Lori la Mizigo lenye namba za usajili T 112 BAL lililokuwa na tela lenye namba za T 108 AVT likiwa halitamaniki baada ya kupata ajali alfajiri ya leo kwenye kijiji cha Kitumbi, Wilayani Handeni Mkoa wa Tanga. Kwa mujibu wa utingo wa lori hilo, aliefahamika kwa jina la Makeke Moses, amesema kuwa kutokea kwa ajali hiyo kulisababishwa na Lori lingine (halipo pichani) lililokuwa limeharibika na kusimama katikati ya barabara bila ya kuwa na ishara yeyote ya tahadhali, hali iliyompelea dereva wake kutumia maarifa yake ya kiudereza ili kulikwepa lori hilo, lakini maarifa hayo hayakuzaa matunda na kujikuta wakitoka kando ya barabara mpaka kufikia hapo. hakuna aliepoteza maisha katika ajali hiyo.
 Kichwa cha lori hilo kikiwa pembeni baada ya kutolewa.
 Zoezi la ufaulishaji mizigo likaanza na hapo barabara ikafungwa kwa muda ila kufanikisha zoezi hilo.
 Baadhi ya Matingo wa malori mengine wakimjulia hali Utingo mwenzao alienusurika ajalini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 28, 2015

    Madereva muwe makini hivi vyombo vimeshatutia hasara sana ya nguvu kazi na mali za wenyenavyo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...