Msajili wa Bodi ya Wahandisi nchini Tanzania(ERB) Muhandisi Steven Mlope akiongea na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam kuelezea mafanikio ya Bodi hiyo katika kipindi cha miaka 10 hasa ukuzaji wa sekta ya ajira nchini Tanzania.

NA.Aron Msigwa - MAELEZO.

Bodi ya Usajili wa Wahandisi nchini Tanzania (ERD) imefanikiwa kutengeneza ajira 1600 kwa Watanzania kufuatia usajili wa makampuni 160 ya ushauri wa kihandisi yaliyoanzishwa nchini kote nchini katika kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2005 hadi 2015.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuelezea mafanikio ya Bodi hiyo kwa kipindi cha miaka 10 Msajili wa Wahandisi nchini Tanzania (ERB) Muhandisi Steven Mlope amesema kuwa kwa kusajili makampuni 160 katika kipindi cha miaka 10 pia wamefanikiwa kusajili wahandisi wapatao 8496 ambao kwa ujumla wao wametengeneza ajira kwa Watanzania 256,480.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...