THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY TIGO THE LEADING MOBILE COMPANY IN TANZANIA THAT VALUE AND LISTEN ITS CUSTOMERS. | AND EASY FINANCE, THE MONEY PEOPLE | Karibu katika hii blog, Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Ila nawaomba tuweze kujieshimu kila mmoja wetu kwa kutumia lugha zisizo na matusi. Akhasante.

 

May 21, 2008
kaburi la banda


Hellow Mr. Michuzi,


nadhani u mzima. Ingawa siyo mdau wa Blog yako ila ni mfuatiliaji , msomaji na mpenzi mzuri sana wa blog hii. Sielewi sifa za kuwa mdau lakini tuyaache hayo ila nakutumia picha alipozikwa Rais wa Malawi Kamuzu Banda. Sijui ni kiasi gani cha fedha kilitumika kujenga kaburi hilo ila kweli wamalawi wameamua kumuenzi kiongozi wao huyo. Pamoja na yote sehemu hiyo ya kaburi imekuwa ni kivutio kikubwa kwa watalii wengi wafikapo huko malawi. Nami nilibahatika kufika huko kama mtalii wa kibongo. Sijui Baba yetu wa taifa alizikwa vipi ila naomba kama itawezekana tuwekee picha ya sehemu alipozikwa na kama ilishawahi kuwekwa tafadhali nijuze ni tarehe gani uliweka. Maana wengine hatujawahi fika butihama.

Kazi njema.
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 8
BALALI KUZIKWA IJUMAA MAREKANI

ALIYEKUWA GAVANA WA BENKI KUU DAUDI BALALI (PICHANI) AMBAYE ALIFARIKI DUNIA SIKU MBILI ZILIZOPITA HUKO BOSTON, MAREKANI, ANATARAJIWA KUZIKWA SIKU YA IJUMAA HUKO HUKO BOSTON.


HABARI ZA UHAKIKA KUTOKA MAREKANI NA NDANI YA BENKI KUU AMBAKO TAYARI MSIBA HUU MZITO UMETANGAZWA RASMI SASA HIVI, ZINASEMA HAYATI BALALI ALIFARIKI BAADA YA KUUGUA KWA MUDA MREFU.

MUDA NA MAHALI ATAPOZIKWA TUTAJULISHANA BAADAYE KIDOGO....
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 55
shoo ya muziki toka denmark

 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
libeneke washington dc

The time has come and the LINK Entertainment in conjuction with MAO(mlimani alumni association) and konyagiusa are proud to invite everybody to come and celebrate the birth of our entertainment company on may 31 in washington dc..


we would love to see u there...some of the proceeds of this event will help to facilitate the madawati project at mlimani primary school in tanzania...
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
msaada tutani
Hello Kaka Michuzi,
Habari yako. Naomba msaada. Naomba unitangazie kwa blog yako huyu mtu anaitwa Aston Kabeta (Tonny Kabeta).
Nina ujumbe wake muhimu sana. Number ya simu aliyotoa ni +1 267- 230 - 3999. Tumejaribu kupiga hiyo simu na anayepokea simu katika number hii hamjui huyu Tonny au Aston Naomba tafadhali uniwekee jamani hii ili kama kuna mtu anamfahamu au yeye mwenyewe akiona basi awasiliane na mimi. Nina ujumbe wake muhimu sana.
Asante sana na Mungu akuengezee kwa kazi hii unayofanya
Sara
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
balali
wadau kunradhi,

habari za aliyekuwa gavana wa benki kuu mh. balali nimezipata toka jana, ila bado sijazithibitisha, ingawa vyombo kadhaa vimerusha. tutapashana mara mambo yatapokuwa tayari.
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 12
kinga
nimefurahi kukuta mambo haya kwenye vyoo vingi vya ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa aicc, kuonesha kuwa wanaafiki kwamba kinga ni bora kuliko tiba. na hii siyo kwa nanihii tu bali pia hata fegi. huu ni mfano wa kuigwa, mnasemaje wadau - hala hala waosha vinywa msianze... huo mkono si wangu.....

 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 23
bagamoyo kumekucha!!

Mtanange wa kumtafuta mrembo wa wilaya ya Bagamoyo linatarajiwa kufanyika jumamosi hii tarehe 24.05.2008 kuanzia saa 1:30 katika hotel ya Kiromo View Resort & Hotel, iliyopo upande wa kulia kwenye barabara ya Dar- Bagamoyo, umbali wa takriban km 10 kabla hujafika mjini Bagamoyo.


Jumla ya arembo 10 wanaendelea na mazoezi katika hotel ya kiromo view resort & hotel iliopo kambi ya miss bagamoyo 2008 chini ya mkufunzi Neema Chande, miss Ruvuma 2007.


Warembo 10 waliopo kambini ni Amina Mlogwa, Time Salim, Ummy Mndolwa, Wilhelmina John, Zena Mohamed, Ashura Msese, Rose Kinyaha, Betty Kwezi, Dominica Chuwa na Claudia Massao.


Wana wa Akudo Impact, vijana wa masauti na mtindo wao wa pekechapekecha, ndiyo watakaosindikiza shindano hili linalotarajia kuwa la kipekee.
Viingilio katika shindano hili ni Sh. 10,000/= kwa viti vya kawaida na Sh. 30,000/= kwa viti maalum yaani v.i.p. Vituo vya kuuzia tiketi vitatajwa kesho siku ya Alhamisi tarehe 22.05.2008.


Usafiri wa kutoka Bagamoyo kwenda Kiromo utakuwepo siku ya tukio. Uhakika wa usalama utakuwepo na mashabiki wa mashindano ya urembo mnatakiwa mjitokaze kwa wingi.
Imetolewa na:
Kim H.M. Kimenya
Mkurugenzi Mkuu
KimKev Entertainment
Miss Bagamoyo
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
rugimbana na mfugale
wadau rugimbana (shoto) na mfugale wakiwa a-taun kwenye mkutano wa utalii. rugimbana ni mmoja wa wadau wakubwa wa sekta ya utalii na pia alikuwa kiongozi wa mchezo wa lawn tennis kwa miaka kibao wakati mfugale ndiye bosi wa hoteli za peacock
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 5
MKOMBOZI WA NAMBA ZA SIMU
NATUMAINI KILA MTU ANAFAHAMU ADHA ANAYOIPATA PALE ANAPO POTEZA SIMU UKWELI KIKUBWA KINACHOUMANI NAMBA ZAKO ZA SIMU ZINAKUWA NYINGI ZIMEPOTEA.
LEO HII KUNA VIFAA AMBAVYO UNAWEZA KUWEKA NAMBA ZAKO ZA SIMU 1000 NA KUKIHIFADHI NYUMBANI. CHOMBO HIKI KINA UWEZO WA KUCOPY NAMBA ZAKO ZILIZOKO KWENYE SIM CARD YAKO NAKUZIHIFADHI.
PIA KUKUONYESHA JINA NA NAMBA WAKATI UNAPOHITAJI KWA HARAKA.NIKITU AMBACHO KILA MMOJA WETU NAFIKIRI ANAKIHITAJI.
WASILIANA NASI KATIKA NO ZILIZOTAJWA HAPO JUU BEI NI NAFUU SANAAA PIA UNAWEZA KUPIGA NO 0712404044 KWA MAELEZO.
MDAU MKOMBOZI
 
© Michuzi Tarehe: 21.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
May 20, 2008
uso-kwa-uso na maprofesa
leo nimepata bahati ya kugongana uso-bin-uso na profesa pius z. yanda ambaye ni mmoja wa wasomi waliokuwa kwenye jopo la utafiti wa athari za mazingira duniani liliopelekea makamu wa rais wa marekani al gore kupokea tuzo ya nobel. profesa yanda, pamoja na kuwa pia mkurugenzi wa taasisi ya institute of resource assessment (www.ira.udsn.tz) ya udsm pia ni mkurugenzi wa afrika wa the pan african start secretariat (http://pass-africa.org)

niko na profesa wa uchumi, yaw nyarko, wa chuo kikuu cha new york university (http://www.nyarko.com/) cha marekani ambaye pia yupo a-taun kumwaga pepa katika mkutano wa kimataifa wa africa travel association juu ya hali ya uchumi katika sekta ya utalii na safari duniani



 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
jk alipotembelea afrika sana
jk akiangalia nguo za kitamaduni katika banda la maonyesho la afrika sana siku alipofungua mkutano wa kimataifa wa utalii na safari wa africa travel association (ata) a-taun jana. mkurugenzi wa afrika sana mwafrika merinyo yuko pembeni akifurahia ugeni huo

 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
kumbukumbu ya mv bukoba
mnara wa kumbukumbu ya ajali ya mv bukoba uliojengwa maeneo ya bwiru, mwanza
mdau miriam makalla wa chuo kikuu mtakatifu agostino huko nyegezai mwanza katutumia picha hizi kutukumbusha waliopoteza maisha katika ajali ya mv bukoba iliyotokea miaka takriban 12 iliyopita
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
vazi la taifa
hili ni vazi la kitaifa kwa kinamama
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 26
wapi hapa
kwa kukusaidia hii sehemu ipo dar, na sio a-taun...
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 15
simba

kwenye ukumbi wa simba katika aicc kuna bonge la simba mlangoni. halafu wala haumi...
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 9
mwili wa mama mary mackeja wawasili nyumbani
MAREHEMU MARY MACKEJA AKISALIWA MARA BAADA YA MWILI WAKE KUWASILI KATIKA UWANJA WA NDEGE WA JK NYERERE JANA. KUTOKA KUSHOTO NI NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI ALHAJ KAGASHEKI, WAZIRI MEMBE, NA WAZIRI WA ZAMANI NA MWANA DIPLOMASIA MSTAAFU SIR GEORGE KAHAMA
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 13
nyumbani ni nyumbani
Wadau wenzangu ni imani yangu kuwa mtakubaliana nami kuwa asilimia kubwa ya wakazi wa mijini tulitokea vijijini tena kwenye makazi ya kawaida kabisa ila wengi tunajisahau hata hatukumbuki tulikotoka mimi nimeamua kuwafahamisha wadau wenzangu mahali nilipozaliwa hukoooo...Thuji milima ya upare ;Karibuni sana .Kuna umeme,mitandao yasimu,maji safi ya bomba bila kusahau makande hata mtandao wa google unatambua kijiji chetu andika neno SUJI KISHA SEARCH
Mdau baba Jordan
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 11
fulanazzzz
Mdada Susan Evans wa Bedfordshire university Luton akivunja guiness book of records for wearing the most T shirts in just under 4 hrs jana .Total T shirts 230! Looking on are Mayor of Luton, Norris Bullock, and Tanzania's Deputy High Commissioner to UK Chabaka Kilumanga
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
msiba dar
DEATH ANNOUNCEMENT
The family of Brigadier General (Rtd), William S. Kotta Sr. Sadly announces the untimely demise of their beloved Mom, Mrs Margaret Mdakie Kotta that occurred on Sunday 18th May 2008 at Lugalo Military Hospital.
Mrs Margaret Mdakie Kotta the wife of Brigadier General (Rtd) William s. Kotta Sr. Mother to Steve Kotta Jr, Capt. Yves Kotta, Genevieve Kotta Kasanga and Faraja Kotta Nyalandu, Mother in law to Isaack Kasanga, Hon. Lazaro Nyalandu, Rhoda Memba Kotta and Charlotte Rukia Kotta. Grandmother to Leroy Kotta III, Lorna Kotta and Clarrisa Kasanga.
She is Deeply Missed by her family.
Funeral will be held on Wednesday, 21st May 2008.
Funeral Arrangements are taking place at Brigadier General (Rtd), William S. Kotta's home at Kunduchi Kilongawima, Dar es Salaam.
Mama Kotta's funeral will be held on Wednesday at her Mbezi Luisi shamba in the outskirts of Dar es salaam
May the Lord, rest her soul in eternal peace
Amen
 
© Michuzi Tarehe: 20.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 15
May 19, 2008
mambo ya a-taun
niko na mdau deo mushi ambaye ni mwakilishi w daily news a-taun leo. niko huku kwa muda, napata mambo elekezi kwa jamu
 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 25
nondozzzz uturuki

Pole sana na kazi bro!
Ningependa kukutumia picha zangu za graduation iliyofanyika hapa Turkey tarehe 17 may 2008.Naomba uwakilishe kwenye blog yetu ya jamii.Napenda kumshukuru Mungu kwa kunisaidia kujinyakulia degree yangu ya udaktari.Mungu ajaalie na watanzania wote wafanikiwe katika elimu.Sasa naitwa rasmi Dr.Lydenge nikiwa katika picha hapo ya pamoja na Mama yangu na aunt yangu ambapo hawakuweza kuacha kujumuika nami kwenye tafrija hii hapa ubatani.

Kazi njema.
 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 25
libeneke la sama

 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
david beckham kutia timu bongo?
Sema mjomba misupu..
ebwana leo wakati napitia nyuzi za duniani nimekutana na hii habari njema kwa sekta yetu ya utalii kuhusiana na mjomba bekham na babu bono kutaka kuja bongo.
Haki ya nani media yetu ikishindwa kutumia hii chance kuutangaza mlima wetu nitawacheka.
Hebu gonga hapo usome mwenyewe kama vipi wajuze na wadau.
 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
sauzi yawa jehanamu kwa wahamiaji

Habari za kazi Kaka!

Naomba nikupatie hii taarifa lakini mimi siyo mtaalamu wa haya mambo hivyo naomba usiweke jina langu.
Pamoja na kuwa mnatupatia taarifa nyingi nono tu, nimekuletea taarifa hii ili wasomaji wako wengi wawezi elewa kuwa sasa hivi Afrika Kusini kuna moto. Wenzetu hawa wametengeneza chuki ya ajabu kwa wageni wanaotoka nchi zaafrika (weusi), wanawauwa na kuwachoma moto na polisi wana kazi nzito ambayoinaonekana inawashinda.


picha nimeambatanisha inatoka hapa http://photos.mg.co.za/view_photo.php?pid=3446&gid=225 na kuna taarifa nyingi mtandaoni.
watu wengi (wageni wa kiafrika - weusi)sasa wanalala vituo vya polisi kuogopa kuuliwa na hawa ndugu zetu.

pia taarifa zaidi zipo hapa:
breaking_news__national
 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 43
profesa kamuzo atema cheche juu ya teknohama
profesa faustin kamuzora, ambaye ni makamu mkuu wa chuo cha mzumbe, leo ametema cheche kwenye mkutano wa kimataifa wa utalii na safari jijini a-taun kwa kusema bongo inabidi wafunge mikanda katika teknohama ama sivyo wataachwa solemba na wengine duniani. ametoa mifano kadhaa lakini kubwa na la ukweli ni kushindwa kwa taaisi kuwa na website na kama wanazo hawazi up-date kila siku na kdhalika. kasema bongo inapitwa na wengine kwa kuwa kila mtu nimbumbu kwenye mtandao.wadau mnaizungumziaje mada hii?

 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 18
ukumbi wa simba, aicc
baada ya ukarabati wa kufa mtu, ukumbi wa mikutano wa simba wa arusha international conference centre (aicc) waonekana hivi sasa. hii ni leo wakati jk alipokuwa anafungua mkutano wa siku tatu wa kimataifa wa africa travel association (ata). mkutano wa sullivan utafanyika hapa pia kuanzia juni 2 hadi juni 6, 2008.

 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 12
miss tz EU 2008
Vituo kwa washiriki
Miss Tanzania EU 2008 Germany



Form na maelezo kwa wale watakaoshiriki Miss Tanzania EU 08 zinaendelea kupatikana kwa:-

HOLLAND & BELGIUM - Charles Gadi Promotions
+31634236408
Charlesmwagadi@yahoo.com
au
DJ Gtown (turntable)
Georgesimba60@hotmail.com

NORWAY – Hassan Nganzo
+4747262181
Nganzo88@yahoo.no

DENMARK – Msimbazi
+4540958552
jumuiatz@hotmail.com

FINLAND – Bantu
Salnee@hotmail.com

FRANCE - Bruno
bruno_bcbg@hotmail.com

Others –
info@misstanzania.eu
+49 1520 5880 863

Mshindi wa kinyangányiro hichi hapo 28.06.08 nchini Germany atajiunga na warembo wengine katika shindano la kitaifa mjini Dar es saalam mwezi August.
www.misstanzania.eu
 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
Miriam Chemmoss aendeleza lieneke

Endapo kuchanganya utaifa,damu na tamaduni mbalimbali ni mojawapo ya chachu za mafanikio fulani hapa duniani, basi ushahidi wa dhana hiyo unaweza kuupata kwa kuangalia maisha ya mrembo Miriam Chemmoss(pichani).


Miriam ni muigizaji,mwimbaji,mtunzi wa nyimbo na pia mwanamitindo (model) ambaye mpaka hivi leo ana haki ya kusimama na kujivunia rekodi yake katika ulimwengu changamani wa sanaa na maonyesho.Mwenyewe anasema safari yake ndio kwanza inaanza kwani bado ana ndoto na malengo chungu mbovu ya kutimiza.Hivi leo kazi zake nyingi anazifanyia kutokea jijini New York nchini Marekani anapoishi. habari kamili nenda http://bongocelebrity.com/
 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
ndege za ATC
leo wakati napaa kwenda nanihii kwa semina elekezi nimebahatika kukuta madege yote ya atc yakiwa yamepaki uwanja wa julius nyerere. kunradhi kioo cha dirisha nililoketi hakikuwa safi
 
© Michuzi Tarehe: 19.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 13
May 18, 2008
msiba na mazishi copenhagen

FUNERAL OF LATE ABDALLAH KHAMIS

NAOME KASOZI WIFE OF THE HANDSOME LATE ABDALLAH KHAMIS MUSSA WHO HAILS FROM UGANDA AND BROTHER MUSSA BAUCHA WHO HAILS FROM ZANZIBAR - TANZANIA WISH TO INVITE ALL MEMBERS OF THE FAMILY AND FRIENDS WHO WISH TO JOIN OUR SORROWFUL HOLY EVENT WHICH STARTS AT 12.00 HRS,TUESDAY, 20 -05- 2008

AT:THE HOLY MOSQUE
AMERIKAVEJ 19
1756 COPENHAGEN V
BUS 6A






LATER SAME DAY TUESDAY, 20 -05- 2008,

AT 14.45 PM
FINAL FUNERAL EVENT WILL TAKE PLACE
AT: GRAVE YARD
VESTER KIRKE ALLE,
1756 COPENHAGEN
VJÆLØR STATION
BUS 4A

FOR FURTHER INFORMATION PLEASE CONTACT:

MR MARK /NAOME + 45 3284480
MR MUSSA BAUCHER +45 61906867
MR BAHANI +4540104427

EXPECTED AT THE FAREWELL EVENT FOR THE LAST RESPECTS ARE BOTH THE EMBASSADOR OF UNITED REPUBLIC OF TANZANIA HON. DR. BEN MOSES AND THE EMBASSADOR OF UGANDA HON. JOSEPH TOMUSANGE






WE HUMBLY THANK OUR UNIFIED AND OUTSTANDING GREAT MORAL SUPPORTERS THROUGHOUT THIS DIFFICULT MOMENT FOR THE FAMILY .






MICKEY JOHN AMOS
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
lister elia alipokuwa orchestra sambulumaa
ORCHESTRA SAMBULUMAA...chini ya uongozi wa Nguza Viking (gitaa begani),ni moja ya bendi zilizotingisha anga la muziki Tanzania miaka ya 90. Hapa wana Sambulumaa wakiwa kwenye mazoezi ya mwisho kabla ya kujimwaga kwenye shoo yao ya kwanza Diamond Jubilee. lister elia ni huyo aliyesimama wa tatu toka kulia. wa mwanzo kulia ni king kikii

Lister Elia(kati) ni miongoni mwa waanzilishi wa bendi ya Sambulumaa,alishiriki katika ukung'utaji wa keyboards nyimbo zote za wana Sambulumaa kama "Kadiri Kasimba" utunzi wa Kianga Songa,"CCM imekua" utunzi wake Skassy Kasambula na "Mama Happy" utunzi wake mwenyewe Lister Elia.


Kwa sasa Lister anaendeleza libeneke katika jiji la Tokyo ambako anaishi na kufanya kazi kama mpiga kinanda wa kulipwa na pia Lister ndiye mtunzia wa vitabu viwili vinavyohusu upigaji wa vyombo vya muziki kama Piano na Gitaa.


Kitabu chake cha tatu ambacho ni cha riwaya(novel) kinachoitwa "The mystery of Tamko's death,ambacho ni cha kiingereza na kimetafsiriwa pia kwa kiswahili kipo mitamboni kuchapwa na kinatarajiwa kutoka baada ya muda si mrefu.


Tembelea tovuti ya kijana huyu ugundue mengi. http://www.listerelia.com/



 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 11
mama kikwete shambani
Mama Salma Kikwete akikagua shamba la mpunga lililolimwa kwa kutumia mbinu bora na kanuni za kilimo muda mfupi kabla ya kufunga Mafunzo ya shamba Darasa kwa wakulima wa Msoga wilayani Bagamoyo leo
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
pinda akiwa misri
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Misri, Dr Abuu Zeid (kushoto) na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk. Cyril Chami (kulia) nje ya ukumbi wa mikutano wa kituo cha Sharm El Shikh nchini Misri leo. Watatu kushoto ni balozi Mohamed Mzale, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
salamu toka moscow
Mheshimiwa bro Michuzi!

wadau huku haruna budi kukualika rasmi wewe, familia yako na watanzania wenzangu huku Moscow(RUSSIA) kushuhudia fainali ya champions league ya club bora zinazotisha ambazo zimeweka historia kuwa timu mbili za uingereza kukutana fainali kwa mara ya kwanza kwenye mchuano huo.
yaani lazima tujimwage uwanjani hata kama masomo ya udaktari yanatuweka bize kidogo. Pia nawapa hongera wahitimu vipaji wa Mzumbe secondary form 6 kwa kuendeleza libeneke la kufaulu na itupe raha kwa sisi tuliohitimu miaka iliopita.
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 9
athumani iddi 'chuji'
huyu ndiye athumani iddi 'chuji' aliyefunga bao muhimu jana taifa staaz ilipotoka 1-1 dhidi ya uganda huko kampala na kuisongesha mbele timu yetu kwenye michuano ya kwanza ya afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani. staaz imepita ngwe hiyo kwa mabao 3-1 baada ya kushinda katika mchezo wa kwanza uliofanyika uwanja wa ccm kirumba kwa magoli 2-0, mabao yaliyofungwa na emmanuel gabriel na shabani nditi.
staaz imeweza kuweka rekodi ya kihistoria katika soka kwani hayo ni mafanikio ya kwanza katika ardhi ya waganda tangu mwaka 1984, ikiwa ni miaka 24 baada ya Stars kushinda kwenye uwanja wa Nakivubo.
katika mchezo huo staaz iliyoundwa na juma pondamali, mohamed bakari 'tall', jellah mtagwa, juma mkambi 'jenerali', makumbi juma 'homa ya jiji', charles boniface mkwasa 'master', zamoyoni mogella 'golden boy' iliibuka na ushindi wa mabao 3-0, ikiwa ni baada ya kufungwa nyumbani bao 1-
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 18
vichwa vya habari
msaada kwenye tuta wadau. nna hamu ya kujua maana ya hivyo vichwa vya habari maana kama mjuavyo mie kiinglishi ndio hivyo tena..
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 22
msiba ujerumani na moshi

Familia ya Mzee Wilfred Shangali wa Moshi Kilimanjaro, ina majonzi makubwa na inatangaza kifo cha mpendwa wao Pius Wilfred Shangali, kilichotokea tarehe 30/04/2008 huko Dresden, Ujerumani.

Marehemu aliugua maradhi ya mapafu.

Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kutoka Ujerumani inafanywa na inatarajiwa kuwa mwili utawasili siku ya jumatano tarehe 21/05/2008 katika uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA).

Mipango ya mazishi inaendelea kupangwa na taarifa kamili itatolewa, mara tu mwili utakapowasili nchini.

Marehemu Pius alizaliwa tarehe 18/09/1976 huko Mwanza.

Alisoma secondary (O-Level) katika shule za sekondari za Mawenzi-moshi na Magamba-Lushoto, kati ya miaka ya 1991 - 1994.

Baada ya kumaliza masomo ya O-Level alijiunga na sekondari ya Tanga (Tanga School) kati ya miaka ya 1995 – 1997.

Alijiunga na chuo kikuu Dar es salaam katika kitivo cha uhandisi mwaka 1998 na kuhitimu shahada ya uhandisi mwaka 2002.

Alikwenda Ujerumani kusomea shahada ya pili ya uhandisi wa maji mnamo mwaka 2005.

Kwa salamu za rambirambi wasiliana kwa namba za simu zifuatazo
Wilfred Shangali (0784535030), Dr. Theophil W. Shangali (0767101012),
Christa W. Shangali (0714125000)

Tulimpenda Pius Lakini Mungu Amempenda Zaidi
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIBARIKIWE
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 8
msaada tutani
Mr. Supu!!
Sometimes, at the small hours, we get so down that we need to fume it out.I am down and low. At the same time, have to serve the Satan to get my daily bread (night boxes).This is where you come in.
Will be so happy to hear from people I have not seen for many, many years.Those are people who the name “Sly Robbins” rings a bell. Since we gate crashed together a lot, these following old hits should bring many good gone feelings:
2.
Will appreciate if you post this massage in your blog kama msaada tutani And they can get hold of me on:
Thanx in advance
Blackmpingo
aka Sly Robbins
 
© Michuzi Tarehe: 18.5.08 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
May 17, 2008
BREKING NYUUUUUZZZZZZZZZ
TAIFA STAAAZ IMEFANIKIWA KUVUKA KIGINNGI CHA KUSAKA TIKETI YA KUSHIRIKI FAINALI ZA KWANZA ZA MATAIFA YA AFRIKA KWA WACHEZAJI WANAOCHEZA LIGI ZA NYUMBANI MAARUFU KAMA CHAN BAADA YA KUILAZIMISHA SARE YA 1-1 TIMU YA UGANDA CRANES UWANJA WA NAKIVUBO HUKO UKWENI.
GOLI LA STAA LIMEPATIKANA DAKIKA YA 44 MFUNGAJI AKIWA ATHUMANI IDDI 'CHUJI'
HII NDO KUSEMA STAAZ INAPETA KWA MABAO 3-1 BAADA YA USHINDI WA 1-0 ILIYOPATA IKIWA NYUMBANI WIKI MBILI ZILIZOPITA. SASA TUNAMNGOJA MSHINDI KATI YA SUDAN NA RWANDA AMBAPO TUKIMSHINDA TUNAINGIA FAINALI YA KOMBE HILO ZITAZOFANYIKA IVORY COAST MAPEMA MWAKANI.
 
© Michuzi Tarehe: 17.5.08