia ( Metropolitan Area ) kuwa kutakuwa na mkutano tarehe 22.11.2009 wa kumshukuru Mungu na kuliombea Taifa letu Tanzania, Marekani na kuziombea familia mbali mbali za Watanzania waishio Ughaibuni.

Mambo ya kuombea ni pamoja na :-
1. Hali ya uchumi nchini Tanzania na Marekani
2. Majanga ya njaa, magonjwa na Ukame nchini Tanzania
3. Kuziombea Serikali za Tanzania na Marekani pamoja na viongozi wote
4. Kuombea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa mwaka 2010.
5. Tutaendelea kuzikemea roho chafu za mauaji ya vikongwe na albino pamoja
na roho zinazoshawishi kutoa ama kupokea rushwa nchini Tanzania.

Na mengine mengi yahusuyo familia zetu za hapa Marekani.
Mahali pa kufanyia mkutano ni ndani ya chuo kikuu cha Maryland katika
anwani hii-
3621 Campus Dr
College Park MD 20740-
Muda ni kuanzia saa 7:00 mchana.

Tangazo hili limeletwa kwenu na Wachungaji
Malekela MJ, Ferdnand Shideko na
Jonh Kadyollo
kwa nia ya uongozi wa kanisa la
The Way of the Cross Gospel Church
Maryland na Washington DC.

Kwa mawasiliano zaidi piga simu
202 609 3313,
202 438 6753
na
202 367 3275

WOTE MNAKARIBISHWA SAAAAAAAAAAAAANA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
ZABURI 133:1-3, II NYAKATI 7:14 na YEREMIA 1:12
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
Baby Powder Premiere Yafana Atlanta.
Uzinduzi wa sinema ya Baby Powder uliofanyika huko Atlanta, Ga. ulikamilika kwa mafanikio makubwa. Onyesho hilo lililofanyika katika thieter ya Porter Sanford III ulitanguliwa na Red Carpet ambayo kamera ya mdau iliwadaka waigizaji na wageni mbali mbali wakila manepu.
Baada ya hapo sinema ilianza hapo saa moja kamili. Watu walikuwa ni wengi kupita kiasi ambao walionekana kushindwa kujizuia kushangilia kwa vifijo na ndelemo wakati onyesho hilo likiendelea. Baada ya movie kumalizika zoezi la upigaji picha katika red carpet liliendelea hadi hapo mid night ambapo wadau walijirusha katika kiota kipya cha maraha hapa Atlnata "The Valley International"".

Ratiba ya onyesho la movie hii inaendelea kama kawaida kwa kufuatiwa na Houston, TX. hapo tarehe 26 siku ya Thanksgiving. Washington DC hapo tarehe 5 december. Na kufuatiwa na Minnessota wiki mbili baadae kabla ya kuelekea Esat Africa na Europe.

Waratibu wa shughuli hizi wanapenda kutoa shukrani zao za dhati kwa wadau wote waliojitokeza na wale walioshindwa kujitokeza kutokana na kubanwa na miangaiko ya dunia. Pia shukrani za dhati zikuendee wewe Mr. Michuzi kwa ushirikiano wako katika kufanikisha shughuli hizi na mungu akuzidishie. Kwa picha zaidi pitia
or
Hadjihelper
wa Globu ya Jamii
mastaa wa filamu hiyo
mambo ya red carpet

mastelingi wakila pozi
kila mtu alifurahia fanaka ya uzinduzo wa babypowder





 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 19
libeneke la globu ya jamii
timu nzima ya Globu ya Jamii imefarijika kuona sasa libeneke linatambulika rasmi kiasi hata cha kualikwa kwenye matukio mbalimbali, la karibuni likiwa ni hili la Mo Ibrahim juzi jijini Dar. Globu ya Jamii inatoa shukrani kwa Mo Ibrahim Foundation kwa kutambua libeneke la globu pamoja na taasisi kadhaa zingine ambazo nazo zinaheshimu kazi ya mabloga na kuwaalika sambamba na wanahabari wa vyombo vingine. hii ni hatua ya kutia moyo na nawaasa wana libeneke wenzangu wakaze buti na globu zao kwani kuna mwanga mwisho wa korongo.
-Michuzi

 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 15
Sababu za watu kutozeeka mapema

Kaka Michuzi,

Na mimi leo naomba kuwakumbusha wanajamii umuhimu wa kunywa chai. Najua wengi yumkini wanafahamu ila ninaona bado kuna haja ya watu kuelewa umuhimu huu.


Ukiangalia hata kwa nchi zilizoendelea, watu wengi unakutana nao mitaani wana nguvu zao hata vikongwe (zaidi ya miaka 70 hata 80) wanafanya shughuli zao na wako wakakamavu, tofauti na kwetu Tanzania.


Wenzetu wanakadesturi ka kupenda kunywa chai mara kwa mara (hata mara kumi kwa siku!) na wanapenda sana chai ya rangi (tofauti na kwetu Tanzania watu wengi tunapenda chai za maziwa)
NAWASILISHA.
------------------------------------------
Antioxidants, and How They Help Your Health
Few people would argue the fact that tea is good for you, and green tea is the best form of it for your health. One of the components of tea that make it so healthy, are the antioxidants. Alright, so tea is packed with antioxidants. What exactly are they, and what have they done for me lately?

Oxidation is a normal process that takes place in the body. It causes damage to our cells, and it's believed that this cumulative damage is what causes aging and eventually death. It happens as a result of regular metabolism, but is accelerated by pollution, excessive exposure to sunlight, alcohol and smoking. A free radical is a charged atom or a piece of a molecule. In order to re-establish its own stability, a free radical looks to steal an electron from its surroundings.

This usually means from one of your own healthy cells. You end up with a little bit of DNA damage, or a protein becomes dysfunctional. It may not seem like much, but all these little damages add up. Antioxidants are chemicals that generously offer up their own electrons to the free radicals, thus sparing you the cellular damage.

Every time they neutralize a free radical, the antioxidant loses an electron and stops being able to function as an antioxidant. This is why you must continually resupply your body with the vitamins and other chemicals that act as antioxidants.

There are many chemicals that perform as antioxidants, such as vitamins C and E, beta-carotine, and selenium. You can get these from all kinds of nuts, fruits, vegetables and meats. The specific kind of antioxidants found in tea is called phenols, and they can also be found in a variety of berries and grapes.

Mdau DJM
Liverpool, UK
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 14
matukio mbalimbali rukwa
WANAFUNZI wa Shule ya Sekondari ya Msakila High School katika Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa wakishiriki katika ujenzi wa uzio wa shule yao kwa njia ya kujitolea leo
MAFUNDI wakijenga daraja lililopo maeneo ya Majengo katika Manuspaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa hivi leo. Daraja hili limeharibiwa vibaya kutoka na mvua kubwa za msimu uliopita na zinazoendelea kunyesha msimu huu katika maeneo mengi mkoani humo.
Picha na mdau wa Rukwa Peti Siyame









 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
kumbukumbu ya tobi jibaba jumapili hii dar
Tarehe 19/11/09 mpendwa wetu Toby Jibaba anatimiza miaka mitatu kaburini na kutakuwa na misa katika kanisa la St. Joseph saa saba mchana na baadae kwenda makaburini.
Siku ya jumapili tarehe 22/11/09 kutakuwa na misa ya shukrani nyumbani kwao Ocean Road jijini Dar kuanzia saa tano asubuhi na baadae chakula cha mchana kwa pamoja. Ndugu, jamaa,majirani na marafiki wote wanakaribishwa siku hiyo.

Kwa niaba ya familia,
mimi ni dada wa Jibaba
Catherine Magambo
0783932393
0754814115(Mama Magambo)
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
MEMORIAL SERVICE,WASHINTON DC

Tujumuike na familia ya Elias Stafford Mshana(Massawe) katika ibada jumapili november 22 saa nane mchana(2:00pm) ya kumuombea mama yao mpendwa Bertha Stafford Mshana aliyefariki nov 12/2009 katika hospitali ya KCMC,Moshi Kilimanjaro na kuzikwa november 16/2009,Moshi,Kilimanjaro

Ibada itafanyika
Good Samaritan Lutheran Church,
10110 Greenbelt Road,
Lanham,Md,20706.
Sisi tulikupenda lakini mwenyezi Mungu amekupenda zaidi,ukae katika amani mpaka hapo mwenyezi Mungu atakapo tukutanisha tena,yeye alitoa na yeye ametwaa,jina lake lihimidiwe.

Kwa maelekezo zaidi,wasiliana:
Marco Mbullu 571 426 7124,
Elvis Saria 301 213 0657,
Elias Stafford 301 646 5683
Ray Abraham 301 793 4467
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
TAARIFA KWA UMMA.
MABADILIKO YA SIKU YA TAIFA KUPANDA MITI

Serikali imebadilisha Siku ya Taifa ya Kupanda Miti kutoka Januari Mosi ya kila mwaka na kuwa Aprili Mosi. Mabadiliko hayo yametokanana Waraka wa Waziri Mkuu Na 1 wa mwaka 2009 kuhusu kubadili Siku ya Taifa ya Kupanda Miti kutoka Januari Mosi na kuwa Aprili Mosi ya Kila mwaka.

Kwa mujibu wa waraka huo, kuanzia mwaka 2010 Siku ya Taifa ya Kupanda Miti itaadhimishwa Aprili Mosi ya kila mwaka. Waraka huo unaanza kutumika rasmi tarehe 01 Juni, 2009 na unafuta waraka wa Waziri Mkuu Namba 1 wa Oktoba, 2000.

Uamuzi wa kubadilisha siku hiyo unatokana na mapendekezo yaliyotolewa na Mhe. Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Januari Mosi 2008 aliposhiriki maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Kupanda Miti na kutaka maadhimisho hayo yahamishiwe kipindi ambacho sehemu nyingi za nchi zitakuwa zinapata mvua.

Kwa mujibu wa waraka huo, Aprili Mosi itakuwa ni siku ya Taifa kuhamasisha upandaji miti huku kila mkoa ukiendelea kujipangia Siku ya Kupanda Miti kutokana na majira ya mvua yatakavyoruhusu. Ili kazi ya kupanda miti iwe inatekelezwa na wadau wote, Waraka huo umeagiza Wizara, Mikoa, Wilaya, Viongozi wa wilaya, Halmashauri za Jiji, Manispaa na Mamlaka za Miji midogo, Tarafa, Kata, Vijiji na mitaa kuandaa programu za utekelezaji mapema iwezekanavyo.

Maafisa Misitu walioko mijini, mikoani, wilayani na vijijini wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu aina ya mbegu na miche inayofaa katika eneo husika na kushauri utayarishaji wa vitalu vya miche kwa wakati unaofaa.

Waraka umemtaka kila kiongozi ahakikishe zoezi la upandaji miti linatekelezwa na kusimamiwa ipasavyo kwenye eneo lake. Aidha, pamoja na masuala mengine kiongozi atapimwa kutokana na juhudi zake za kuhamasisha, kutekeleza na kusimamia wananchi kupanda miti. Halmashauri zote kwa kushirikiana na mamlaka husika, zihakikishe kuwa upandaji miti ni pamoja na kupanda kando kando ya barabara zote nchini.

Waraka huo umetahadharisha kuwa kupanda miti pekee hakutoshi kukabiliana na jangwa kama hatua za makusudi za kutunza na kulinda uoto wa asili hazitachukuliwa. Siku ya Taifa ya Kupanda Miti iliadhimishwa kitaifa kwa mara ya kwanza mwaka 2001 katika eneo la Jangwani mkoani Dar es Salaam.


Ezekiel Maige (Mb)
NAIBU WAZIRI
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
dogo wa uswazi leo

 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
tamasha la sauti za busara 2010 laiva!
Mtanange wa saba wa tamasha la Sauti za Busara ambalo hufanyika Zanzibar kila mwaka itakuwa ni kuanzia tarehe 11 hadi 16 Februari 2010; hakutakuwa na kiingilio kwa watakaoingia kabla ya saa kumi na moja.
Sauti za Busara ni tamasha la kimataifa ambalo linautambulisha na kuutangaza muziki wa Afrika Mashariki, na ambalo hufanyika katika kila wiki ya pili ya mwezi wa Februari kila mwaka kisiwani Zanzibar.
Kwa habari kamili...
BOFYA HAPA
Mwanamuziki Fresh Jumbe anayeishi na kufanyia kazi zake huko Japan ni mmoja wa Nyota wa kimataifa wataopamba tamasha la sauti za busara mwaka huu. Mcheki kwenye http://freshjumbe.com



 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
Mh. sitta amtembelea Dk. Migiro New York
Spika wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe.Samuel Sitta akisalimiana na Naibu katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dr. Asha - Rose Migiro alipomtembelea ofisini kwake, makao makuu ya Umoja huo mjini New York Marekani leo. Spika yupo Jijini New York kuhudhuria Mkutano wa pili wa kamati ya maandali ya mkutano wa Maspika wa Mabunge Duniani utakaofanyika Julai 2010 huko Geneva. Chini wakiwa na Afisa habari wa Bunge Owen Mwandumbya wa Bunge.



 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
kahawa ya kenya made in TZ
Hello Ndugu Michuzi!
Naitwa Daniel, ni mtanzania niliyepo Korea ya Kusini nasoma.
Niliingia kwenye mgahawa (coffee bean) hapa jijini Seoul, kupata kawaha kidogo manaake hivi sasa huku baridi ya kufa mtu.
Nikakuta tangazo ambalo linaloonesha kuwa ati mlima Kilimanjaro upo Kenya na kwamba kahawa ya Kenya inalimwa maeneo hayo. Nakutumia picha ya tangazo lenyewe uwahabari watanzania wenzetu waone tunavyonyongwa na hawa watani wetu wa jadi.
Mdau Daniel,
Seoul –Korea.
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 19
utapeli sampuli mpya bongo??
Ndugu wapendwa,

Story ifuatayo ni ya kweli maana imenitokea mimi binafsi jana tarehe 11/11/2009. Najua kwa kiasi fulani itakuwa inaninizalilisha kwa kutokuwa makini lakini naona ni vyema niwashirikishe rafiki zangu ili msije mkatapeliwa kama mimi na wengine wengi wameshatapeliwa kama vile ndugu yake Galeba, laiti Galeba angeweza kutuelezea yaliyomsibu ndugu yake labda na mimi ningeweza kuepuka utapeli huu. Kinchosikitisha matapeli wenyewe ni watu wanaotufahamu vizuri.
-----------------------------------------------
Mnamo muda wa saa tano asubuhi nikiwa nyumbani (nipo likizo) nikapokea simu nisiyoifahamu kutoka kwa mtu ambaye alijitambulisha ananifahamu, na kwa jinsi alivyonitaja kwa jina na career background details zangu sikuwa na shaka kwamba hanifahamu. Mazungumzo yalikuwa kama ifuatavyo:

TAPELI: Mr. Alex Matovu habari za siku nyingi.
Mimi: Nzuri
Tapeli: Vipi bado unafanya kazi Blue Financial Services?
Mimi: Hapana, nani mwenzangu?
Tapeli: John, nilikuwa nafanya kazi Wizara ya elimu, na uliwahi kunisaidia nikapata mkopo, ila kwa sasa nipo World food programme, Kigoma kama Chief supplies officer.
Mimi: okay sasa nikusaidie nini John (ukweli nikwamba sikumkumbuka ila kwa kuwa tulikuwa tunatoa mikopo kwa wafanyakazi wa serikali, siku jiuliza sana , after all alikuwa hajasema anachotaka)

Tapeli: Sasa nina issue naomba unisikilize kwa makini, kama unavyofahamu WFP tunatoamisaada ya vyakula hivyo tuna maghala makubwa ya kuhifaadhi chakula, hivyo ili kuhakikisha vyakula haviharibiki huwa tuna weka presavative inayoitwa Damoline Liquid solution made in Sweeden, hii inapatikana MSD na kwa licensed dealers kama Mohamedi Enterprises. Kwahiyo tuli float tender mwaka jana na supplier aliyeshinda tulikubaliana anipe 10% lakini baada ya ku supply hayo madawa akanidhulumu na kunitisha kuwa iwapo nitamdai hiyo 10% angeniripoti kwa mabosi wangu. Kwa hiyo sikuwa na cha kumfanya bali kusubiri contract yake iishe alafu nimtafute supplier mwingine. Sasa ndio nikaona nikupigie ndugu yangu maana nakujua wewe hii kazi utaweza kuifanya ukizingatia unalipwa cash on delivery!

NOTE: nimeshawahi ku deal na supplies officer wengi hivyo sikuwa na doubt yeyote, bali nikaona hii is just another deal kama ambazo nimeshawahi kufanya successfully.

Mimi: Okay sasa unataka nifanye je?

Tapeli: Unachotakiwa kufanya ni kwenda MSD umuone Dr. Shija, huyu ndiye mkuu wa hapo na ndiye aliyekuwa supplier wetu wa zamani aliye ni dhulumu, sasa kwa kuwa sitaki kumpa kazi tena, wewe uende ujifanye unaulizia hiyo liquid solution, na u negotiate ujue atakuuzia shillingi ngapi. Kwahiyo nakutumia simu yake mpigie muongee akupe quotation, alafu akisha kupa bei nipigie ili nikuelekeze cha kufanya.

Basi wandugu nikampigia dr. shija, mwanzoni shija ana hesitate kuzungumza na mimi aki pretend kuwa hapendi kuongea na strangers na akataka kujua namba yake nimeipataje, sasa kwa kuwa siwezi kumwambia ukweli kuhusu aliyenipa namba yake, ikabidi na mimi niwe muongo kwa muda, nika pretend kuwa mimi ni mkulima na nahitaji hiyo presavative kwa ajili ya maghala yangu yaliyopo arusha. Basi akawa na imani na kukiri kuwa anayo stock yakutosha, na hiyo liquid inauzwa kwa pair ya chupa mbili zenye ujazo wa 1000mls, kila pair ni 1.2m. Sasa angalia nilivyoingia katika mtego, baada ya kunipa bei ni kaomba punguzo na akasema atauza kwa 1million.

Nikafanya kama nilivyoelekezwa na John wa WFP kuwa baada ya kupata bei nimjulishe nilivyomjulisha akasema kinachofuata ni kuwa mimi nitauza kwa USD. 1700, na tofauti kwa maana ya faida tutagawana, hivyo nisubiri aniunganishe kwa bosi wake for further final details.

Basi wandugu kama mnavyonijua katika issue za fwedha, nikachukua calculator ya simu ili nijue deal ina shillingi ngapi, hela zilivyokuwa nyingi hata calculator iligoma, maana WFP wanahitaji 50 pairs @ usd 1700, mimi nanunua kila pair kwa 1million ambayo ni kama usd 770 hivyo difference usd 930 x 50 pairs = USD 46500, ALAFU tunagawana pasu pasu. Guys you can imagine what was going on in my head!

Basi kweli muda si mrefu nikapigiwa simu na huyo bosi wake ambaye ni mzungu na mazungumzo yalikua kama ifuatavyo:

MZUNGU: This is Mr. Scheinder from WFP, are you the new supplier?
MIMI: YES
MZUNGU: Do you have enough stock of Damoline Liquid solution, we are looking for 50 pairs?
MIMI: Yes I have sufficeint stock
Mzungu: what is your price per pair?
Mimi:$1700
Mzungu: ahaaaaaaaa thats a very good price, do you want to be paid in dollars or TZS
MIMI: Dollar of course, you how how unstable the local currency is ( Hapo tena na mimi nataka kuonyesha kuwa ni International businessman)
Mzungu: No problem, we have enough dollars, you want to be paid cash or by cheque?
Mimi:Cash
Mzungu: Okay no problem, now listen very carefully mr. new supplier we need this liquid urgently possibly today, and since you have said you have enough
stock we are taking off this morning from Kigoma coming to Dar, please arrange for the transport to take us to Movenpick, we will pay usd. 200 for your fuel, but most importantly make sure you bring one pair of the sample with you.
Mimi: No problem at all I have been in this business for quite sometime now you can be sure everthing will be fine.

Masikini bila kujua nimeingizwa kingi, nikachukua cheque book, nikaandika cash withdraw 1million ili nikanunue sample yakwenda kuwaonyesha wateja wangu. Baada ya kutoka bank nikampigia dr. shija ili aniuzie hiyo sample, akasema kwa sasa ametoka ofisini ila sample anazo katika gari na alikuwa anaelekea Mwananyamala hosp, then Magomeni alafu Muhimbili, hivyo tukutane Magomeni hosp. Yaani jinsi nilivykuwa naendesha gari basi hata kama ni mashindano ningeweza kushinda, basi mimi mbio mpaka magomeni hosp namsubiri dr. shija. Nikampigia akasema yupo ndani hospitalini na yupo na mabosi wake asingeweza kutoka ila anamtuma kijana wake nimpe hizo fedha na yeye anipe hizo dawa, kweli ikawa hivyo kijana akaja akaingia kwenye gari nikamwambie anipe hizo sample kwanza nikazisoma ziko exactly kama WFP wanavyotaka! NIKAKABIDHI HELA 1 MILLION. Bila hata aibu yule kijana akaniomba 50,000/= nikamwambie asijali maana deal kubwa itakamilishwa saa nane.

Kwa kuwa wageni wangu walishaniambia niwaaandalie usafiri, nikampigia dreva tax wangu aje airport saa nane, nikamuuliza bei kutoka airport mpaka movenpick ni ngapi akasema 25,000 nikamwambia usijali ntakupa 50,000/=!!!!!!!!!!!!! (kumbuka mimi ntalipwa usd 200 ya usafiri).

Basi mimi mbio nikaenda airport terminal one kusubiri ndege ya WFP ili tumalize biashara, nilipofika kuulizia reception nikaambiwa hakuna kitu cha namna hiyo na mimi ni mtu wa 10 kutapeliwa, basi tena nikajirudia kimya kimya. Nikaenda kula chefs pride nikamsimulia jamaa mmoja yaliyonisibu, kabla sijamaliza akasema hata ndugu yake ametapeliwa wiki iliyopita, nikampigia Galeba akasema yeye jamaa yake alipigwa 3.5m last week.

Taarifa nilizonazo mpaka nikuwa hii ni network ya wahaya na mpaka sasa ni wahaya wengi wameishaibiwa ukilinganisha na makabila mengine.

So guys thats my story for yesterday!

Foward to everyone you know.
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 71
mh. burian na ujumbe wa EU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Batilda Burian akizungumza na Ujumbe wa Umoja wa Ulaya{EU} kulia kwa Waziri ni Balozi wa Sweden Bw Staffan Herrstrom na Balozi wa Jumui ya Ulaya Bw Tim Clarke uliomtembelea na Kumweleza msimamo wao Kuhusu Mabadiliko wa Tabianchi kuelekea Mkutano wa Denmmark. Picha na Ali Meja
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
kumbukumbu ya kumuaga mzee robert lugarema feruzi
NDUGU ZETU,

Tunapenda kuwajulisha kwamba kutakuwa na kumbukumbu ya kumuaga Marehemu, Mzee Robert Lugarema Feruzi, kabla ya kusafirisha kwenda nyumbani Tanzania, itakayofanyika Jumamosi, tarehe 21 November, 2009.

Mahali:
Faggas Funeral Home, 551 Mt. Auburn St, Watertown, MA 02472
Toll Free 1-800-222-2586 or 617-926-2163

Muda:
3pm to 5pm (Tisa mchana mpaka kumi na moja jioni) - tafadhalini tuzingatie muda.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na:

Bw. Innocent E. Lugumamu 978 996 7690
Bw. Steven Buberwa Mutasa 603 320 3220
Bw. Crispine Kahabuka 603 261 0802

Kwa maelezo zaidi pia, tembelea
www.faggas.com.

Ratiba itasambazwa siku hiyo ya "WAKE"
Tunatanguliza Shukrani zetu.
Steven Mutasa.
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
MISA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU TOBI aka JIBABA, MILTON-KEYNES
Milton Keynes TZ Society invites you for a prayer to commemorate our beloved Brother,Family & Friend TOBY aka JIBABA.
Its 3yrs Since His tragic Death. The Ceremony will be held on Sat 21st November, 2009 @ Jesus Celeb Centre,
Lloyds Court,
Central Milton Keynes,
MK9 3AT(Formerly Known as Flames)
from 2pm-6pm...
For more info please Contact
07899 784806/07897 362757....
 
© Michuzi | Wednesday, November 18, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
Tuesday, November 17, 2009
mapacha wanne kuzindua albamu mwisho wa mwezi huu

MAPACHA WANNE - CHOKORAA, CHAZ BABA, JOSE MARA NA KALALA JNR
WAMEJIPANGA KUFANYA MAAJABU YA KUTIKISA ULIMWENGU WA MUZIKI NCHINI TANZANIA KWA KUTAMBULISHA ALBAMU YAO TAR 30/11/09 KATIKA UKUMBI WA KINONDONI STEREO. WANAOMBA SAPPORT KWA MASHABIKI WA MUZIKI WA DANCE
NDANI NA NJE YA NCHI
 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 22
wanafunzi 95 wajipatia zawadi za NBM
Jimmy Mfuru (kulia) akibonyeza kitufe cha kompyuta wakati wa droo ya kwanza ya kuwatafuta washindi wa akaunti ya wanafunzi ya benki ya NMB iliyochezeshwa Dar leo ambapo jumla ya washindi 95 walijishindia zawadi za Mabegi ya shule, Simu za mkononi na muda wa maongezi. Kushoto ni Meneja Mwandamizi wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Imani Kajula.


Meneja Mwandamizi wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Imani Kajula, akiongelea zawadi hizo akiwa na maafisa waandamizi wa benki hiyo.

 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
JK akiwa mkutanoni Rome
JK akisalimiana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mh. Ban Ki-Moon jijini Rome leo wanakohudhuria mkutano wa wakuu wa nchi kwa usalama wa chakula
JK akiongea na Waziri wa Kilimo na Chakula Mh. Stephen Wasira na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mazingira na Ushirika wa Zanzaibar Mh. Burhani Saadat Haji wakati wa mkutano huo
JK akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa FAO Mh. Jacques Diouf na baadaye kufanya maongezi ofisini kwake jijini Rome, Italy, asubuhi ya leo


JK akisalimiana na rais wa Burundi Mh. Pierre Nkurunzinza ambaye naye anahudhuria mkutano wa wakuu wa nchi kuhusu usalama wa chakula duniani jijini Rome, Italy

 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
mh. spika ziarani marekani
Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta akihudhuria kikao cha kamati ya maandalizi ya kongamano la Maspika kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na umoja wa Mabunge Duniani IPU katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York
Spika wa Bunge akiwa katika picha ya pamoja na balozi wa Uingerza UN Mhe. Philip Parham (katikati) katika hafla iliyoa nae kwa baadhi ya mabalozi mara baada ya kuhuduria kikao cha kwanza cha cha kamati ya maandalizi ya kongamano la Maspika kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na umoja wa Mabunge Duniani IPU mkutano unaofanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani. Kushoto ni balozi wa wa kudumu katika umoja wa mataifa toka Tanzania Dr. Augustine P. Mahiga. Mhe. Philip Parham kabla ya kuamisjhiwa New York alikuwa balozi wa Uingereza nchini Tanzania. Picha ya chini Mh. Sitta akiteta jambo na Bi. Ashura Duala (kulia) katika hafla iliyoa andaliwa na balozi wa Uingereza UN mjini New york mara baada ya kuhuduria kikao cha kwanza cha cha kamati ya maandalizi ya kongamano la Maspika kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na umoja wa Mabunge Duniani IPU mkutano unaofanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani. Katikati ni balozi wa kudumu katika umoja wa mataifa toka Somalia ambaye pia ni mume wa Bi Ashura Mhe. Elmi Duala.
Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta akijadili jambo na na balozi wa wa kudumu wa umoja wa mataifa toka Tanzania Dr. Augustine P. Mahiga alipomtembelea ofisini kwake leo. Mh. Spika yupo Marekani kuhuduria kikao cha kamati ya maandalizi ya kongamano la Maspika kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na umoja wa Mabunge Duniani IPU mkutano unaofanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York.





 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
msiba dar, rome na bukoba
Ndugu Andrew Kyabashasa wa Rome, Italy anasikitika kutangaza kifo cha kaka yake Mzee Godfrey Kyabulyo kilichotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 17 November 2009 Katika Hospitali ya Mikocheni, Dar Es Salaam.
Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Burugo, Bukoba kwa ajili ya mazishi inafanyika Ada Estate Kinondoni nyumbani kwa binti yake Winifrida Kyabulyo.

Mungu alitoa, na Mungu ametwaa jina lake lihimidiwe.
Kwa niaba ya Watanzania hapa Roma na Italia kwa ujumla tunakupa pole. Mwenyezi Mungu amlaze Marehemu Mzee Godfrey Kyabulyo Mahali Pema Peponi. Amina

Andrew Mhella
Katibu wa Watanzania Italia Tawi la Roma
Source: www.watanzania-roma.blogspot.com
 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
MZEE ABUSHIRI KILUNGO HATUNAYE TENA
HAYATI ABUSHIRI KILUNGO

MZEE ABUSHIRI KILUNGO (PICHANI) AMEFARIKI DUNIA USIKU WA KUAMKIA LEO NYUMBANI KWAKE TANDIKA,MTAA WA KIVUNGO BAADA YA KUUGUA UGONJWA WA KISUKARI KWA MUDA MREFU.

MAREHEMU KILUNGO AMBAYE ALIWAHI KUWA NAIBU MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM MIAKA YA NYUMA NA PIA ALIWAHI KUWA MWENYEKITI WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA DAR (DRFA).

MAREHEMU KILUNGO AMEACHA MKE NA WATOTO WATANO WATATU WAKIWA NI WA KIUME NA WAWILI WA KIKE.MAZISHI YATAFANYIKA LEO (17/11/2009) SHAMBANI KWAKE TUANGOMA,NJE KIDOGO YA JIJI LA DAR.

TUNAMUOMBEA KWA MWENYEZI MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU MZEE WETU ABUSHIRI KILUNGO MAHALI PEMA PEPONI

-AMIN

 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
vodacom tanzania boss dietlof mare honoured in iringa
VODACOM Tanzania Director Dietlof Mare, being presented with a traditional spear by Ismani village elder in Iringa Rural district, as a sign of the village’s appreciation of the firm’s contribution to the development of the constituency.
Photo by Frank Leonard.
 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
msiba boston, massachusetts
MZEE ROBERT L. FERUZI
1946-2009

Ndugu, jamaa na marafiki, Tunasikitika kuwajulisha ya kuwa Mzee Robert L. Feruzi was Boston-Masachusetts amefariki dunia siku ya Jumapili [Nov 15th 2009] asubuhi hapa Boston,USA.

Taratibu na mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Dar es salaam kwa mazishi zinafanyika nyumbani kwake
98 Itasca St,
Mattapan, MA

Tunawaomba ndugu zetu mtusaidie kuchangia fedha kwa ajili ya kuwezesha kusafirisha mwili wa marehemu kurudi nyumbani kwa mazishi. Gharama za kuhifadhi mwili,kusafirisha mwili, Jeneza pamoja na gharama zingine ambazo kwa kawaida huja na haya matatizo.

Unaweza kusaidia kutuma mchango wako kwenye Account ya wafiwa kama ifuatavyo:

Innocent E. Lugumamu
BANK OF AMERICA,
ROUTE NUMBER :011000138
ACCOUNT NUMBER:004628572563
Address: 12 Walker St, Lowell, MA 01854

IMPORTANT: Kwa wale waliopo nje ya state ya Massachusetts, Out of state deposit circle (zungushia) namba 77 , MA. Unapotuma pesa. (haya ni maelezo muhimu toka kwa bank of America)

Kwa mawasiliano zaidi unaweza kuwasiliana na wafuatao:
Innocent E. Lugumamu 978 996 7690
Steven Buberwa Mutasa 603 320 3220
Crispine Kahabuka 603 261 0802

TUNATANGULIZA SHUKRANI ZETU.
Email-Address:-
au
stevebube@gmail.com




 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 16
nadia car for sale
Toyota Nadia
Type SU L Widebody Aero,
2000 year,
SXN10-0044572,
78k kms,
Metallic Pearl white colour,
Automatic transmission,
2000cc petrol, Air con., Pwr steering,
Pwr windows, Pwr locks, Pwr mirrors, Radio, CD, Mini Disc, Alloy wheels, Rear spoiler, Double Airbags, ABS, Rear hi stop lamp, Rear wiper, Fog lamps, Door visors.
ALL DUTIES FULLY PAID!
Price: US$ 10,000 – NEGOTIABLE!
DRIVEN BY A LADY,
ONLY 4 MONTHS SINCE IMPORTATION on 30 June 2009,
in IMMACULATE CONDITION
Reason for selling: Just bought another car
PLEASE CALL 0784 444 668












 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 7
richa adhia alonga

SWALI: Ni tukio gani la kihistoria unalokumbuka na watanzania watalikumbuka pia?

RICHA: Ni pale niliposhinda taji la Miss Tanzania na kuibua mtazamo tofauti kwa wengi kutokana na rangi yangu. Pia ilisaidia kufungua macho ya watanzania wengi kwa sababu hawakudhani kama mimi nitashinda lakini ikawezekana. Tukio hili llitabaki kuwa la kihistoria kwa sababu haijawahi kutokea na sidhani kama itatokea tena.

SWALI: Ni wakati gani mgumu unaukumbuka katika maisha yako?

RICHA: Siku kumi kabla ya mashindano ya Miss Tanzania aliyekuwa rafiki yangu wa kiume alipata ajli ya gari na kufariki. Sitaweza kulisahau tukio hilo kwani lilinifanya nitake kujitoa kwenye mashindano,lakini familia yangu ilinipa ilinipa moyo na nikaendelea na mashindano.
Kwa Mahojiano kamili
 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
from china with love



Kaka Issa hebu wafungue macho ndugu zetu
wanaokimbilia China halafu visa inaisha...
 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 16
dogo wa uswazi leo

 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
Taarifa ya mkutano wa Jumuiya Tokyo
Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Japani (Tanzanite society) unapenda kuwaarifu kuwa, kutakuwa na mkutano mkuu wa mwisho wa mwaka wa Wanajumuiya wote utakaofanyika:

Tarehe: 6/12/2009
Mahali(Ukumbi) : odasaga plaza (Odakyu sagamihara station)
Muda: Kuanzia saa 12:15 jioni

Agenda za mkutano huu ni kama zifuatazo:
(1)Kupata taarifa mbalimbali za maendeleo ya Jumuiya. (i.e Kuisajili Jumuiya kuwa NGO)
(2)Kujadili na kutathmini zoezi la ulipaji ada za kila mwezi.
(3)Kujadili na kuamua kuhusu kutenga fedha kwa ajili kusaidia wenye shida nyumbani Tanzania. (4)Mengineyo.

Uongozi unapenda kuchukuwa fursa hii kuwakumbusha wanajumiya kuwa, kama tulivyokubaliana katika mkutano uliopita, kwa wale wote watakaochelewa kufika kwenye mkutano au wasiofika bila kutoa taarifa rasmi kwa uongozi watatozwa faini.

Mkutano utaanza rasmi saa 12:15 jioni, tunaomba kuzingatia muda.

Taarifa za kutoweza kufika kwenye mkutano zipelekwe kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya Bw Julluis Mwombwki :
Simu: 09041304754
Email ya simu:jullius57@ docomo.ne.jp
Email:jlmwombekijnr@gmail.com

(NB) Ili kudhibiti nidhamu kwenye mkutano huu, wale wote wasio wanachama(Wanajumui ya)
hawataruhusiwa kuingia kwenye chumba cha mkutano.

Ahsanteni
Uongozi,
Jumuiya ya Watanzania
Wanaoishi Japani( Tanzanite Society)
 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
flaviana matata pours her heart on top US ebrity blog
Flaviana Matata with one of the many orphans she had visited during her tenure as Miss Universe Tanzania. Following is an excerpt of an article she posted on www.globalgrind.com which is one of the most top celebrity blogs with authors like Russell Simons and Bill Cosby. If the responses to Flavy's post are any indication, this home girl is going places. Watch this space.
Oftentimes, children in many parts of the world, leave home without breakfast and this leads to the weakening of their immune system, and acquiring curable diseases like malaria, diarrhea, and cholera. Education is key to a better life for a society because children learn not only for themselves but for their future children and generations to come.
So, it is important for Americans to show how education is important to their children by explaining that every day in school is a blessing for many children in parts of the world who strive for it. Food, shelter and clothing are basic needs yet they are privileges in many cases.
-Flaviana
To read the whole piece
 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
yanga yahitimisha duru la kwanza kwa ushindi mnono
Beki wa Yanga, Fred Mbuna (kushoto) akimtoka mchezaji wa Tanzania Prisons, Dickson Oswald wakati timu hizo zilipokutana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es salaam. Yanga ilishinda 4-2. Duru la kwanza limemalizika na ligi itaendelea mwezi wa kwanza mwakani.
Mshambuliaji wa timu ya Yanga, Mrisho Ngasa (kushoto) akimiliki mpira huku akizongwa na beki wa Tanzania Prisons, David John katika mchezo wa ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar, Novemba 16.2009. Yanga ilishinda 4-2.
Picha na Francis Dande wa Globu ya Jamii


USHINDI wa mabao 4-2 dhidi ya Prisons umewawezesha mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga, kumaliza mzunguko wa kwanza wakiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Yanga sasa inasubiri kuanza mzunguko wa pili Januari mwakani ikiwa na pointi 21 sawa na Azam inayoshika nafasi ya pili kwa uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Kwa habari kamili





 
© Michuzi | Tuesday, November 17, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
Monday, November 16, 2009
JK ahutubia mkutano wa usalama wa chakula leo
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia mkutano
wa wakuu wa nchi kuhusu usalama wa chakula jijini Rome, Italy
Na Mwandishi Maalum,

Rome, Italia

Ni jambo aibu kwamba bado watu wanaendelea kufa kwa njaa duniani, bila sababu ya maana, kwa sababu dunia inacho chakula cha kutosha kuweza kumulisha kila binadamu, Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema leo, Jumatatu, Novemba 16, 2009.

Akihutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi Kuhusu Hali ya Usalama wa Chakula Duniani katika makao makuu ya Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) mjini hapa, Rais Kikwete amesema kuwa wakati umefika kwa dunia kukomesha aibu hiyo.

“Tokea nilipoanza kusoma hotuba yangu, kiasi cha sekunde 60 zilizopita, watoto kiasi cha kumi tayari wamekwishakufa kwa njaa. Ni dhahiri basi kuwa hatuna tena muda wa kupoteza katika kujaribu kukabiliana na balaa hili,” Rais Kikwete amewaambia wajumbe wa mkutano huo ulioanza leo asubuhi.

Ameongeza Rais Kikwete, “Ni aibu kubwa kwa upande wetu kwa mtoto ama hata mtu mwingine yoyote mzima katika kona yoyote ya dunia yetu hii kwenda kitandani akiwa na njaa ama kufa kwa njaa. Kuna chakula cha kutosha kwenye ulimwengu wetu huu kuhakikisha kuwa vifo hivyo havitokei.”

Rais pia amesema kuwa dunia inazo nyenzo na raslimali za kutosha, teknolojia mwafaka na ujuzi unaofaa kuweza kuzalisha chakula cha kutosha kwa sasa na hata katika miaka ijayo.

Amesema kuwa kinachotakiwa kwa dunia kutokomeza njaa duniani ni kwa kushirikiana na kuamsha ari muhimu ya kisiasa ili kuweza kukabiliana na changamoto hiyo.

“Kwa hakika ni jambo la kutia moyo kuwa Azimio la Mkutano huu tulilolipitisha asubuhi hii linathibitisha ari yetu ya pamoja kutaka kumaliza njaa wakati wa uhai wetu. Nimefurahi kuwa Azimio hilo limesisitiza umuhimu wa kurekebisha makosa ya kutokuwekeza kiasi cha kutosha katika “usalama wa chakula, kilimo na maendeleo.”

Rais Kikwete pia ametaka misaada ya maendeleo katika kilimo kuongezwa kwa kuwa imeshuka mno kutoka asilimia 19 mwaka 1980 hadi kufikia asilimia tano mwaka huu.

“Sasa ni wakati wa kubadilisha hali hii. Ningependelea kuwa katika Azimio letu tungeweka malengo na muda wa kufikia malengo hayo, ama hata kulenga kuongeza maradufu kiwango hicho cha uwekezaji wa sasa katika kilimo.”

Rais Kikwete pia amezitaka nchi zinazoendelea kuhakikisha kuwa bajeti za nchi hizo zinakuwa na fedha za kutosha kulingana na misaada itakayotolewa na nchi tajiri ili kuwekeza katika kilimo.

Akizungumzia kuhusu Tanzania amesema kuwa “kwetu sisi kilimo ni chakula na ni kila kitu katika maisha. Kiasi cha asilimia 80 ya watu wetu wote wanaishi vijijini na kilimo ndicho chimbuko lao kuu la maisha. Kilimo cha kisasa zaidi na chenye kuzalisha zaidi kitapunguza kiwango cha umasikini kidogo na kuongeza hali bora zaidi kwa watu wetu walio wengi.”

Rais Kikwete pia amesema kuwa uwekezaji katika kilimo utakuwa na athari kubwa na nzuri kwenye chumi za nchi masikini. “Wachumi wanabashiri, kwa imani kabisa, kuwa kila asilimia mia moja inayoongezeka kwenye uzalishaji wa kilimo, husababisha ongezeko la asilimia 1.6 ya nyongeza kwenye mapato ya asilimia 20 watu masikini zaidi katika kila nchi.”

Kuhusu uhusiano kati ya kilimo na tabianchi, Rais Kikwete amewaambia wajumbe wa Mkutano huo kuwa Tanzania ina matumaini makubwa kwamba Mkutano wa Tabianchi uliopangwa kufanyika mjini Copenhagen, Denmark, mwezi ujao, utafikia maamuzi muhimu yanayoweza kunufaisha kilimo na kubatilisha madhara ya tabianchi.

“Wakati tunapokutana kwenye Mkutano Kuhusu Usalama wa Chakula, lazima tukumbuke kuwa ajenda ya usalama wa chakula haiwezi kamwe kutenganishwa na ajenda ya mazingira,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:

“Kwa sababu ya madhara ya tabianchi, mienendo ya hali ya hewa imebadilika kabisa. Mvua hazitabiriki zaidi na hali ya ukame imekuwa mbaya zaidi na inayojitokeza zaidi. Hii imeathiri sana mazao, mifugo na usalama wa chakula kwa jumla. Mataifa yetu mengi na watu wake wanaotegemea kilimo sasa wamekuwa watu ambao maisha yao hayana uhakika na watu wa kutahayari zaidi.”

Rais Kikwete amekuwa miongoni mwa viongozi waliozungumza kwenye siku ya kwanza ya Mkutano huo wa siku tatu. Miongoni mwa viongozi wengine waliozungumza leo ni pamoja na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Baba Mtakatifu Benedict wa 16.
 
© Michuzi | Monday, November 16, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
ndolela chaseleleka
anajulikana kama Bw. Maringo a.k.a Ndolela Chaseleleka. Yeye ndiye bingwa wa tuzo ya Kili Music awards ya mwimbaji bora wa nyimbo za utamaduni. Ukitaka kumuona na kumsikiliza
 
© Michuzi | Monday, November 16, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 12
limo la iddi janguo lilivyoteketea: tatizo spea hamna?
Michuzi please watahadharishe wadau wanaopenda kunukua limo zisizo na vipuri ndani ya jiji la DSM Magari marefu yamekuwa yakiingia kwa kasi jijini .Mengi hayana spare mitaanai hivyo kuwekya spares za kubahatisha. Miezi kadhaa niliona hili limo likiwa limeungua kabisa mitaa ya Mikocheni,spare za kubahatisha zilichemka.
Limo nyingi sasa hivi zimepotea mitaani.
Mdau Lole wa Lole



kwa taarifa tu: mdau Lole wa Lole na wadau ni kwamba hilo ndilo lillilokuwa limo la kwanza la iddi janguo ambalo lilishika moto mapema mwaka huu maeneo ya Mikocheni Coca Cola jijini Dar. nimeongea naye kasema spea zipo kibao na kwake si taabu kuagiza nje na kwamba si kweli kwamba lilishika moto kwa sababu hiyo, bali ni hitilafu ya wayaring...
-Michuzi


 
© Michuzi | Monday, November 16, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 18
dogo wa uswazi leo

 
© Michuzi | Monday, November 16, 2009 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1


Idadi ya watu
eXTReMe Tracker