Mkuu wa wilaya ya Kilwa, Abdala Ulega amewakata watendaji na watoa
huduma wilayani humo kuhakikisha huduma muhimu za matibabu hasa dawa
zinapatina muda wote ili kuboresha huduma wilayani hapo.
Ulega ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya
uhamasiahaji wananchi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa taifa wa bima ya afya katika halmashauri kumi
nchi nzima iliyozinduliwa kata ya Tingi njia nne wilayani kilwa.
Ulega amesema Serikali kupitia mfuko wa uchangiaji wa bima ya afya
(NHIF) na mfuko wa afya ya jamii (CHF) imetoa fursa kwa wamiliki wa
vituo vya matibabu na watoa huduma kutumia fedha za uchangiaji huduma
kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vitendanishi kwa ajili ya kuboresha
huduma kwa wananchi na kwamba fedha hizo sio za kulipana posho katika
vikao.
Awali, Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Bima ya Afya, Rehani Athumani
alimweleza Mkuu huyo wa Wilaya kuwa kampeni hiyo iliyozinduliwa
leo itafanyika katika halmashauri nyingine kumi na hivyo kufanya jumla ya
halmashauri zilizohamasishwa nchi nzima kufikia 74 katika
mwaka wa fedha wa 2014/15.
Rehani alizitaja halmashauri hizo kuwa ni Kilwa, Ruangwa, Ulanga, Korogwe na
Rufiji. Nyingine tano ambazo huduma za mfuko wa CHF zitaanzishwa na
kuhamasishwa katika kampeni hii ni Halmashauri ya Kaliua, Kakonko,
Ushetu na Itirima.
Naye mwakilishi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Mtandao wa Mifuko
ya Afya ya Jamiii nchini (TNCHF), Kidani Mhenga aliwaahidi
wananchi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuendelea kushirikiana nao katika
kutatua changamoto mbalimbali ili kuboresha huduma za matibabu kupitia Mfuko wa Afya wa Jamii katika mikoa hiyo.
Aliomba ushirikiano wa
wananchi kwa ujumla kwani mafanikio ya utekelezaji wa huduma za mfuko
huo zinategemea ushiriki wa wananchi katika kuchangia na kusimamia
huduma.
Hadi tarehe 31 machi, 2015 mfuko wa afya ya jamii ulikuwa umeandikisha
jumla ya kaya 930,879 sawa na wanufaika 5,85,274.
Mkuu
wa wilaya ya Kilwa, Abdallah Ulega akizungumza na Wananchi wa Kijiji
cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilayani Kilwa, wakati uzinduzi wa awamu ya
pili ya kampeni ya
uhamasiahaji kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF)
inafanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika halmashauri
kumi
nchi nzima.
Mkurugenzi
wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Rehani Athumani
akielezea namna kampeni hiyo inavyofanyika katika halmashauri nyingine
kumi na hivyo kufanya jumla ya
halmashauri zilizohamasishwa nchi nzima kufikia halmashauri 74 katika
mwaka wa fedha wa 2014/15, katika uzinduzi uliofanyika leo katika
Kijiji cha Njia Nne, Kata ya Tingi wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi.
Mkuu
wa wilaya ya Kilwa, Abdallah Ulega (kushoto) akipokea sehemu ya mashuka
150 kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Bima ya Afya
(NHIF), Rehani Athumani(kulia) kwa ajili ya Zahanati za Wilaya ya
Kilwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...